< Hesabu 11 >

1 Sasa watu wakanung'unika juu ya matatizo yao wakati BWANA alipokuwa akiwasikiliza. BWANA akawasikia watu naye akakasirika. Moto kutoka kwa BWANA ukashuka na ukawaka kati yao na kuteketeza baadhi ya kambi kwenye pembe zake.
And the people is evil, as those sighing habitually in the ears of Jehovah, and Jehovah heareth, and His anger burneth, and the fire of Jehovah burneth among them, and consumeth in the extremity of the camp.
2 Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
And the people cry unto Moses, and Moses prayeth unto Jehovah, and the fire is quenched;
3 Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
and he calleth the name of that place Taberah, for the fire of Jehovah hath 'burned' among them.
4 Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
And the rabble who [are] in its midst have lusted greatly, and the sons of Israel also turn back and weep, and say, 'Who doth give us flesh?
5 Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
We have remembered the fish which we do eat in Egypt for nought, the cucumbers, and the melons, and the leeks, and the onions, and the garlick;
6 Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
and now our soul [is] dry, there is not anything, save the manna, before our eyes.'
7 Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
And the manna is as coriander seed, and its aspect as the aspect of bdolach;
8 watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
the people have turned aside and gathered [it], and ground [it] with millstones, or beat [it] in a mortar, and boiled [it] in a pan, and made it cakes, and its taste hath been as the taste of the moisture of oil.
9 Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.
And in the descending of the dew on the camp by night, the manna descendeth upon it.
10 Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, na kila mtu alikuwa kwenye lango la hema yake. BWANA alikasirika sana, na mbele ya macho ya Musa malalamiko yao yalikuwa mabaya.
And Moses heareth the people weeping by its families, each at the opening of his tent, and the anger of Jehovah burneth exceedingly, and in the eyes of Moses [it is] evil.
11 Musa akasema na BWANA, “Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna hiyo? kwa nini hujapendezwa na mimi? unanifanya kubeba mizigo ya hawa watu.
And Moses saith unto Jehovah, 'Why hast Thou done evil to Thy servant? and why have I not found grace in Thine eyes — to put the burden of all this people upon me?
12 Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia, “wabebe kwa ukaribu vifuani mwako kama baba abebavyo mtoto wake? Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ambayo uliwaahidi mababu zao kuwapa?
I — have I conceived all this people? I — have I begotten it, that Thou sayest unto me, Carry it in thy bosom as the nursing father beareth the suckling, unto the ground which Thou hast sworn to its fathers?
13 Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa? Wanalia mbele zangu na wanasema, 'tupe nyama tule.'
Whence have I flesh to give to all this people? for they weep unto me, saying, Give to us flesh, and we eat.
14 Mimi peke yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa. Ni wengi sana kwangu.
I am not able — I alone — to bear all this people, for [it is] too heavy for me;
15 Kwa vile unanitendea hivi, basi uniue, na kama wewe ni mpole kwangu, basi niondolee mzigo huu.”
and if thus Thou art doing to me — slay me, I pray Thee; slay, if I have found grace in thine eyes, and let me not look on mine affliction.'
16 BWANA akamwambia Musa, “Niletee wazee sabini miongoni mwa Waisraeli. Hakikisha ni wazee na viongozi wa watu. Uwalete kwenye hema ya kukutania wasimame pamoja na wewe.
And Jehovah saith unto Moses, 'Gather to Me seventy men of the elders of Israel, whom thou hast known that they are elders of the people, and its authorities; and thou hast taken them unto the tent of meeting, and they have stationed themselves there with thee,
17 Nami nitashuka niseme nawe mahali pale. Nitatoa sehemu ya roho iliyo ndani yako na kuwapatia wao. Nao watabeba mzigo wa watu pamoja nawe. na hautaubeba peke yako.
and I have come down and spoken with thee there, and have kept back of the Spirit which [is] upon thee, and have put on them, and they have borne with thee some of the burden of the people, and thou dost not bear [it] thyself alone.
18 Waambie watu, 'Jitakaseni ninyi wenyewe, kwa kuwa kesho mtakuala nyama, kwa kuwa mmelia na BWANA amesikia, “Mlipokuwa mkisema kuwa nani atakayetupa nyama tule? Kule Misri tulikula chakula kizuri!” Kwa hiyo BWANA atawapeni nyama, nanyi mtakula nyama.
'And unto the people thou dost say, Sanctify yourselves for to-morrow, and ye have eaten flesh (for ye have wept in the ears of Jehovah, saying, Who doth give us flesh? for we [had] good in Egypt) — and Jehovah hath given to you flesh, and ye have eaten.
