< Luka 1 >

1 Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
如你所知,很多人都曾试图用文字记录我们参与的成就。
2 kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
他们所记录的证据,来自最早见证和传递上帝讯息之人。
3 Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
由于我从始至终都参与其中,所以应该可以准确无误地撰写所发生的一切。
4 Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
敬爱的提阿非罗们,我之所以这么做,是为了让你们确认自己所学之道完全值得信赖。
5 Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
希律担任犹太王的那段时间,亚比雅班里有一位名叫撒迦利亚的祭司,他妻子以利沙伯是亚伦的后人。
6 Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
他们的一举一动都遵循上帝正道,严格遵守主所立下的一切诫命规条。
7 Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
但他们没有孩子,因为以利沙伯无法生育,而且二人都年岁已高。。
8 Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
有一天,撒迦利亚按照排班的时间履行作为上帝祭司的职责,
9 Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
照惯例抽签后,他被选中进入主的神庙上香。
10 Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
在烧香的过程,众人都在外面祈祷。
11 Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
这时天使向撒迦利亚显化,立于香坛的右侧。
12 Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
撒迦利亚见状颇感惊慌,非常害怕。
13 Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
天使说:“撒迦利亚,别害怕,上帝听到了你的祈求。你妻子以利沙伯将为你生下一子,你将为他起名为约翰。
14 Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
这孩子会为你带来欢喜和快乐,许多人都会来庆祝他的降生。
15 Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
他将成为主面前的尊者,滴酒不沾,未降生之前便有圣灵附体。
16 Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
他将带领众多以色列人,回到主、也就是他们的上帝身边。
17 Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
他将以以利亚的圣灵和力量走在前,劝说父亲们关爱自己的儿女,规劝悖逆之人走正道,让民众准备好迎接主。”
18 Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
撒迦利亚问天使:“我要如何相信这一切?我老了,我妻子也是一把年纪。”
19 Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
天使回答:“我是上帝面前的加百列,奉命向你传话,告诉你这个好消息。
20 Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
但你并不相信我所说的一切,所以你会失语,直到我所言之事成真,你才能开口说话。”
21 Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
众人正在外面等候撒迦利亚,见他迟迟未从神庙出来,很是奇怪。
22 Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
但他出来时却真的失语了,无法讲话,只能打手势。于是众人意识到刚才在神庙中出现了神迹。
23 Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
他完成自己的职责后便回了家。
24 Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
几天后,他妻子以利沙伯果真怀孕,在家中待了五个月。
25 “Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
她说:“这一切是主的旨意,他这样待我,便是要让我不再在世人面前感到羞辱。”
26 Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
在怀孕的第六个月,上帝派天使加百列来到加利利的拿撒勒镇,现身在一个名叫玛利亚的少女面前。
27 kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
玛利亚当时已与一位名叫约瑟夫的男人订婚。
28 Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
天使向她问候,然后对她说“你很幸运,主与你同在。”
29 Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
玛利亚对此颇感困惑,不知道这问候到底意味着什么。
30 Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
天使说:“玛利亚,不要怕!因为上帝已对你施以恩典。
31 Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
你将怀孕生子,那婴儿将起名叫耶稣。
32 Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
他将成为一位伟人,被称为至高上帝之子,上帝将把向其赐予祖先大卫的王位,
33 Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
他将永远统治雅各的家园,他的王国将永续存在。” (aiōn g165)
34 Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
玛利亚问天使:“但这怎能可能?我还是处女。”
35 Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
天使回答:“圣灵将降临于你,至高上帝将笼罩于你。那即将诞下的婴儿生而神圣,将被称为上帝之子。
36 Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
甚至连你的亲戚以利沙伯都怀孕了,人们说那女人无法生育,现在怀胎已有六个月。
37 Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
对于上帝而言,一切皆有可能。”
38 Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
玛利亚说:“我听你的,随时准备服侍上帝,愿你所言的事情发生在我身上。”于是天使便离开了。
39 Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
稍后,玛利亚准备了一下便急忙赶去犹太山地的一座城市,
40 Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
来到撒迦利亚的家。她走进屋向以利沙伯问安。
41 Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
听见玛利亚的问候,以利沙伯腹中的婴儿立刻开始跳动,表达着喜悦。圣灵注入了以利沙伯的体内,
42 Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
于是她高声说:“你是一位如此有福的女人,你腹中的婴儿能由你诞下,也是一种福气!
