< Mika 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Mika Mmorashti katika siku za Yotahamu, Ahazi, na Hezekeia, mfalme wa Yuda, lile neno aliloliona kuhusiana na Samaria na Yerusalemu.
This is the word of Yahweh that came to Micah the Morashtite in the days of Jotham, Ahaz, and Hezekiah, kings of Judah, which he saw concerning Samaria and Jerusalem.
2 Sikilizeni, ninyi watu wote. Sikilizeni, dunia, na vyote vilivyomo kwenye dunia. Acheni Yahwe ashuhudiwe dhidi yenu, Bwana kutoka kwenye hekalu lake takatifu.
Listen, all you peoples. Listen, earth, and all that is in you. Let the Lord Yahweh be a witness against you, the Lord from his holy temple.
3 Tazama, Yahwe anakuja kutoka mahali pake; atashuka chini na kupakanyaga mahali pa juu katika dunia.
Look, Yahweh comes out of his place; he will come down and tread on the high places of the earth.
4 Milima itayeyuka chini yake; mabonde yatapasuka vipande vipande kama mshumaa mbele ya moto, kama maji ambayo yamemwagika chini ya mteremko mkali.
The mountains will melt under him; the valleys will break apart, like wax before fire, like waters that are poured down a steep place.
5 Haya yote ni kwasababu ya uasi wa Yakobo, na kwasababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Je sababu ilikuwa nini kwa uasi wa Yakobo? Je ilikuwa Samaria? Je sababu ilikuwa nini kwa mahali pa juu pa Yuda? Je haiukuwa Yerusalemu?
All this is because of the Jacob's transgression, and because of the sins of the house of Israel. What is Jacob's transgression? Is it not Samaria? What is Judah's high place? Is it not Jerusalem?
6 “Nitaifanya Samaria rundo la uharibifu katika shamba, kama eneo la kupandia mizabibu. Nitayavuta mawe ya jengo lake kwenda kwenye bonde; Nitaifunua misingi yake.
“I will make Samaria a heap of ruins in the field, a place for planting vineyards, and I will pour her stones down into the valley and I will uncover her foundations.
7 Sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa vipande vipande; na zawadi zake zote zitachomwa moto. Kwa kuwa zawadi zake za ukahaba amezikusanya, na kama malipo ya ukahaba yatarudi.”
All her carved figures will be broken to pieces, and all her gifts that she received will be burned with fire, and I will destroy all her idols. Since she gathered her gifts from the wages of prostitutes, they will become the wages of prostitutes again.”
8 Kwa sababu hii nitalia na kuomboleza; nitaenda peku peku na uchi; Nitaomboleza kama mbeha na kuomboleza kama bundi.
For this reason I will lament and wail; I will go barefoot and naked; I will wail like the jackals and mourn like owls.
9 Kwa kuwa jeraha lake haliponi, kwa kuwa imefika kwa Yuda. Imefikia lango la watu wangu, hadi Yerusalemu.
For her wound is incurable, for it has come to Judah. It has reached the gate of my people, to Jerusalem.
10 Msiache kuwambia kuhusu katika Gathi; msilie tena. Katika Bethi Leafra nabiringisha mwenyewe kwenye mavumbi.
Do not tell about it in Gath; do not weep at all. At Beth Leaphrah I roll myself in the dust.
11 Piteni karibu na, makao ya Shafiri, katika uchi na aibu. Makazi ya Zaanani hayatatoka nje. Maombolezo ya Beth Ezeli, kwa ajili ya ulinzi yamechukuliwa.
Pass by, inhabitants of Shaphir, in nakedness and shame. The inhabitants of Zaanan do not come out. Beth Ezel mourns, for their protection is taken away.
12 Kwa kuwa wakaaji wa Marothi hungoja habari njema, kwa sababu hofu, kwa sababu msiba umetoka kwa Yahwe hadi kwenye malango ya Yerusalemu.
For the inhabitants of Maroth wait anxiously for good news, because disaster has come down from Yahweh to the gates of Jerusalem.
13 Wfuungeni lijamu farasi wakokote gari la farasi, makazi ya Lakishi. Wewe Lakishi, ulikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalionekana kwako.
Harness the chariot to the team of horses, inhabitants of Lachish. You, Lachish, were the beginning of sin for the daughter of Zion, for the transgressions of Israel were found in you.
14 Hivyo utaipa zawadi ya kuagia Moreshethi Gathi; mji wa Akzibu utawavunja moyo wafalme wa Israeli.
So you will give a parting gift to Moresheth Gath; the town of Akzib will disappoint the kings of Israel.
15 Tena nitaleta ushindi kwako, makazi ya Maresha; uzuri wa Israeli utakuja Adulamu.
I will again bring a conqueror to you, inhabitants of Mareshah; the splendor of Israel will come to Adullam.
16 Kata kipara chako na kata nywele zako kwa ajili ya watoto ambao unaowafurahisha. Fanya kipara chako mwenyewe kama tai, kwa ajili ya watoto wako watakao kwenda utumwani kutoka kwako
Shave your head and cut off your hair for the children in whom you delight. Make yourself as bald as eagles, for your children will go into exile from you.

< Mika 1 >