< Yoshua 6 >

1 Basi, milango yote ya Yeriko ilikuwa imefungwa kwasababu ya jeshi la Israeli. Hapakuwa na mtu wa kutoka nje au kuingia ndani.
Forsothe Jerico was closid and wardid, for the drede of the sones of Israel, and no man durste entre, ethir go out.
2 Yahweh akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeweka Yeriko katika mkono wako, mfalme wake pamoja na wanajeshi wake waliofunzwa.
And the Lord seide to Josue, Lo! Y yaf in to thin hondis Jerico, and the king therof, and alle strong men.
3 Ni lazima kutembea kwa kuuzunguka mji, wanaume wote wa vita wauzunguke mji mara moja. Ni lazima mfanye hivi kwa siku sita.
Alle ye fiyteris, cumpasse the citee onys bi the day; so ye schulen do in sixe daies.
4 Makuhani saba lazima wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele za sanduku. Na katika siku ya saba, ni lazima mtembee kwa kuuzunguka mji mara saba, na makuhani lazima wapulize tarumbeta.
Forsothe in the seuenthe dai the preestis schulen take seuene clariouns, of whiche `the vss is in iubile; and thei schulen go bifor the arke of boond of pees; and seuen sithes ye schulen cumpasse the citee, and the preestis schulen trumpe with clariouns.
5 Kisha watapuliza pembe za kondoo waume kwa nguvu kuu, na mtakaposikia sauti za tarumbeta watu wote na wapige kelele kwa mshindo mkuu, na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale. Wanajeshi ni lazime washambulie, kila mmoja eende mbele moja kwa moja.
And whanne the vois of the trumpe schal sowne lengere, and more bi whiles, and schal sowne in youre eeris, al the puple schal crie togidere with gretteste cry; and the wallis of the citee schulen falle alle doun, and alle men schulen entre bi the place, ayens which thei stonden.
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni, aliwaita makuhani na kuwaambia, “Lichukueni sanduku la agano, na waacheni makuhani saba wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Yahweh.”
Therfor Josue, the sone of Nun, clepide preestis, and seide to hem, Take ye the ark of boond of pees, and seuene othere preestis take seuene clariouns of iubile yeeris, and go thei bifor the arke of the Lord.
7 Yoshua aliwaambia watu, “Nendeni na mkatembee kuuzunguka mji, na watu wa vita wataenda mbele ya sanduku la Yahweh.”
Also Josue seide to the puple, Go ye, and cumpasse ye the citee, and go ye armed bifor the arke of the Lord.
8 Makuhani saba walibeba tarumbeta saba za pembe za kondoo mbele ya Yahweh kama Yoshua alivyowaambia watu. Na walivyokuwa akiendelea mbele, walipuliza tarumbeta.
And whanne Josue hadde endid the wordis, and seuene preestis trumpiden with seuen clariouns bifor the arke of boond of pees of the Lord,
9 Sanduku la Yahweh liliwafuata kwa nyuma yao. Watu wa vita walitembea mbele ya makuhani, na walipuliza tarumbeta zao, lakini walinzi wa nyuma walilifuata sanduku kwa nyuma, na makuhani waliendelea kupuliza tarumbeta zao.
and al the puple armed yede bifore, the tothir comyn puple of fiyteris suede the arke, and alle thingis sowneden with clariouns.
10 Lakini Yoshua aliwaagiza watu, akisema, “Msipige kelele. Sauti yoyote isitoke vinywani mwenu mpaka siku nitakayowaambia kupiga kelele. Ndipo hapo mtakapopiga kelele.”
Sotheli Josue comaundide to the puple, and seide, Ye schulen not crye, nethir youre vois schal be herd, nethir ony word schal go out of youre mouth, til the dai come, in which Y schal seie to you, Crye ye, and make ye noyse.
11 Hivyo, alisababisha sanduku la Yahweh kuuzunguka mji mara moja kwa siku hiyo. Kisha wakaingia katika kambi yao, wakakaa usiku ule katika kambi.
Therfor the arke of the Lord cumpasside the citee onys bi day, and turnede ayen in to the castels, and dwellide there.
12 Basi Yoshua aliamka asubuhi na mapema, na makuhani wakalichukua sanduku la Yahweh.
Therfor while Josue roos bi nyyt, preestis tooken the arke of the Lord;
13 Makuhani saba waliobeba tarumbeta saba za pembe za kondoo waume walikuwa mbele ya sanduku la Yahweh, wakitembea kwa ushupavu, huku wakipuliza tarumbeta. Wanajeshi wenye silaha walikuwa wakitembea mbele yao, lakini walinzi wa nyuma walitembea nyuma ya sanduku la Yahweh, huku tarumbeta ziliendelea kupigwa.
and seuene of the preestis token seuen clariouns, of whiche `the vss is in iubilee, and yeden bifor the arke of the Lord, `and yeden, and trumpiden; and the puple yede armed bifor hem. Sotheli the tother comyn puple suede the arke, and sownede with clariouns.
14 Walitembea kuuzunguka mji mara moja katika siku ya pili na kisha wakarudi kambini. Walifanya hivi kwa siku sita.
And thei cumpassiden the citee in the secunde dai onys, and turneden ayen in to the castels; so thei dyden in sixe daies.
15 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambayo waliamka mapema katika mapambazuko, na walitembea kuuzunguka mji kwa namna ile kama ilivyokuwa kawaida yao, katika siku hii walifanya mara saba.