43 Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
我太荣幸了,我主之母能够造访我的寒舍。
44 Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
听到你问候的那一刻,我腹中的婴儿就欢喜跳跃。
45 Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
你真荣幸,因为你已确信,主将把对你的承诺变为现实!”
46 Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
玛利亚说:“赞美主!
47 na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
上帝救世主让我如此欢喜,
48 Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
因为我作为他的仆人,尽管身世卑微,他却决定垂青于我。今后万代都会认为我是获得赐福之人。
49 Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
全能上帝对我做出伟大之举,他的名字如此神圣。
50 Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
他的怜悯将在尊敬他的世界中传递。
51 Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
他凭借其力量,击败了那些自作聪明之人。
52 Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
他能够让位高权重之人跌落王位,让谦卑之人获得升华,
53 Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
他让饥肠辘辘之人饱餐美食,也让富足之人两手空空。
54 Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
在他的帮助下,他的仆人以色列将永记他的怜悯, (aiōn g165)
55 (kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
正如他向我们先父、亚伯拉罕及其后裔所做的承诺。”
56 Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
玛利亚和以利沙伯同住了三个月,然后便返回自己的家。
57 Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
以利沙伯终于诞下一名男婴。
58 Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
邻居和亲戚们得知主向她施以如此善意,便和她一同庆祝。
59 Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
到了第八天,他们前来为孩子行割礼,打算让他随父亲的名字叫撒迦利亚。
60 Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
但以利沙伯说:“不要,他应该叫做约翰。”
61 Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
众人回答:“但你的亲戚中并没有这样的名字。”
62 Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
他们通过手势询问孩子的父亲撒迦利亚,询问他的意见。
63 Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
撒迦利亚示意要写字。令众人诧异的是,他写下的是:“他就叫约翰。”
64 Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
忽然他再次开口说话了,开始赞美上帝。
65 Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
这一切让住在周围的人心生敬畏,这个消息很快就传遍整个犹太山地。
66 Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
众人听闻此事便思量它的含义:“这孩子将会成为怎样的人?”因为很显然,他对上帝而言非常特别。
67 Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
婴儿的父亲撒迦利亚体内充满了圣灵,他预言道:
68 “Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
“主就是以色列的上帝,他如此伟大,因为他降临到子民之中,为其赋予自由,
69 Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
他向其仆人大卫的家族赐予伟大的救赎,
70 kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
正如他自古以来借由其神圣先知所传达的预言。 (aiōn g165)
71 Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
他承诺拯救我们摆脱敌人,远离那些憎恨我们的人。
72 Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
他怜悯我们的祖先,记得他的圣约,
73 kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
那是他向我们的祖先亚伯拉罕所发誓言。
74 Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
他让我们摆脱恐惧,从敌人手中拯救我们,
75 katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
这让我们可以毕生遵循正道并服侍于他。
76 Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
尽管你现在只是一个婴儿,但却会被称为至高上帝的先知,因你将先于主之前,为他铺好道路,
77 kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
通过宽恕其子民的罪,传播救赎的讯息。
78 Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
蒙上帝对我们的关爱怜悯,天堂的黎明将降临照耀我们,
79 kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
照亮那些活在黑暗中、笼罩在死亡阴影中的人,引导我们走上平安之路。”
80 Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.
这个叫做约翰的男孩逐渐长大,精神变得很强大。他一直住在荒野之中,等待在以色列人中公开露面的时机。

< Luka 1 >