< Nehemia 11 >

1 Viongozi wa watu waliishi Yerusalemu, na watu wengine walipiga kura ili kuleta mmoja kati ya watu kumi kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, na wengine tisa walibakia katika miji mingine.
And the rulers of the people dwelt at Jerusalem: the rest of the people also cast lots, to bring one of ten to dwell in Jerusalem the holy city, and nine parts [to dwell] in [other] cities.
2 Na watu wakawabariki wote waliojitoa kwa hiari kuishi Yerusalemu.
And the people blessed all the men that willingly offered themselves to dwell at Jerusalem.
3 Hawa ndio viongozi wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu. Hata hivyo, katika miji ya Yuda kila mtu aliishi katika nchi yake mwenyewe, ikiwa ni pamoja na Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu, na wazao wa watumishi wa Sulemani.
Now these [are] the chief of the province that dwelt in Jerusalem: but in the cities of Judah dwelt every one in his possession in their cities, [to wit], Israel, the priests, and the Levites, and the Nethinims, and the children of Solomon's servants.
4 Katika Yerusalemu waliishi baadhi ya wana wa Yuda na baadhi ya wana wa Benyamini. Watu wa Yuda walikuwa pamoja na Athaya, mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Peresi.
And at Jerusalem dwelt [certain] of the children of Judah, and of the children of Benjamin. Of the children of Judah; Athaiah the son of Uzziah, the son of Zechariah, the son of Amariah, the son of Shephatiah, the son of Mahalaleel, of the children of Perez;
5 Na Maaseya, mwana wa Baruki, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zakaria, mwana wa Mshelani, alikuwa mwana wa Baruki.
And Maaseiah the son of Baruch, the son of Col-hozeh, the son of Hazaiah, the son of Adaiah, the son of Joiarib, the son of Zechariah, the son of Shiloni.
6 Wana wote wa Peresi waliokaa Yerusalemu walikuwa 468. Walikuwa masujaa.
All the sons of Perez that dwelt at Jerusalem [were] four hundred sixty and eight valiant men.
7 Hao ndio wana wa Benyamini, Salu, mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseva, mwana wa Ithieli, mwana wa Yehaya.
And these [are] the sons of Benjamin; Sallu the son of Meshullam, the son of Joed, the son of Pedaiah, the son of Kolaiah, the son of Maaseiah, the son of Ithiel, the son of Jesaiah.
8 Na baada yake, Gabai na Salai, watu 928.
And after him, Gabbai, Sallai, nine hundred twenty and eight.
9 Yoeli mwana wa Zikri alikuwa mwangalizi wao; na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa mkuu wa pili juu ya mji.
And Joel the son of Zichri [was] their overseer: and Judah the son of Senuah [was] second over the city.
10 Kutoka kwa makuhani Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
Of the priests: Jedaiah the son of Joiarib, Jachin.
11 Seraya mwana wa Hilikia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayoti, mwana wa Ahitubu, mkuu wa nyumba ya Mungu,
Seraiah the son of Hilkiah, the son of Meshullam, the son of Zadok, the son of Meraioth, the son of Ahitub, [was] the ruler of the house of God.
12 na wenzake waliofanya kazi ya ukoo, watu 822. na Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amzi, ​​mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya.
And their brethren that performed the work of the house [were] eight hundred twenty and two: and Adaiah the son of Jeroham, the son of Pelaliah, the son of Amzi, the son of Zechariah, the son of Pashur, the son of Malchiah,
13 Nao walikuwa washirika wake waliokuwa wakuu wa jamaa, wanaume 242, na Maasai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri;
And his brethren, chief of the fathers, two hundred forty and two: and Amashai the son of Azareel, the son of Ahasai, the son of Meshillemoth, the son of Immer,
14 na ndugu zao, 128 wapiganaji wenye ujasiri, wenye ujasiri; Waziri wao aliyeongoza alikuwa Zabdieli, mwana wa Hageoli.
And their brethren, mighty men of valor, a hundred twenty and eight: and their overseer [was] Zabdiel, the son of [one of] the great men.
15 Na Walawi Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni,
Also of the Levites: Shemaiah the son of Hashub, the son of Azrikam, the son of Hashabiah, the son of Bunni;
16 na Shabethai, na Yozabadi, ambao walikuwa ni viongozi wa Walawi, waliosimamia kazi za nje ya nyumba ya Mungu.
And Shabbethai and Jozabad, of the chief of the Levites, [had] the oversight of the outward business of the house of God.
