< Hesabu 31 >

1 BWANA alinena na Musa na kumwambia,
The LORD spoke to Moses, saying,
2 “Uwalipizie kisasi Wamidiani kwa kile walichowafanya Waisraeli. Baada ya kufanya hivyo utakufa na kukusanyika na watu wako.”
“Avenge the children of Israel on the Midianites. Afterward you shall be gathered to your people.”
3 Kwa hiyo Musa akawaambia watu. Akasema, “andaeni baadhi ya majeshi yenu kwa ajili ya vita ili kwamba wakawapige Wamidiani na kubeba kiapo cha BWANA.
Moses spoke to the people, saying, “Arm men from amongst you for war, that they may go against Midian, to execute the LORD’s vengeance on Midian.
4 Kwa kila kabila la Israeli watatuma askari elfu moja kwa ajili ya vita.”
You shall send one thousand out of every tribe, throughout all the tribes of Israel, to the war.”
5 Kwa hiyo kati ya wanaume maelfu elfu wa Israeli, wanaume elfu moja walitolewa kwa ajili ya vita, jumla ya wanaume elfu kumi na mbili.
So there were delivered, out of the thousands of Israel, a thousand from every tribe, twelve thousand armed for war.
6 Kisha Musa akawatuma kwenda vitani, elfu moja toka kila kabila pamoja na Finehasi mwana wa Eliazari kuhanai, wakiwa na vitu kutoka mahali patakatifu wakiwa na matarumbeta kwa ajili ya ishara za sauti.
Moses sent them, one thousand of every tribe, to the war with Phinehas the son of Eleazar the priest, to the war, with the vessels of the sanctuary and the trumpets for the alarm in his hand.
7 Wakapigana na Midiani, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa. Wakamwua kila mwanaume.
They fought against Midian, as the LORD commanded Moses. They killed every male.
8 Wakawaua wafalme wa Midiani pamoja na wengine waliowaua ni: Evi, Rekimu, Zuri, Huri, na Reba, hawa walaikuwa ndio waflme watano wa Midiani. pia walimwua Balaamu mwana wa Beori, kwa upanga.
They killed the kings of Midian with the rest of their slain: Evi, Rekem, Zur, Hur, and Reba, the five kings of Midian. They also killed Balaam the son of Beor with the sword.
9 Jeshi la Israeli likawachukua mateka wanawake wa Midiani, watoto wao, mifugo yao yote, kondoo wao na bidhaa zao zote. walivichukua hivi kama mateka.
The children of Israel took the women of Midian captive with their little ones; and all their livestock, all their flocks, and all their goods, they took as plunder.
10 Waliichoma moto miji yao yote walimoishi na kambi zao zote.
All their cities in the places in which they lived, and all their encampments, they burnt with fire.
11 Walichukua vitu vyote na wafungwa, watu na wanyama.
They took all the captives, and all the plunder, both of man and of animal.
12 Wakawaleta mateka, nyara, na wakakamata vitu wakavileta kwa Musa, na Eliazari kuhani, na kwa jamii ya watu wa Israeli. Wakavileta hivi vitu kambini katika uwanda wa Moabu, kule Yorodani karibu na Yeriko.
They brought the captives with the prey and the plunder, to Moses, and to Eleazar the priest, and to the congregation of the children of Israel, to the camp at the plains of Moab, which are by the Jordan at Jericho.
13 Musa, Eliazari kuhani, pamoja na viongozi wa watu wakaenda kukutana nao nje ya kambi.
Moses and Eleazar the priest, with all the princes of the congregation, went out to meet them outside of the camp.
14 Lakini Musa alikuwa na hasira dhidi ya viongozi wa jeshi, Wale majemedari wa maelfu na maakida wa mamia, waliotoka kupigana.
Moses was angry with the officers of the army, the captains of thousands and the captains of hundreds, who came from the service of the war.
15 Musa akawaambia, “Je, mmeawaacha wanawake wote kuishi?
Moses said to them, “Have you saved all the women alive?
16 Tazama, wanawake hawa ndio waliosababisha watu wa Israeli, kwa kupitia ushauri wa Balaamu, kufanya dhambi dhidi ya BWANA huko Peori, wakati ile tauni iliposambaa kwa watu wa Mungu.
Behold, these caused the children of Israel, through the counsel of Balaam, to commit trespass against the LORD in the matter of Peor, and so the plague was amongst the congregation of the LORD.
