< Luka 1 >

1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
Efter månge hafva tagit sig före att beskrifva de ting, som ibland oss aldravissast äro;
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
Såsom de oss sagt hafva, som af begynnelsen det med sin ögon sågo, och sjelfve en del voro af det de sade;
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
Syntes ock mig, sedan jag af begynnelsen all ting granneliga utfrågat hafver, ordenteligen skrifva dig till, min gode Theophile;
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
Att du må förfara vissa sanningen om de stycker, der du om undervister äst.
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
Uti Herodis, Judee Konungs, tid, var en Prest, utaf Abie skifte, benämnd Zacharias; och hans hustru, af Aarons döttrar, benämnd Elisabet.
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
De voro både rättfärdige för Gud, vandrande i all Herrans bud och stadgar ostraffeliga.
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
Och de hade inga barn; ty Elisabet var ofruktsam, och både voro de framlidne i sin ålder.
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
Så begaf det sig, då han i sitt skifte skulle hålla sitt Prestaämbete för Gudi,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
Efter Presterskapets sed, och det föll på honom, att han skulle upptända rökelse, gick han in i Herrans tempel;
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
Och allt folket var utantill, och bad, så länge rökelsen skedde.
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
Så syntes honom Herrans Ängel, ståndandes på högra sidon vid rökaltaret.
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
Och Zacharias vardt förskräckt, då han såg honom, och en räddhåge föll öfver honom.
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
Så sade Ängelen till honom: Var icke förfärad, Zacharia; ty din bön är hörd, och din hustru Elisabet skall föda dig en son, hvilkens namn du skall kalla Johannes.
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
Och dig skall varda glädje och fröjd; och månge skola fröjdas af hans födelse;
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
Ty han skall varda stor för Herranom; vin och starka drycker skall han icke dricka; och skall straxt i moderlifvet uppfylld varda med den Helga Anda;
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
Och han skall omvända många af Israels barn till Herran, deras Gud.
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
Och han skall gå för honom, med Elie anda och kraft, till att omvända fädernas hjerta till barnen, och de ohöriga till de rättfärdigas snällhet; och göra Herranom ett beredt folk.
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
Då sade Zacharias till Ängelen: Hvaraf skall jag detta veta? Ty jag är gammal, och min hustru är framliden i åldren.
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
Ängelen svarade, och sade till honom: Jag är Gabriel, som står i Guds åsyn, och är utsänd till att tala dig till, och båda dig denna goda tidenden.
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
Och si, du skall varda mållös, och skall intet kunna tala, intill den dagen, då detta sker; derföre, att du icke trodde minom ordom, hvilke skola fullkomnad varda i sin tid.
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
Och folket förbidde Zachariam, och förundrade sig, att han så länge dvaldes i templet.
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
Men då han utgick, kunde han intet tala med dem; och så förmärkte de, att han hade sett någon syn i templet; och han tecknade dem, och blef mållös.
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
Och det begaf sig, då hans ämbetsdagar ute voro, gick han hem i sitt hus.
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
Och efter de dagar vardt hans hustru Elisabet hafvandes; och fördolde sig i fem månader, och sade:
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
Så hafver nu Herren gjort med mig, i de dagar, då han såg till mig, på det han skulle borttaga min försmädelse ibland menniskorna.
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
Uti sjette månaden vardt Gabriel Ängel utsänd af Gudi, uti en stad i Galileen, benämnd Nazareth;
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
Till en jungfru, som förlofvad var enom man, hvilkens namn var Joseph, af Davids hus; och jungfrunes namn Maria.
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
Och Ängelen kom in till henne, och sade: Hel, full med nåd! Herren är med dig; välsignad du ibland qvinnor.
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
Då hon såg honom, vardt hon förfärad af hans tal, och tänkte uppå, hurudana helsning detta var.
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
Då sade Ängelen till henne: Frukta dig icke, Maria; ty du hafver funnit nåd för Gudi.
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
Si, du skall afla i ditt lif, och föda en son, hvilkens Namn du skall kalla JESUS.
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
Han skall varda stor, och kallas dens Högstas Son; och Herren Gud skall gifva honom hans faders Davids säte;
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
Och han skall vara en Konung öfver Jacobs hus i evig tid; och på hans rike skall ingen ände vara. (aiōn g165)
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
Då sade Maria till Ängelen: Huru skall detta tillgå? Ty jag vet af ingen man.
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
Ängelen svarade, och sade till henne: Den Helge Ande skall komma öfver dig, och dens Högstas kraft skall öfverskygga dig; derföre ock det Helga, som af dig födt varder, skall kallas Guds Son.
