< Hesabu 10 >

1 BWANA alinena na Musa, akasema,
And the Lord said to Moses,
2 “tengenza tarumbeta mbili za fedha. Uzitengeneze kwa kufua hizo fedha. Utazitumia hizo tarumbeta kwa kuwaita watu waje pamoja na kwa kuwaita watu wote wakati wa kuondoka kwenye kambi zao.
Make two silver horns of hammered work, to be used for getting the people together and to give the sign for the moving of the tents.
3 Makuhani watapiga tarumbeta kwa ajili ya kuwaita watu wote mbele yako kwenye lango la hema ya kukutania.
When they are sounded, all the people are to come together to you at the door of the Tent of meeting.
4 Kama makuhani watapiga tarumbeta moja tu, basi viongozi, vichwa koo za Israeli ndipo watakapokutana kwako.
If only one of them is sounded, then the chiefs, the heads of the thousands of Israel, are to come to you.
5 Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu, ile kambi ya upande wa mashariki itaanza kusafiri.
When a loud note is sounded, the tents placed on the east side are to go forward.
6 Nawe utakapopiga tarumeta kwa sauti kuu mara ya pili, ile kambi ya upande wa kusini wataanza kusafiri. Watapiga tarumbeta kwa sauti kuu ili kuanza safari yao.
At the sound of a second loud note, the tents on the south side are to go forward: the loud note will be the sign to go forward.
7 Watu wote watakapokutana pamoja, piga hizo tarumbeta lakini si kwa sauti kuu.
But when all the people are to come together, the horn is to be sounded but not loudly.
8 Wana wa Haruni, makuhani, watapiga hizo tarumbeta. Huu ndio utakaokuwa utaratibu wa watu wako kwa vizazi vyote.
The horns are to be sounded by the sons of Aaron, the priests; this is to be a law for you for ever, from generation to generation.
9 Nanyi mtakapoenda vitani katika ardhi yenu dhidi ya maadui wenu wanaowakandamiza, ndipo mtakapotoa ishara ya sauti ya tarumbeta. Mimi, BWANA Mungu wako nitawaita kuwakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
And if you go to war in your land against any who do you wrong, then let the loud note of the horn be sounded; and the Lord your God will keep you in mind and give you salvation from those who are against you.
10 Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
And on days of joy and on your regular feasts and on the first day of every month, let the horns be sounded over your burned offerings and your peace-offerings; and they will put the Lord in mind of you: I am the Lord your God.
11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
Now in the second year, on the twentieth day of the second month, the cloud was taken up from over the Tent of witness.
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
And the children of Israel went on their journey out of the waste land of Sinai; and the cloud came to rest in the waste land of Paran.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
They went forward for the first time on their journey as the Lord had given orders by the hand of Moses.
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
First the flag of the children of Judah went forward with their armies: and at the head of his army was Nahshon, the son of Amminadab.
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
And at the head of the army of the children of Issachar was Nethanel, the son of Zuar.
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
And at the head of the army of the children of Zebulun was Eliab, the son of Helon.
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
Then the House was taken down; and the sons of Gershon and the sons of Merari, who were responsible for moving the House, went forward.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
Then the flag of the children of Reuben went forward with their armies: and at the head of his army was Elizur, the son of Shedeur.
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
And at the head of the army of the children of Simeon was Shelumiel, the son of Zurishaddai.
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
At the head of the army of the children of Gad was Eliasaph, the son of Reuel.
21 Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
Then the Kohathites went forward with the holy place; the others put up the House ready for their coming.
22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
Then the flag of the children of Ephraim went forward with their armies: and at the head of his army was Elishama, the son of Ammihud.
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
At the head of the army of the children of Manasseh was Gamaliel, the son of Pedahzur.
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
At the head of the army of the children of Benjamin was Abidan, the son of Gideoni.
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
And the flag of the children of Dan, whose tents were moved last of all, went forward with their armies: and at the head of his army was Ahiezer, the son of Ammishaddai.
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
At the head of the army of the children of Asher was Pagiel, the son of Ochran.
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
And at the head of the army of the children of Naphtali was Ahira, the son of Enan.
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
This was the order in which the children of Israel were journeying by armies; so they went forward.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
Then Moses said to Hobab, the son of his father-in-law Reuel the Midianite, We are journeying to that place of which the Lord has said, I will give it to you: so come with us, and it will be for your profit: for the Lord has good things in store for Israel.
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
But he said, I will not go with you, I will go back to the land of my birth and to my relations.
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
And he said, Do not go from us; for you will be eyes for us, guiding us to the right places in the waste land to put up our tents.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
And if you come with us, we will give you a part in whatever good the Lord does for us.
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
So they went forward three days' journey from the mountain of the Lord; and the ark of the Lord's agreement went three days' journey before them, looking for a resting-place for them;
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
And by day the cloud of the Lord went over them, when they went forward from the place where they had put up their tents.
35 Kila hilo sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema, “Inuka BWANA, Uwatawanye maadui wako. Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia.”
And when the ark went forward Moses said, Come up, O Lord, and let the armies of those who are against you be broken, and let your haters go in flight before you.
36 Na kila lile sanduku liliposimama, Musa alisema, “BWANA uwarudie, hawa Waisraeli makumi elfu.”
And when it came to rest, he said, Take rest, O Lord, and give a blessing to the families of Israel.

< Hesabu 10 >