< Mathayo 26 >

1 Wakati Yesu alipomaliza kusema maneno yote hayo, aliwaambia wanafunzi wake,
When Yeshua had finished all these words, he said to his disciples,
2 “Mnajua kwamba baada ya siku mbili kutakuwa na sikukuu ya pasaka, na mwana wa Adamu atatolewa ili asulibiwe.”
“You know that after two days the Passover is coming, and the Son of Man will be delivered up to be crucified.”
3 Baadaye wakuu wa makuhani na wazee wa watu walikutana pamoja katika makao ya Kuhani Mkuu, aliye kuwa anaitwa Kayafa.
Then the chief priests, the scribes, and the elders of the people were gathered together in the court of the high priest, who was called Caiaphas.
4 Kwa pamoja walipanga njama ya kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
They took counsel together that they might take Yeshua by deceit and kill him.
5 Kwa kuwa walisema, “Isifanyike wakati wa sikukuu, kusudi isije ikazuka ghasia miongoni mwa watu.”
But they said, “Not during the feast, lest a riot occur amongst the people.”
6 Wakati Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,
Now when Yeshua was in Bethany, in the house of Simon the leper,
7 alipokuwa amejinyoosha mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa amebeba mkebe wa alabasta iliyokuwa na mafuta yenye thamani kubwa, na aliyamimina juu ya kichwa chake.
a woman came to him having an alabaster jar of very expensive ointment, and she poured it on his head as he sat at the table.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona jambo hilo, walichukia na kusema, “Nini sababu ya hasara hii?
But when his disciples saw this, they were indignant, saying, “Why this waste?
9 Haya yangeweza kuuzwa kwa kiasi kikubwa na kupewa maskini.”
For this ointment might have been sold for much and given to the poor.”
10 Lakini Yesu, akiwa anajua hili, aliwaambia, “Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu? Kwa kuwa amefanya kitu kizuri kwangu.
However, knowing this, Yeshua said to them, “Why do you trouble the woman? She has done a good work for me.
11 Masikini mnao siku zote, lakini hamtakuwa pamoja nami daima.
For you always have the poor with you, but you don’t always have me.
12 Kwa sababu alipomimina mafuta haya juu ya mwili wangu, alifanya hivyo kwa ajili ya maziko yangu.
For in pouring this ointment on my body, she did it to prepare me for burial.
13 Kweli nawaambieni, popote Injili hii itakapohubiriwa katika ulimwengu mzima, kitendo alichofanya huyu mwanamke, pia kitakuwa kinasemwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
Most certainly I tell you, wherever this Good News is preached in the whole world, what this woman has done will also be spoken of as a memorial of her.”
14 Ndipo mmoja wa wale Kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariote, alienda kwa wakuu wa makuhani
Then one of the twelve, who was called Judah Iscariot, went to the chief priests
15 na kusema, “Mtanipatia nini nikimsaliti?” Wakampimia Yuda vipande thelathini vya fedha.
and said, “What are you willing to give me if I deliver him to you?” So they weighed out for him thirty pieces of silver.
16 Tangu muda huo alitafuta nafasi ya kumsaliti.
From that time he sought opportunity to betray him.
17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi walimwendea Yesu na kusema, “Wapi unataka tukuandalie ule chakula cha Pasaka?”
Now on the first day of unleavened bread, the disciples came to Yeshua, saying to him, “Where do you want us to prepare for you to eat the Passover?”
18 Akawaambia, “Nendeni mjini kwa mtu fulani na mwambieni, Mwalimu anasema, “Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.””
He said, “Go into the city to a certain person, and tell him, ‘The Rabbi says, “My time is at hand. I will keep the Passover at your house with my disciples.”’”
19 Wanafunzi walifanya kama Yesu alivyowaagiza, na waliandaa chakula cha Pasaka.
The disciples did as Yeshua commanded them, and they prepared the Passover.
20 Ilipofika jioni, aliketi kula chakula pamoja na wale wanafunzi Kumi na Wawili.
Now when evening had come, he was reclining at the table with the twelve disciples.
