< Yoshua 6 >

1 Basi, milango yote ya Yeriko ilikuwa imefungwa kwasababu ya jeshi la Israeli. Hapakuwa na mtu wa kutoka nje au kuingia ndani.
Now Jericho was straitly shut up because of the children of Israel: none went out, and none came in. —
2 Yahweh akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeweka Yeriko katika mkono wako, mfalme wake pamoja na wanajeshi wake waliofunzwa.
And the LORD said unto Joshua: 'See, I have given into thy hand Jericho, and the king thereof, even the mighty men of valour.
3 Ni lazima kutembea kwa kuuzunguka mji, wanaume wote wa vita wauzunguke mji mara moja. Ni lazima mfanye hivi kwa siku sita.
And ye shall compass the city, all the men of war, going about the city once. Thus shalt thou do six days.
4 Makuhani saba lazima wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele za sanduku. Na katika siku ya saba, ni lazima mtembee kwa kuuzunguka mji mara saba, na makuhani lazima wapulize tarumbeta.
And seven priests shall bear seven rams' horns before the ark; and the seventh day ye shall compass the city seven times, and the priests shall blow with the horns.
5 Kisha watapuliza pembe za kondoo waume kwa nguvu kuu, na mtakaposikia sauti za tarumbeta watu wote na wapige kelele kwa mshindo mkuu, na ukuta wa mji utaanguka chini pale pale. Wanajeshi ni lazime washambulie, kila mmoja eende mbele moja kwa moja.
And it shall be, that when they make a long blast with the ram's horn, and when ye hear the sound of the horn, all the people shall shout with a great shout; and the wall of the city shall fall down flat, and the people shall go up every man straight before him.'
6 Ndipo Yoshua mwana wa Nuni, aliwaita makuhani na kuwaambia, “Lichukueni sanduku la agano, na waacheni makuhani saba wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele ya sanduku la Yahweh.”
And Joshua the son of Nun called the priests, and said unto them: 'Take up the ark of the covenant, and let seven priests bear seven rams' horns before the ark of the LORD.'
7 Yoshua aliwaambia watu, “Nendeni na mkatembee kuuzunguka mji, na watu wa vita wataenda mbele ya sanduku la Yahweh.”
And he said unto the people: 'Pass on, and compass the city, and let the armed body pass on before the ark of the LORD.'
8 Makuhani saba walibeba tarumbeta saba za pembe za kondoo mbele ya Yahweh kama Yoshua alivyowaambia watu. Na walivyokuwa akiendelea mbele, walipuliza tarumbeta.
And it was so, that when Joshua had spoken unto the people, the seven priests bearing the seven rams' horns before the LORD passed on, and blew with the horns; and the ark of the covenant of the LORD followed them.
9 Sanduku la Yahweh liliwafuata kwa nyuma yao. Watu wa vita walitembea mbele ya makuhani, na walipuliza tarumbeta zao, lakini walinzi wa nyuma walilifuata sanduku kwa nyuma, na makuhani waliendelea kupuliza tarumbeta zao.
And the armed men went before the priests that blew the horns, and the rearward went after the ark, the priests blowing with the horns continually.
10 Lakini Yoshua aliwaagiza watu, akisema, “Msipige kelele. Sauti yoyote isitoke vinywani mwenu mpaka siku nitakayowaambia kupiga kelele. Ndipo hapo mtakapopiga kelele.”
And Joshua commanded the people, saying: 'Ye shall not shout, nor let your voice be heard, neither shall any word proceed out of your mouth, until the day I bid you shout; then shall ye shout.'
11 Hivyo, alisababisha sanduku la Yahweh kuuzunguka mji mara moja kwa siku hiyo. Kisha wakaingia katika kambi yao, wakakaa usiku ule katika kambi.
So he caused the ark of the LORD to compass the city, going about it once; and they came into the camp, and lodged in the camp.
12 Basi Yoshua aliamka asubuhi na mapema, na makuhani wakalichukua sanduku la Yahweh.
And Joshua rose early in the morning, and the priests took up the ark of the LORD.
13 Makuhani saba waliobeba tarumbeta saba za pembe za kondoo waume walikuwa mbele ya sanduku la Yahweh, wakitembea kwa ushupavu, huku wakipuliza tarumbeta. Wanajeshi wenye silaha walikuwa wakitembea mbele yao, lakini walinzi wa nyuma walitembea nyuma ya sanduku la Yahweh, huku tarumbeta ziliendelea kupigwa.
And the seven priests bearing the seven rams' horns before the ark of the LORD went on continually, and blew with the horns; and the armed men went before them; and the rearward came after the ark of the LORD, the priests blowing with the horns continually.
14 Walitembea kuuzunguka mji mara moja katika siku ya pili na kisha wakarudi kambini. Walifanya hivi kwa siku sita.
And the second day they compassed the city once, and returned into the camp; so they did six days.
15 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambayo waliamka mapema katika mapambazuko, na walitembea kuuzunguka mji kwa namna ile kama ilivyokuwa kawaida yao, katika siku hii walifanya mara saba.
