< Yoshua 22 >

1 Kwa wakati huo, Yoshua aliwaita Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase.
At that time Joshua called the Reubenites, the Gadites, and the half tribe of Manasseh.
2 Aliwaambia, “Mmefanya kila kitu ambacho Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi. Mmeitii sauti yangu katika yote niliyowaagiza.
He said to them, “You have done everything that Moses the servant of Yahweh commanded you. You have obeyed my voice in all that I commanded you.
3 Bado hamjawaacha ndugu zenu hawa kwa siku zote hizi, mpaka siku hii ya leo. Na mmetimiza wajibu unaotakiwa na amri za Yahweh Mungu wenu.
You have not deserted your brothers these many days, down to this present day, and you have fulfilled the duties required by the commandments of Yahweh your God.
4 Sasa Yahweh Mungu wenu amewapa pumziko ndugu zenu, kama alivyowaahidi. Hivyo basi, rudini na mwende katika hema zenu katika nchi mnayoimiliki, ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapeni katika upande mwingine wa Yordani.
Now Yahweh your God has given rest to your brothers, just as he promised them. Therefore turn and go to your tents in the land you own, which Moses the servant of Yahweh gave you on the other side of the Jordan.
5 Lakini zingatieni kuzishika amri na sheria ambazo Musa mtumishi wa Yahweh aliwaagiza ninyi, kumpenda Yahweh Mungu wenu, kutembea katika njia zake, kuzitunza amri zake, na kuambatana naye na kumwabudu yeye kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.
Just be very careful to observe the commandments and the law that Moses the servant of Yahweh commanded you, to love Yahweh your God, to walk in all his ways, to keep his commandments, and to cling to him and worship him with all your heart and with all your soul.”
6 Basi Yoshua akawabariki na kisha akawaacha waende zao, nao wakarudi katika hema zao.
So Joshua blessed them and sent them away, and they went back to their tents.
7 Na kwa nusu ya kabila la Manase, Musa alikuwa amewapa urithi katika Bashani, lakini kwa nusu ya kabila hilo, Yoshua aliwapa urithi karibu na ndugu zao katika nchi magharibi mwa Yordani. Yoshua aliwaaga waende katika hema zao; aliwabarikia,
Now to one-half of the tribe of Manasseh Moses had given an inheritance in Bashan, but to the other half Joshua gave an inheritance beside their brothers in the land west of the Jordan. Joshua sent them away to their tents; he blessed them
8 na kisha akawaambia, “Rudini katika hema zenu mkiwa na pesa nyingi, na mkiwa na mifugo mingi, pamoja na na fedha, na dhahabu, na shaba na chuma, na nguo nyingi. Gawaneni na ndugu zenu nyara mlizochukua kutoka kwa maadui zenu.
and said to them, “Return to your tents with much money, and with very much livestock, and with silver and gold, and with bronze and iron, and with very many garments. Divide the plunder from your enemies with your brothers.”
9 Hivyo, wazawa wa Rubeni, wazawa wa Gadi na nusu ya kabila la Manase walirudi nyumbani, waliwaacha watu wa Isaeli hapo Shilo, ambayo imo ndani ya nchi ya Kanaani. Waliondoka wakaenda katika mkoa wa Gileadi, katika nchi yao, ambayo wao wenyewe waliimiliki, katika utiifu wa amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.
So the descendants of Reuben, the descendants of Gad, and the half tribe of Manasseh returned home, leaving the people of Israel at Shiloh, which is in the land of Canaan. They left to go to the region of Gilead, to their own land, which they themselves possessed, in obedience to the commandment of Yahweh, by the hand of Moses.
10 Nao walipofika hapo Yordani iliyo katika nchi ya Kanaani, Warubeni na Wagadi na nusu ya kabila la Manase walijenga madhabahu karibu na Yordani, madhabahu kubwa na iliyotokeza na mashuhuri.
When they came to the Jordan that is in the land of Canaan, the Reubenites and the Gadites and the half tribe of Manasseh built an altar beside the Jordan, a very large and prominent altar.