19 Hamtakula nyama kwa siku moja tu, au siku mbili, au siku tano, au siku kumi, au siku ishirini,
Ye do not eat one day, nor two days, nor five days, nor ten days, nor twenty days; —
20 Lakini mtakula nyama kwa mwezi mmoja mpaka zitakapowatokea puani. Mpaka zitawakinai kwa sababu mmemkataa BWANA ambaye yuko kati yenu. Mmelia mbele yake. mmesema, “Kwa nini tulitoka Misri?””
unto a month of days, till that it come out from your nostrils, and it hath become to you an abomination; because that ye have loathed Jehovah, who [is] in your midst, and weep before Him, saying, Why is this? — we have come out of Egypt!'
21 Kisha Musa akasema, “Mimi nina watu 600, 000, na wewe umesema, “Nitawapa nyama mle kwa mwezi mmoja,'
And Moses saith, 'Six hundred thousand footmen [are] the people in whose midst I [am]; and Thou, Thou hast said, Flesh I give to them, and they have eaten, a month of days!
22 Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuwatosheleza?”
Is flock and herd slaughtered for them, that one hath found for them? — are all the fishes of the sea gathered for them — that one hath found for them?'
23 BWANA akasema na Musa, “Je mkono wangu ni mfupi? Sasa utaona kama maneno yangu ni ya kweli ama sivyo.
And Jehovah saith unto Moses, 'Is the hand of Jehovah become short? now thou dost see whether My word meeteth thee or not.'
24 Musa alitoka nje kwenda kuwaambia watu maneno ya BWANA. Aliwakusanya wazee sabini wa watu na kuwaweka kuizunguka hema.
And Moses goeth out, and speaketh unto the people the words of Jehovah, and gathereth seventy men of the elders of the people, and causeth them to stand round about the tent,
25 BWANA akashuka chini katika wingu akaongea na Musa. BWANA akachukua sehemu ya roho iliyokuwa kwa Musa na kuiweka kwa wale wazee sabini. Roho alipowashukia, wakaanza kutoa unabii, lakini ilitokea kwenye tukio hilo tu na haikujirudia tena.
and Jehovah cometh down in the cloud, and speaketh unto him, and keepeth back of the Spirit which [is] on him, and putteth on the seventy men of the elders; and it cometh to pass at the resting of the Spirit on them, that they prophesy, and do not cease.
26 Watu wawili waitwao Elidadi na Medadi walibaki kambini. Lakini Roho aliwashukia pia. Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha lakini walikuwa hawajaenda hemani. Hata hivyo nao walitoa unabii wakiwa kambini.
And two of the men are left in the camp, the name of the one [is] Eldad, and the name of the second Medad, and the spirit resteth upon them, (and they are among those written, and have not gone out to the tent), and they prophesy in the camp;
27 Kijana mmoja huko kambini alikimbia akaenda kumwambia Musa, “Elidadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
and the young man runneth, and declareth to Moses, and saith, 'Eldad and Medad are prophesying in the camp.'
28 Joshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa, ambaye ni miongoni mwa wale aliowachagua akamwambia Musa, “Bwana wangu Musa, wazuie.”
And Joshua son of Nun, minister of Moses, [one] of his young men, answereth and saith, 'My lord Moses, restrain them.'
29 Musa akamwambia, “una wivu kwa niaba yangu? Natamani kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kwamba angeweka Roho yake juu yao wote!”
And Moses saith to him, 'Art thou zealous for me? O that all Jehovah's people were prophets! that Jehovah would put His Spirit upon them!'
30 Kisha Musa na wale wazee wakarudi kambini.
And Moses is gathered unto the camp, he and the elders of Israel.
31 Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA ukaja na kware kutokea baharini. Wakaanguka karibu na kambi, kiasi cha umbali wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine. Wale kware wakaizunguka kambi kiasi cha mita moja toka uso wa dunia.
And a spirit hath journeyed from Jehovah, and cutteth off quails from the sea, and leaveth by the camp, as a day's journey here, and as a day's journey there, round about the camp, and about two cubits, on the face of the land.
32 Watu wakawakusanya hao kware kwa bidii mchana huo wote na usiku huo wote, na mchana wote uliofuatia. Hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili za uajazo. Wakawaanika kweye ardhi yote hapo kambini.
And the people rise all that day, and all the night, and all the day after, and gather the quails — he who hath least hath gathered ten homers — and they spread them out for themselves round about the camp.
33 Wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno yao, wakiwa bado wanatafuna, BWANA akawakasirikia. Akwapiga watu wale kwa gonjwa kubwa sana.
The flesh is yet between their teeth — it is not yet cut off — and the anger of Jehovah hath burned among the people, and Jehovah smiteth among the people — a very great smiting;
34 Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava, kwa sababu pale walizika watu waliotamani nyama.
and [one] calleth the name of that place Kibroth-Hattaavah, for there they have buried the people who lust.
35 Kutoka Kibroti Hataava watu wakasafiri hadi Hazeroti, ambapo walipumzika.
From Kibroth-Hattaavah have the people journeyed to Hazeroth, and they are in Hazeroth.

< Hesabu 11 >