21 Walipokuwa wanakula chakula, alisema, “Kweli nawaambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
As they were eating, he said, “Most certainly I tell you that one of you will betray me.”
22 Walihuzunika sana, na kila mmoja alianza kumuuliza, “Je, hakika siyo mimi, Bwana?”
They were exceedingly sorrowful, and each began to ask him, “It isn’t me, is it, Lord?”
23 Akawajibu, “Yule ambaye anachovya mkono wake pamoja nami katika bakuli ndiye atakaye nisaliti.
He answered, “He who dipped his hand with me in the dish will betray me.
24 Mwana wa Adamu ataondoka, kama alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu ambaye atamsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa vizuri kwa mtu huyo kama asingezaliwa.”
The Son of Man goes even as it is written of him, but woe to that man through whom the Son of Man is betrayed! It would be better for that man if he had not been born.”
25 Yuda, ambaye angemsaliti alisema, “Je!, Ni mimi Rabi?” Yesu akamwambia, “Umesema jambo hilo wewe mwenyewe.”
Judah, who betrayed him, answered, “It isn’t me, is it, Rabbi?” He said to him, “You said it.”
26 Walipokuwa wakila chakula, Yesu aliutwaa mkate, akaubariki, na kuumega. Akawapa wanafunzi wake akisema, “Chukueni, mle. Huu ni mwili wangu.”
As they were eating, Yeshua took bread, gave thanks for it, and broke it. He gave to the disciples and said, “Take, eat; this is my body.”
27 Akatwaa kikombe na kushukuru, akawapa na kusema, “Kunyweni wote katika hiki.
He took the cup, gave thanks, and gave to them, saying, “All of you drink it,
28 Kwa kuwa hii ni damu ya agano langu, inayomwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.
for this is my blood of the new covenant, which is poured out for many for the remission of sins.
29 Lakini nawaambieni, sitakunywa tena matunda ya mzabibu huu, hadi siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
But I tell you that I will not drink of this fruit of the vine from now on, until that day when I drink it anew with you in my Father’s Kingdom.”
30 Walipokuwa wamemaliza kuimba wimbo, walitoka kwenda Mlima wa Mizeituni.
When they had sung the Hallel, they went out to the Mount of Olives.
31 Kisha Yesu aliwaambia, “Usiku huu ninyi nyote mtajikwaa kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika.
Then Yeshua said to them, “All of you will be made to stumble because of me tonight, for it is written, ‘I will strike the shepherd, and the sheep of the flock will be scattered.’
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
But after I am raised up, I will go before you into Galilee.”
33 Lakini Petro alimwambia, “Hata kama wote watakukataa kwa sababu ya mambo yatakayokupata, mimi sitakukataa.”
But Peter answered him, “Even if all will be made to stumble because of you, I will never be made to stumble.”
34 Yesu akamjibu, “kweli nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Yeshua said to him, “Most certainly I tell you that tonight, before the rooster crows, you will deny me three times.”
35 Petro akamwambia, “hata kama ingenipasa kufa na wewe, sitakukana.” Na wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Peter said to him, “Even if I must die with you, I will not deny you.” All of the disciples also said likewise.
36 Baadaye Yesu alienda nao mahali panapoitwa Gethsemane na aliwaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nikienda huko na kuomba.”
Then Yeshua came with them to a place called Gethsemane, and said to his disciples, “Sit here, while I go there and pray.”
37 Akamchukua Petro na wana wawili wa Zebedayo na akaanza kuhuzunika na kusononeka.
He took with him Peter and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and severely troubled.
38 Kisha aliwaambia, “Roho yangu ina huzuni kubwa sana, hata kiasi cha kufa. Bakini hapa na mkeshe pamoja nami.”
Then Yeshua said to them, “My soul is exceedingly sorrowful, even to death. Stay here and watch with me.”
39 Akenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, na kuomba. Akasema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kiniepuke. Isiwe kama ninavyotaka mimi, bali kama utakavyo wewe.”