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
Och si, Elisabet, din fränka, hafver ock aflat en son i sin ålderdom; och detta är sjette månaden åt henne, som hetes vara ofruktsam;
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
Ty för Gud är ingen ting omöjelig.
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
Då sade Maria: Si, Herrans tjenarinna; varde mig efter ditt tal. Och Ängelen skiljdes ifrå henne.
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
Uti de dagar stod Maria upp, och gick i bergsbygdena med hast, uti Jude stad;
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
Och kom uti Zacharie hus, och helsade Elisabet.
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
Och det begaf sig, då Elisabet hörde Marie helsning, sprang barnet uti hennes lif. Och Elisabet vardt uppfylld med den Helga Anda;
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
Och hon ropade med höga röst, och sade: Välsignad du ibland qvinnor, och välsignad dins lifs frukt.
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
Och hvadan kommer mig detta, att mins Herras moder kommer till mig?
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
Si, då rösten af dine helsning kom i min öron, sprang barnet af glädje i mitt lif.
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
Och salig äst du, som trodde; ty all ting varda fullbordad, som dig sagd äro af Herranom.
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
Och Maria sade: Min själ prisar storliga Herran;
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
Och min ande fröjdar sig i Gudi, minom Frälsare;
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
Ty han hafver sett till sine tjenarinnos ringhet: Si, härefter varda all slägte mig saliga kallande.
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
Ty den Mägtige hafver gjort mägtig ting med mig, och hans Namn är heligt;
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
Och hans barmhertighet varar ifrå slägte till slägte, öfver dem som frukta honom.
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
Han hafver bedrifvit magt med sinom arm, och förskingrat dem, som högfärdige äro uti deras hjertas sinne.
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
De mägtige hafver han satt af sätet, och uppsatt de ringa.
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
De hungriga hafver han med god ting uppfyllt, och de rika hafver han låtit tomma blifva.
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
Han hafver upptagit sin tjenare Israel, tänkande på sina barmhertighet;
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
Såsom han sagt hafver till våra fäder, Abraham och hans säd, till evig tid. (aiōn g165)
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
Och Maria blef när henne vid tre månader; och gick så hem i sitt hus igen.
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
Så vardt då Elisabet tiden fullbordad att hon skulle föda, och hon födde en son.
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
Och hennes grannar och fränder fingo höra, att Herren hade gjort stor barmhertighet med henne, och fröjdade sig med henne.
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
Och det begaf sig, på åttonde dagen kommo de till att omskära barnet; och kallade honom, efter hans fader, Zacharias.
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
Då svarade hans moder, och sade: Ingalunda; men han skall heta Johannes.
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
Då sade de till henne: Uti dine slägt är ingen, som hafver det namnet.
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
Så tecknade de hans fader, hvad han ville kalla honom.
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
Och han äskade ena taflo, der han uti skref, sägandes: Johannes är hans namn; och alle förundrade sig derpå.
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
Och straxt öppnades hans mun, och hans tunga; och han talade, lofvandes Gud.
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
Och stor fruktan kom öfver alla deras grannar; och ryktet om allt detta gick ut öfver alla Judiska bergsbygdena.
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Och alle de, som det hörde, sattet i sitt hjerta, sägande: Hvad månn varda utaf detta barnet? Ty Herrans hand var med honom.
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
Och hans fader Zacharias vardt uppfylld med den Helga Anda, propheterade, och sade:
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
Lofvad vare Herren, Israels Gud; ty han hafver besökt och förlossat sitt folk;
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
Och hafver upprättat oss salighetenes horn, uti sins tjenares Davids hus;
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
Såsom han i förtiden talat hafver, genom sina helga Propheters mun; (aiōn g165)
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
Att han skulle frälsa oss ifrå våra ovänner, och utur allas deras hand, som hata oss;
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
Och bevisa barmhertighet med våra fäder, och minnas på sitt helga Testamente;
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
Och på den ed, som han svorit hafver vårom fader Abraham, att gifva oss;
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
Att vi, frälste utur våra ovänners hand, måtte honom tjena utan fruktan;
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
I helighet och rättfärdighet, för honom, i alla våra lifsdagar.
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
Och du barn skall kallas dens Högstas Prophet; du skall gå för Herranom, till att bereda hans vägar;
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
Och gifva hans folke salighetenes kunskap, till deras synders förlåtelse;
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
Genom vår Guds innerliga barmhertighet, genom hvilken uppgången af höjdene hafver oss besökt;
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
Till att uppenbaras dem, som sitta i mörkret och dödsens skugga, och styra våra fötter på fridsens väg.
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
Och barnet växte upp, och stärktes i Andanom; och vistades i öknene, till den dagen han skulle framkomma för Israels folk.

< Luka 1 >