17 Alikuwepo Matania, mwana wa Mika, mwana wa Zakri, mwana wa Asafu, aliyekuwa mkurugenzi aliyeanza shukrani kwa sala, na Bakbukia, wa pili miongoni mwa ndugu zake, na Abda mwana wa Shemaya, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
And Mattaniah the son of Micha, the son of Zabdi, the son of Asaph, [was] the principal to begin the thanksgiving in prayer: and Bakbukiah the second among his brethren, and Abda the son of Shammua, the son of Galal, the son of Jeduthun.
18 Katika mji wote mtakatifu walikuwa Walawi 284.
All the Levites in the holy city [were] two hundred and eighty four.
19 Walinzi wa malango Akubu, Talmoni, na washirika wao, ambao waliolinda milango, wanaume 172.
Moreover the porters, Akkub, Talmon, and their brethren that kept the gates, [were] an hundred and seventy two.
20 Na wale waliosalia wa Israeli, na makuhani, na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda. Kila mtu aliishi katika milki yake mwenyewe.
And the residue of Israel, of the priests, [and] the Levites, [were] in all the cities of Judah every one in his inheritance.
21 Wafanyakazi wa hekalu waliishi Ofeli, na Siha na Gishpa walikuwa wakiwaongoza.
But the Nethinims dwelt in Ophel: and Ziha and Gispa [were] over the Nethinims.
22 Mtawala mkuu juu ya Walawi waliokuwa wakitumikia Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, ambao walikuwa waimbaji wa kazi katika nyumba ya Mungu.
The overseer also of the Levites at Jerusalem [was] Uzzi the son of Bani, the son of Hashabiah, the son of Mattaniah, the son of Micha. Of the sons of Asaph, the singers [were] over the business of the house of God.
23 Walikuwa chini ya maagizo kutoka kwa mfalme na maagizo imara yalitolewa kwa waimbaji kila siku inavyohitajika.
For [it was] the king's commandment concerning them, that a certain portion should be for the singers, due for every day.
24 Pethahia mwana wa Meshezabeli, mwana wa Zera, mwana wa Yuda, alikuwa upande wa mfalme kwa habari zote za watu.
And Pethahiah the son of Meshezabeel, of the children of Zerah the son of Judah [was] at the king's hand in all matters concerning the people.
25 Kuhusu vijiji na mashamba yao, baadhi ya watu wa Yuda wakakaa Kiriath-arba, na vijiji vyake, na Diboni, na vijiji vyake, na Yekabzeeli na vijiji vyake.
And for the villages, with their fields, [some] of the children of Judah dwelt at Kirjath-arba, and [in] its villages, and at Dibon, and [in] its villages, and at Jekabzeel, and [in] its villages,
26 Wakaishi katika Yeshua, Molada, Beth-Peleti,
And at Jeshua, and at Moladah, and at Beth-phelet,
27 Hazar-Shuali, Beersheba na vijiji vyake.
And at Hazar-shual, and at Beer-sheba, and [in] its villages,
28 Nao wakakaa Siklagi, na Mekona, na vijiji vyake,
And at Ziklag, and at Mekonah, and in its villages,
29 Enrimoni, Sora, Yarmuthi,
And at En-rimmon, and at Zareah, and at Jarmuth,
30 Zanoa, Adulamu, na vijiji vyake, na Lakishi, na mashamba yake, na Azeka, na vijiji vyake. Basi wakakaa kutoka Beer-sheba mpaka bonde la Hinomu.
Zanoah, Adullam, and [in] their villages, at Lachish, and its fields, at Azekah, and [in] its villages. And they dwelt from Beer-sheba to the valley of Hinnom.
31 Watu wa Benyamini pia walikuwa wakiishi kutoka Geba, kwenda Mikmashi na Aiya, na Beth-eli na vijiji vyake.
The children also of Benjamin from Geba [dwelt] at Michmash, and Aija, and Beth-el, and [in] their villages.
32 Waliishi Anathothi, Nobu, Anania,
[And] at Anathoth, Nob, Ananiah,
33 Hazori, Rama, Gitaimu,
Hazor, Ramah, Gittaim,
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati,
Hadid, Zeboim, Neballat,
35 Lodi, na Ono, bonde la wafundi.
Lod, and Ono, the valley of artificers.
36 Walawi wengine waliishi Yuda wengine Benyamini.
And of the Levites [were] divisions [in] Judah, [and] in Benjamin.

< Nehemia 11 >