He went forward a little, fell on his face, and prayed, saying, “My Father, if it is possible, let this cup pass away from me; nevertheless, not what I desire, but what you desire.”
40 Akawaendea wanafunzi na akawakuta wamelala usingizi, na akamwambia Petro, “Kwa nini hamkuweza kukesha nami kwa saa moja?
He came to the disciples and found them sleeping, and said to Peter, “What, couldn’t you watch with me for one hour?
41 Kesheni na kuomba kusudi msiingie majaribuni. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Watch and pray, that you don’t enter into temptation. The spirit indeed is willing, but the flesh is weak.”
42 Akaenda zake mara ya pili na kuomba, akasema, “Baba yangu, kama jambo hili haliwezi kuepukika na ni lazima nikinywee kikombe hiki, mapenzi yako yatimizwe.”
Again, a second time he went away and prayed, saying, “My Father, if this cup can’t pass away from me unless I drink it, your desire be done.”
43 Akarudi tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito.
He came again and found them sleeping, for their eyes were heavy.
44 Kisha akawaacha tena akaenda zake. Akaomba mara ya tatu akisema maneno yaleyale.
He left them again, went away, and prayed a third time, saying the same words.
45 Baadaye Yesu aliwaendea wanafunzi wake na kuwaambia, “Bado mmelala tu na kujipumzisha? Tazameni, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Then he came to his disciples and said to them, “Are you still sleeping and resting? Behold, the hour is at hand, and the Son of Man is betrayed into the hands of sinners.
46 Amkeni, tuondoke. Tazama, yule anaye nisaliti amekaribia.”
Arise, let’s be going. Behold, he who betrays me is at hand.”
47 Wakati alipokuwa bado anaongea, Yuda mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Kundi kubwa lilifika pamoja naye likitokea kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu. Walikuja na mapanga na marungu.
While he was still speaking, behold, Judah, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and clubs, from the chief priests and elders of the people.
48 Tena mtu aliyekusudia kumsaliti Yesu alikuwa amewapa ishara, akisema, “Yule nitakayembusu, ndiye yeye. Mkamateni.”
Now he who betrayed him had given them a sign, saying, “Whoever I kiss, he is the one. Seize him.”
49 Mara hiyo alikuja kwa Yesu na kusema, “Salamu, Mwalimu!” Na akambusu.
Immediately he came to Yeshua, and said, “Greetings, Rabbi!” and kissed him.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, lifanye lile ambalo limekuleta.” Ndipo wakaja, na kumnyooshea mikono Yesu, na kumkamata.
Yeshua said to him, “Friend, why are you here?” Then they came and laid hands on Yeshua, and took him.
51 Tazama, mtu mmoja aliyekuwa pamoja na Yesu, alinyosha mkono wake, akachomoa upanga wake, na akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, na kumkata sikio lake.
Behold, one of those who were with Yeshua stretched out his hand and drew his sword, and struck the servant of the high priest, and cut off his ear.
52 Ndipo Yesu akamwambia, rudisha upanga wako pale ulipoutoa, kwa kuwa wote watumiao upanga wataangamizwa kwa upanga.
Then Yeshua said to him, “Put your sword back into its place, for all those who take the sword will die by the sword.
53 Mnadhani kuwa siwezi kumwita Baba yangu, naye akanitumia majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika?
Or do you think that I couldn’t ask my Father, and he would even now send me more than twelve legions of angels?
54 Lakini basi jinsi gani maandiko yangeweza kutimizwa, hivi ndivyo inapasa kutokea?”
How then would the Scriptures be fulfilled that it must be so?”
55 Wakati huo Yesu akauambia umati, “Je! Mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kama mnyang'anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, na hamkunishika!
In that hour Yeshua said to the multitudes, “Have you come out as against a robber with swords and clubs to seize me? I sat daily in the temple teaching, and you didn’t arrest me.
56 Lakini yote haya yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Ndipo wanafunzi wake wakamwacha na kukimbia.
But all this has happened that the Scriptures of the prophets might be fulfilled.” Then all the disciples left him and fled.