And it came to pass on the seventh day, that they rose early at the dawning of the day, and compassed the city after the same manner seven times; only on that day they compassed the city seven times.
16 Ilikuwa ni katika siku ya saba ambapo makuhani walipiga tarumbeta, na ya kwamba Yoshua aliwaagiza watu, “Pigeni kelele! Kwa kuwa Yahweh amewapa ninyi mji.
And it came to pass at the seventh time, when the priests blew with the horns, that Joshua said unto the people: 'Shout; for the LORD hath given you the city.
17 Mji pamoja na vitu vyote ndani yake vitatengwa kwa Yahweh kwa ajili ya uharibifu. Ni Rahabu yule kahaba pekee ataishi - yeye pamoja wote waliokuwa pamoja naye katika nyumba - kwasababu aliwaficha watu tuliowatuma.
And the city shall be devoted, even it and all that is therein, to the LORD; only Rahab the harlot shall live, she and all that are with her in the house, because she hid the messengers that we sent.
18 Lakini kwenu, iweni waangalifu juu ya kuchukua vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu, ili baada ya kuvitia alama kwa ajili ya kuharibiwa, msichukue hata kimoja wapo. Na kama mtafanya hivi, mtaifanya kambi ya Waisraeli iharibiwe na mtaleta matatizo katika kambi.
And ye, in any wise keep yourselves from the devoted thing, lest ye make yourselves accursed by taking of the devoted thing, so should ye make the camp of Israel accursed, and trouble it.
19 Fedha zote, dhahabu na vitu vilivyotengenezwa kwa shaba na chuma vilitengwa kwa ajli ya Yahweh.”
But all the silver, and gold, and vessels of brass and iron, are holy unto the LORD; they shall come into the treasury of the LORD.'
20 Hivyo, watu wakapiga kelele, na wakatoa sauti kwa kupuliza tarumbeta. Ilikuwa watu waliposikia sauti za tarumbeta, walipiga kelele kwa sauti kuu, na ukuta ulianguka chini kabisa na kwamba watu waliungia mji, kila mmoja alisonga mbele moja kwa moja. Na waliuteka mji.
So the people shouted, and the priests blew with the horns. And it came to pass, when the people heard the sound of the horn, that the people shouted with a great shout, and the wall fell down flat, so that the people went up into the city, every man straight before him, and they took the city.
21 Waliteketeza kabisa kila kitu kilichokuwa katika mji kwa makali ya upanga - wanaume kwa wanawake, wadogo kwa wakubwa, ng'ombe, kondoo na punda.
And they utterly destroyed all that was in the city, both man and woman, both young and old, and ox, and sheep, and ass, with the edge of the sword.
22 Kisha Yoshua akawaambia wale watu wawili walioipeleleza nchi, “Nendeni katika nyumba ya kahaba, mtoeni mwanamke na wote walio pamoja naye, kama mlivyomwapia.”
And Joshua said unto the two men that had spied out the land: 'Go into the harlot's house, and bring out thence the woman, and all that she hath, as ye swore unto her.'
23 Basi, vijana wale walioipeleleza nchi waliingia ndani na kumtoa Rahabu nje. Walimtoa nje baba yake, mama, kaka, na ndugu wote waliokuwa pamoja naye. waliwaleta katika sehemu ya nje ya kambi ya Waisraeli.
And the young men the spies went in, and brought out Rahab, and her father, and her mother, and her brethren, and all that she had, all her kindred also they brought out; and they set them without the camp of Israel.
24 Na ndipo waliuteketeza mji na kila kitu ndani yake. Isipokuwa fedha, dhahabu na vyombo vya fedha na chuma viliwekwa kwa hazina ya nyumba ya Yahweh.
And they burnt the city with fire, and all that was therein; only the silver, and the gold, and the vessels of brass and of iron, they put into the treasury of the house of the LORD.
25 Bali Yoshua alimruhusu Rahabu kahaba, nyumba ya baba yake, na wote waliokuwa pamoja naye waishi. Mpaka leo hivi anaishi Israeli kwasababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko.
But Rahab the harlot, and her father's household, and all that she had, did Joshua save alive; and she dwelt in the midst of Israel, unto this day; because she hid the messengers, whom Joshua sent to spy out Jericho.
26 Kisha katika kipindi hicho, Yoshua aliwaamuru kwa kiapo na kusema, “Alaaniwe machoni pa Yahweh mtu yule anayeujenga mji huu, Yeriko. Ataujenga msingi kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza, na kwa gharama ya mzaliwa wake wa pili atapachika milango yake.”
And Joshua charged the people with an oath at that time, saying: 'Cursed be the man before the LORD, that riseth up and buildeth this city, even Jericho; with the loss of his first-born shall he lay the foundation thereof, and with the loss of his youngest son shall he set up the gates of it.'
27 Basi Yahweh alikuwa pamoja na Yoshua, na umaarufu wake ulienea katika nchi yote.
So the LORD was with Joshua; and his fame was in all the land.

< Yoshua 6 >