17 Sasa basi, ueni kila mwanaume kuanzia wadogo, na ueni kila mwanamke aliyelala na mwanamume.
Now therefore kill every male amongst the little ones, and kill every woman who has known man by lying with him.
18 Lakini chukueni wale mabinti wadogo ambao hawajalala na mwanamume.
But all the girls, who have not known man by lying with him, keep alive for yourselves.
19 Mtaweka kambi nje na kambi za Israeli kwa muda wa siku saba. Ninyi wote ambao mmeua watu au ambao mmegusa maiti yeyote mtajitakasa wenyewe katika siku ya tatu na katika siku ya saba - ninyi na mateka wenu.
“Encamp outside of the camp for seven days. Whoever has killed any person, and whoever has touched any slain, purify yourselves on the third day and on the seventh day, you and your captives.
20 Na mtayatakasa mavazi yenu yote, na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi za wanyama, na manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao.”
You shall purify every garment, and all that is made of skin, and all work of goats’ hair, and all things made of wood.”
21 Eliazarai kuahani akawaambia wale wanajeshi waliokuwa wameenda vitani, “Hii ni amri ya sheria ambayo BWANA alimpa Musa:
Eleazar the priest said to the men of war who went to the battle, “This is the statute of the law which the LORD has commanded Moses.
22 Zile dhahabu, fedha, vyuma, bati, risasi,
However the gold, and the silver, the bronze, the iron, the tin, and the lead,
23 na kila kitu knaweza kuhhimili moto, mtakiweka katka moto, navyo vitakuwa safi. Nakisha mtavitakasa vitu hivyo na maji ya farakano. Na vitu vyote ambavyo haviwezi kupita katika moto, mtavitakasa kwa maji hayo.
everything that may withstand the fire, you shall make to go through the fire, and it shall be clean; nevertheless it shall be purified with the water for impurity. All that doesn’t withstand the fire you shall make to go through the water.
24 Na mtazifua nguao zenu katika siku ya saba, ndipo mtakapokuwa safi. Baada ya hapo mnaweza kurudi kwenye kambi za Israeli.”
You shall wash your clothes on the seventh day, and you shall be clean. Afterward you shall come into the camp.”
25 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
The LORD spoke to Moses, saying,
26 “Vihesabu vitu vyote vilivyochukuliwa nyara, wote watu na wanyama. Wewe, Eliazari kuhani, na viongozi wa watu kufuata koo
“Count the plunder that was taken, both of man and of animal, you, and Eleazar the priest, and the heads of the fathers’ households of the congregation;
27 watavigawa hivi vitu katika mkundi mawili. Mvigawe kwa wanajeshi walioenda kupigana na kwa watu wote.
and divide the plunder into two parts: between the men skilled in war, who went out to battle, and all the congregation.
28 Kisha toza kodi ambayo itatolewa kwangu kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wameenda vitani. Hii kodi itakuwa moja kati ya mia tano, katika watu, ng'ombe, punda, kondoo, au mbuzi.
Levy a tribute to the LORD of the men of war who went out to battle: one soul of five hundred; of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks.
29 Uichukue hii kodi kutoka katika nusu yao na umpe Eliazari kuhani kwa ajili ya sadaka itakayotolewa kwangu.
Take it from their half, and give it to Eleazar the priest, for the LORD’s wave offering.
30 Pia kutoka katika nusu ya watu wa Israeli, utachukua moja kati ya hamsini -kutoka vitu, ng'ombe, punda, na mbuzi. Uvitoe hivi kwa Walawi wanaotumika katika masikani yangu.”
Of the children of Israel’s half, you shall take one drawn out of every fifty, of the persons, of the cattle, of the donkeys, and of the flocks, of all the livestock, and give them to the Levites, who perform the duty of the LORD’s tabernacle.”
31 Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakafanya kama BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
Moses and Eleazar the priest did as the LORD commanded Moses.
32 Sasa zile nyara zilizokuwa zimebaki ambazo wanajeshi walikuwa wameteka zilikuwa kondoo 675, 000,
Now the plunder, over and above the booty which the men of war took, was six hundred and seventy-five thousand sheep,
33 maksai elfu sabini na mbili,
seventy-two thousand head of cattle,
34 punda elfu sitini na moja,
sixty-one thousand donkeys,
35 na wanawake elfu thelathini na mbili ambao walikuwa hawajalala na mwanamume yeyote.
and thirty-two thousand persons in all, of the women who had not known man by lying with him.