57 Wale waliomkamata Yesu alimpeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, mahali ambapo waandishi na wazee walikuwa wamekusanyika pamoja.
Those who had taken Yeshua led him away to Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were gathered together.
58 Lakini Petro alimfuata nyuma kwa mbali hadi katika ukumbi wa Kuhani Mkuu. Aliingia ndani na kukaa pamoja na walinzi aone kitakachotokea.
But Peter followed him from a distance to the court of the high priest, and entered in and sat with the officers, to see the end.
59 Basi wakuu wa makuhani na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu, kusudi wapate kumuua.
Now the chief priests, the elders, and the whole council sought false testimony against Yeshua, that they might put him to death,
60 Ingawa walijitokeza mashahidi wengi, Lakini hawakupata sababu yoyote. Lakini baadaye mashahidi wawili walijitokeza mbele
and they found none. Even though many false witnesses came forward, they found none. But at last two false witnesses came forward
61 na kusema, “Mtu huyu alisema, ''Naweza kulivunja hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”'
and said, “This man said, ‘I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.’”
62 Kuhani Mkuu alisimama na kumwuliza, “Hauwezi kujibu? Hawa wanakushuhudia nini dhidi yako?”
The high priest stood up and said to him, “Have you no answer? What is this that these testify against you?”
63 Lakini Yesu alikaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Kama Mungu aishivyo, nakuamuru utwambie, kama wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu.”
But Yeshua stayed silent. The high priest answered him, “I adjure you by the living God that you tell us whether you are the Messiah, the Son of God.”
64 Yesu akamjibu, “Wewe mwenyewe umesema jambo hilo. Lakini nakuambia, toka sasa na kuendelea utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wenye Nguvu, na akija katika mawingu ya mbinguni.”
Yeshua said to him, “You have said so. Nevertheless, I tell you, after this you will see the Son of Man sitting at the right hand of Power, and coming on the clouds of the sky.”
65 Ndipo Kuhani Mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Je, twahitaji tena ushahidi wa nini? Angalia, tayari mmesikia akikufuru.
Then the high priest tore his clothing, saying, “He has spoken blasphemy! Why do we need any more witnesses? Behold, now you have heard his blasphemy.
66 Je! Mnawaza nini? Wakajibu na kusema, “Anastahili kifo.”
What do you think?” They answered, “He is worthy of death!”
67 Kisha walimtemea mate usoni na kumpiga ngumi, na kumchapa makofi kwa mikono yao,
Then they spat in his face and beat him with their fists, and some slapped him,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo. Ni nani amekuchapa?”
saying, “Prophesy to us, you Messiah! Who hit you?”
69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa nje katika ukumbi, na mtumishi wa kike alimwendea na kusema, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Now Peter was sitting outside in the court, and a maid came to him, saying, “You were also with Yeshua, the Galilean!”
70 Lakini alikana mbele yao wote, akisema, Sijui kitu unachosema.”
But he denied it before them all, saying, “I don’t know what you are talking about.”
71 Alipoenda nje ya lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona na kuwaambia waliokuwepo hapo, “Mtu huyu pia alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
When he had gone out onto the porch, someone else saw him and said to those who were there, “This man also was with Yeshua of Nazareth.”
72 Akakana tena kwa kiapo, “Mimi simjui mtu huyu.”
Again he denied it with an oath, “I don’t know the man.”
73 Muda mfupi baadaye, wale waliokuwa wamesimama karibu, walimwendea na kusema na Petro, “Kwa hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa kuwa hata lafudhi yako inaonesha.”
After a little while those who stood by came and said to Peter, “Surely you are also one of them, for your speech makes you known.”
74 Ndipo alianza kulaani na kuapa, “Mimi simfahamu mtu huyu,” na mara hiyo jogoo akawika.
Then he began to curse and to swear, “I don’t know the man!” Immediately the rooster crowed.
75 Petro alikumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu, “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.”
Peter remembered the word which Yeshua had said to him, “Before the rooster crows, you will deny me three times.” Then he went out and wept bitterly.

< Mathayo 26 >