< Hesabu 29 >

1 Katika siku ya kwanza, ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Katika siku hiyo hamtafanya kazi zenu za kila siku. Itakuwa siku ya kupiga matarumbeta.
“‘In the seventh month, on the first day of the month, you shall have a holy convocation; you shall do no regular aboda ·service·: it is a day of blowing of shofarot ·ram horns· to you.
2 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ya kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja na wanakondoo dume saba wa mwaka mmoja, kila mmoja mkamilifu.
You shall offer a burnt offering for a pleasant aroma to Adonai: one young bull, one ram, seven male lambs a year old without defect;
3 Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya huyo fahari, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya huyo kondoo mume,
and their meal offering, fine flour mixed with oil, three tenths for the bull, two tenths for the ram,
4 na sehemu ya kumi ya kila hao wanakondoo waume saba.
and one tenth for every lamb of the seven lambs;
5 Na mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
and one male goat for a sin offering, to make atonement for you;
6 Toeni hizo sadaka katika mwezi wa saba kama nyongeza ya sadaka mtakazotoa kila mwanzo wa kila mwezi: pamoja na sadaka maalumu za kuteketezwa na sadaka za unga. Hizi zitakuwa nyongeza za sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji. Utakapokuwa ukiendelea na sadaka hizi, utakuwa ukitii kile kilichoamriwa kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa BWANA.
besides the burnt offering of the new moon, and its meal offering, and the continual burnt offering and its meal offering, and their drink offerings, according to their judgments, for a pleasant aroma, an offering made by fire to Adonai.
7 Siku ya kumi ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Mtajinyeneyekeza na hamtafanya kazi.
“‘On the tenth day of this seventh month you shall have a holy convocation. You shall afflict your souls. You shall do no kind of work;
8 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja mchanga ili kutoa harufu nzuri, kondoo mmoja mume, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
but you shall offer a burnt offering to Adonai for a pleasant aroma: one young bull, one ram, seven male lambs a year old; all without defect;
9 Pamoja na sadaka hizo utatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya fahari, sehemu mbili za kumi za kondoo dume mmoja,
and their meal offering, fine flour mixed with oil, three tenths for the bull, two tenths for the one ram,
10 na sehemu ya kumi ya efa moja kwa kila mwanakondoo wale saba.
one tenth for every lamb of the seven lambs:
11 Mtatatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya upatanisho. Hii itakuwa sadaka ya nyongeza ya upatanisho, ya sadaka ya kila siku ya kuteketezwa, pamoja na sadaka za unga, na sadaka zake za vinywaji.
one male goat for a sin offering; besides the sin offering of atonement, and the continual burnt offering, and its meal offering, and their drink offerings.
12 Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu lakumwabudu BWANA. Siku hiyo hamtafanya kazi za kila siku, na mtazitunza hizo sikukuu kwa muda wa siku saba kwa ajili ya BWANA.
“‘On the fifteenth day of the seventh month you shall have a holy convocation. You shall do no regular aboda ·service·. You shall keep a feast to Adonai seven days.
13 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ilikutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa mafahari wachanga kumi na tatu, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
You shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a pleasant aroma to Adonai: thirteen young bulls, two rams, fourteen male lambs a year old; all without defect;
14 Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembaba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa kila fahari katika hao kumi na tatu, sehemu mbili za kumi kwa kila hao kondoo dume wawili,
and their meal offering, fine flour mixed with oil, three tenths for every bull of the thirteen bulls, two tenths for each ram of the two rams,
15 na sehemu ya kumi ya efa ya hao wanakondoo kumi na nne.
and one tenth for every lamb of the fourteen lambs;
16 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa, sadaka yake ya unga, pamoja na sadaka za vinywaji.
and one male goat for a sin offering, besides the continual burnt offering, its meal offering, and its drink offering.
17 Siku ya pili ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi na mbili, kondoo dume wawili na wanakondoo dume kumi na mbili wa umri wa mwaka mmoja, wote wakamilifu.
“‘On the second day you shall offer twelve young bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
18 Pamoja nao mtatoa sadaka ya unga, na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na kwa ajili ya wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilvyoamriwa.
and their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
19 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kila siku, sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one male goat for a sin offering; besides the continual burnt offering, with its meal offering and their drink offerings.
20 Siku ya tatu ya kusanyiko, mtatoa sadaka mafahari kumi na moja, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
“‘On the third day eleven bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
21 Pamoja na hizo sadaka mtatoa sadaka ya unga na sdaka ya vinywaji kwa wale mafahari, kwa wale kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, utoe sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
22 Mtatoa sadaka beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya zile sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one male goat for a sin offering; besides the continual burnt offering, and its meal offering, and its drink offering.
23 Siku ya nne ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
“‘On the fourth day ten bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
24 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sdaka za vinywaji kwa wale mafahari, na kwa wale kondoo dume na kwa wale wanakodoo, mtatoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
25 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji
and one male goat for a sin offering; besides the continual burnt offering, its meal offering, and its drink offering.
26 Siku ya tano ya kusanyiko, mtatoa mafahari tisa, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
“‘On the fifth day nine bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
27 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na wale wanakondoo, mkitoa sdaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
28 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka za vinywaji.
and one male goat for a sin offering, besides the continual burnt offering, and its meal offering, and its drink offering.
29 Siku ya sita ya kusanyiko, mtatoa mafahari wanane, kondoo dume wawili, na wanakondoo kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
“‘On the sixth day eight bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
30 Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga nasadaka za vinywaji kwa wale mafahari, kondoo wa dume na wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
31 Mtatoa beberu kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku za kuteketezwa, sadaka zadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one male goat for a sin offering; besides the continual burnt offering, its meal offering, and the drink offerings of it.
32 Siku ya saba ya kusanyiko, mtatoa mafahari saba, kondoo dume saba, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
“‘On the seventh day seven bulls, two rams, fourteen male lambs a year old without defect;
33 Pamoja nao mtataengeneza sadaka ya unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, na kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
and their meal offering and their drink offerings for the bulls, for the rams, and for the lambs, according to their number, after the judgement;
34 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya vinywaji.
and one male goat for a sin offering; besides the continual burnt offering, its meal offering, and its drink offering.
35 Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko lingine makini. Hamtafanya kazi zenu za kila siku.
“‘On the eighth day you shall have a solemn assembly: you shall do no regular aboda ·service·;
36 Mtafanya sadaka za kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja, kondoo mmoja dume, na wanakondoo saba dume wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
but you shall offer a burnt offering, an offering made by fire, of a pleasant aroma to Adonai: one bull, one ram, seven male lambs a year old without defect;
37 Mtatoa sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji kwa ajili ya yule fahari, kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkifanya sadaka nyingi kadri ilivyoamriwa.
their meal offering and their drink offerings for the bull, for the ram, and for the lambs, shall be according to their number, after the judgement:
38 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
and one male goat for a sin offering, besides the continual burnt offering, with its meal offering, and its drink offering.
39 Hivi ndivyo utakavyotoa sadaka kwa BWANA katika sikukuu zenu za kila mwaka. Hivi vitakuwa nyongeza ya viapo vyenu na sadaka zenu za hiari. Mtavitoa hivi kama sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za unga, sadaka za vinywaji, na sadaka za amani.”
“‘You shall offer these to Adonai in your set feasts, besides your vows, and your free will offerings, for your burnt offerings, and for your meal offerings, and for your drink offerings, and for your peace offerings.’”
40 Musa aliwaambia wana wa Israeli kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwamuru kusema.
Moses [Drawn out] told the children of Israel [God prevails] according to all that Adonai enjoined Moses [Drawn out].

< Hesabu 29 >