Sotheli in the seuenthe dai thei risiden eerli, and cumpassiden the citee, as it was disposid, seuen sithis.
16 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambapo makuhani walipiga tarumbeta, na ya kwamba Yoshua aliwaagiza watu, “Pigeni kelele! Kwa kuwa Yahweh amewapa ninyi mji.
And whanne in the seuenthe cumpas preestis sowneden with clariouns, Josue seide to al Israel, Crie ye, for the Lord hath bitake the citee to vs;
17 Mji pamoja na vitu vyote ndani yake vitatengwa kwa Yahweh kwa ajili ya uharibifu. Ni Rahabu yule kahaba pekee ataishi - yeye pamoja wote waliokuwa pamoja naye katika nyumba - kwasababu aliwaficha watu tuliowatuma.
and this citee be cursid, ethir distried, and alle thingis that ben therynne be halewid to the Lord. Raab the hoor aloone lyue, with alle men that ben with hir in the hows; for sche hidde the messangeris whiche we senten.
18 Lakini kwenu, iweni waangalifu juu ya kuchukua vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu, ili baada ya kuvitia alama kwa ajili ya kuharibiwa, msichukue hata kimoja wapo. Na kama mtafanya hivi, mtaifanya kambi ya Waisraeli iharibiwe na mtaleta matatizo katika kambi.
Forsothe be ye war, lest ye touchen ony thing of these that ben comaundid to you, and ye ben gilti of trespassyng; and alle the castels of Israel be vndur synne, and be troblid.
19 Fedha zote, dhahabu na vitu vilivyotengenezwa kwa shaba na chuma vilitengwa kwa ajli ya Yahweh.”
Sotheli what euer thing is of gold, and of siluer, and of brasun vessels, and of yrun, be halewid to the Lord, and be kept in hise tresoris.
20 Hivyo, watu wakapiga kelele, na wakatoa sauti kwa kupuliza tarumbeta. Ilikuwa watu waliposikia sauti za tarumbeta, walipiga kelele kwa sauti kuu, na ukuta ulianguka chini kabisa na kwamba watu waliungia mji, kila mmoja alisonga mbele moja kwa moja. Na waliuteka mji.
Therfor while al the puple criede, and the trumpis sowneden, aftir that the sowne sownede in the eeris of the multitude, the walles felden doun anoon; and ech man stiede bi the place that was ayens hym. And thei token the citee,
21 Waliteketeza kabisa kila kitu kilichokuwa katika mji kwa makali ya upanga - wanaume kwa wanawake, wadogo kwa wakubwa, ng'ombe, kondoo na punda.
and killiden alle thingis that weren therynne, fro man `til to womman, fro yong child `til to eld man; also thei smytiden bi the scharpnesse of swerd, oxun, and scheep, and assis.
22 Kisha Yoshua akawaambia wale watu wawili walioipeleleza nchi, “Nendeni katika nyumba ya kahaba, mtoeni mwanamke na wote walio pamoja naye, kama mlivyomwapia.”
Forsothe Josue seide to twei men, that weren sent aspieris, Entre ye in to the hows of the womman hoore, and brynge ye forth hir, and alle thingis that ben herne, as ye maden stedfast to hir bi an ooth.
23 Basi, vijana wale walioipeleleza nchi waliingia ndani na kumtoa Rahabu nje. Walimtoa nje baba yake, mama, kaka, na ndugu wote waliokuwa pamoja naye. waliwaleta katika sehemu ya nje ya kambi ya Waisraeli.
And the yonge men entriden, and ledden out Raab, and her fadir, and modir, and britheren, and al the purtenaunce of houshold, and the kynrede `of hir; and maden to dwelle without the castels of Israel.
24 Na ndipo waliuteketeza mji na kila kitu ndani yake. Isipokuwa fedha, dhahabu na vyombo vya fedha na chuma viliwekwa kwa hazina ya nyumba ya Yahweh.
Sotheli thei brenten the citee, and alle thingis that weren foundun therynne, without gold, and siluer, and brasun vesselis, and yrun, which thei halewiden in to the `treserie of the Lord.
25 Bali Yoshua alimruhusu Rahabu kahaba, nyumba ya baba yake, na wote waliokuwa pamoja naye waishi. Mpaka leo hivi anaishi Israeli kwasababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko.
Sotheli Josue made Raab the hoore to lyue, and `the hows of hir fadir, and alle thingis that sche hadde; and thei dwelliden in the myddis of Israel, `til in to present dai; for sche hidde the messangeris, whiche he sente to asspie Jerico. In that tyme Josue preiede hertli,
26 Kisha katika kipindi hicho, Yoshua aliwaamuru kwa kiapo na kusema, “Alaaniwe machoni pa Yahweh mtu yule anayeujenga mji huu, Yeriko. Ataujenga msingi kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza, na kwa gharama ya mzaliwa wake wa pili atapachika milango yake.”
and seide, Cursid bifor the Lord be the man, that reisith and bildith the citee of Jerico! Leie he the foundementis therof in his firste gendrid sone, and putte he the yatis therof in the laste of fre children.
27 Basi Yahweh alikuwa pamoja na Yoshua, na umaarufu wake ulienea katika nchi yote.
Therfor the Lord was with Josue, and his name was pupplischid in ech lond.

< Yoshua 6 >