36 Ile hesabu ya nusu iliyokuwa imetunzwa kwa ajili ya wanajeshi ilikuwa kondoo 337, 000. Ile sehemu ya
The half, which was the portion of those who went out to war, was in number three hundred and thirty-seven thousand and five hundred sheep;
37 BWANA ya kondoo ilikuwa kondoo 675.
and the LORD’s tribute of the sheep was six hundred and seventy-five.
38 Maksai walikuwa elfu thelathini na sita ambayo kodi ya BWANA ilikuwa sabini na mbili.
The cattle were thirty-six thousand, of which the LORD’s tribute was seventy-two.
39 Punda walikuwa 30, 500 ambao sehemu ya BWANA ilikuwa sitini na moja.
The donkeys were thirty thousand and five hundred, of which the LORD’s tribute was sixty-one.
40 Watu walikuwa wanawake elfu kumi na sita ambao kodi ya BWANA ilikuwa thelathini na mbili.
The persons were sixteen thousand, of whom the LORD’s tribute was thirty-two persons.
41 Musa aliichukua ile kodi ambayo ilitakiwa kuwekwa sadaka kwa BWANA. Akampatia Eliazari kuhani, kama BWANA alivyomwamuru Musa.
Moses gave the tribute, which was the LORD’s wave offering, to Eleazar the priest, as the LORD commanded Moses.
42 Ile nusu ya watu wa Israeli ambayo Musa alikuwa ameichukua toka kwa wanawjeshi waliokuwa wameenda vitani -
Of the children of Israel’s half, which Moses divided off from the men who fought
43 ile nusu y a watu ilikuwa kondoo 337, 500,
(now the congregation’s half was three hundred and thirty-seven thousand and five hundred sheep,
44 maksai elfu thelathini na sita,
thirty-six thousand head of cattle,
45 punda 30, 500,
thirty thousand and five hundred donkeys,
46 na wanawake elfu kumi na sita.
and sixteen thousand persons),
47 Kutoka kwenye nusu ya watu wa Israeli, Musa alichukua moja katika hamsini, wote watu na wanyama. Aliwapa Walawi ambao huitumikia masikani ya BWANA, kama BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
even of the children of Israel’s half, Moses took one drawn out of every fifty, both of man and of animal, and gave them to the Levites, who performed the duty of the LORD’s tabernacle, as the LORD commanded Moses.
48 Kisha wale maakida wa jeshi, makamanda wa elfu na makapteni wa mamia, wakaja kwa Musa.
The officers who were over the thousands of the army, the captains of thousands, and the captains of hundreds, came near to Moses.
49 Wakamwambia, “watumishi wako wamewahesabu wanajeshi ambao wako chini yetu, hakuna hata mmoja wao aliyekosa.
They said to Moses, “Your servants have taken the sum of the men of war who are under our command, and there lacks not one man of us.
50 Tumemletea BWANA sadaka, ambayo kila mmoja amepata, vitu vya dhahabu, metali, timbi, pete za mhuri, vipini na vikuku, ili kujifanyia upatanisho kwa BWANA.”
We have brought the LORD’s offering, what every man found: gold ornaments, armlets, bracelets, signet rings, earrings, and necklaces, to make atonement for our souls before the LORD.”
51 Musa na Eliazari kuhani akapokea kutoka kwao dhahabu na vitu vyote vilivyotengenezwa kwa ufundi.
Moses and Eleazar the priest took their gold, even all worked jewels.
52 Vitu vyote vya sadaka ya dhahabu ambavyo walimpa BWANA- sadaka toka kwa makamanda wa maelfu na kutoka kwa makepteni wa mamia - vilikuwa na uzito wa shekeli 16, 750.
All the gold of the wave offering that they offered up to the LORD, of the captains of thousands, and of the captains of hundreds, was sixteen thousand and seven hundred and fifty shekels.
53 Kila mwanajeshi alikuwa ameteka nyara ya kila mtu kwa ajili yake.
The men of war had taken booty, every man for himself.
54 Musa na Eliazari kuhani wakazichukuazile dhahabu toka kwa makamanda wa maelfu na makepteni wa mamia. Wakavipeleka kwenye hema ya kukutania kama ukumbusho wa watu wa Israeli kwa BWANA.
Moses and Eleazar the priest took the gold of the captains of thousands and of hundreds, and brought it into the Tent of Meeting for a memorial for the children of Israel before the LORD.

< Hesabu 31 >