11 Watu wa Israeli walisikia habari hizo na wakaseam, “Tazama! Watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wamejenga madhabahu mbele ya nchi ya Kanaani, huko Gelilothi, katika mkoa karibu na Yordani, katika upande ambao ni miliki ya watu wa Israeli.”
The people of Israel heard about this and said, “Look! The people of Reuben, Gad, and the half tribe of Manasseh have built an altar at the front of the land of Canaan, at Geliloth, in the region near the Jordan, on the side that belongs to the people of Israel.”
12 Wakati watu wa Israeli waliposikia hivyo, kusanyiko lote la watu wa Israeli walikusanyika kwa pamoja huko Shilo ili wapande kupigana vita nao.
When the people of Israel heard of it, the whole assembly of the people of Israel gathered together at Shiloh to go up to make war against them.
13 Kisha watu wa Israeli walituma wajumbe kwa Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi. Walimtuma pia Finehasi mwana wa Eliezari, kuhani,
Then the people of Israel sent messengers to the Reubenites, the Gadites, and the half tribe of Manasseh, in the land of Gilead. They also sent Phinehas son of Eleazar, the priest,
14 na viongozi kumi pamoja naye, mmoja kutoka katika familia za mababa wa Israeli, na kila mmoja wao alikuwa ni kiongozi wa ukoo miongoni mwa watu wa Israeli.
and with him ten leaders, one from each of the tribal families of Israel, and every one of them was the head of a family among the clan of Israel.
15 Walienda kwa watu wa Rubeni, Gadi, na nusu ya kabila la Manase, katika nchi ya Gileadi, na wakawaambia:
They came to the people of Reuben, Gad, and the half tribe of Manasseh, in the land of Gilead, and they spoke to them:
16 “Kusanyiko lote la Yahweh linasema kuwa, ' Ni jambo gani hili lisilo la uaminifu ambalo mmelitenda kinyume na Mungu wa Israeli, kwa kugeuka badala ya kumfuata Yahweh siku hii na kujijengea wenyewe madhabahu katika uasi kinyume na Yahweh katika siku hii?
“The whole assembly of Yahweh says this, 'What is this unfaithfulness that you have committed against the God of Israel, by turning this day from following Yahweh by building yourself an altar this day in rebellion against Yahweh?
17 Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha? Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo. Kwa ajili ya dhambi ile lilikuja pigo kwa kusanyiko lote la Yahweh.
Was our sin at Peor not enough for us? Yet we have not even now cleansed ourselves from it. For that sin there came a plague on the assembly of Yahweh.
18 Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh? Kama mtaasi kinyume na Yahweh leo, kesho atakuwa na hasira na kusanyiko lote la Israeli.
Must you also turn away from following Yahweh at this present day? If you also rebel against Yahweh today, tomorrow he will be angry with the whole assembly of Israel.
19 Na kama nchi ambayo mnaimiliki imetiwa unajisi, basi mwaweza kuvuka katika nchi ambayo Sanduku la Yahweh lasimama na mjichukulie kwa ajili yenu umiliki miongoni mwetu. Hamtakiwi kuasi kinyume na Yahweh tu, wala kuasi kinyume chetu kwa kujenga madhabahu kwa ajili yenu wenyewe badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wa wetu.
If the land that you possess is defiled, then you should pass over into the land where Yahweh's tabernacle stands and take for yourselves a possession among us. Only do not rebel against Yahweh, nor rebel against us by building an altar for yourselves other than the altar of Yahweh our God.
20 Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli? Mtu yule hakuangamia peke yake kwa uovu wake.
Did not Achan son of Zerah break faith in the matter of those things that had been reserved for God? Did not wrath fall on all the people of Israel? That man did not perish alone for his iniquity.'”
21 Kisha makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wakawajibu wazee wa koo za Israeli:
Then the tribes of Reuben, Gad, and the half tribe of Manasseh replied in answer to the heads of the clans of Israel:
22 “Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yahweh, Mungu Mwenye nguvu! Yeye anajua, na Israeli naijue yenyewe! Kama ilikuwa ni katika uasi au katika kuvunja imani kinyume na Yahweh, msituache hai katika siku hii ya leo
“The Mighty One, God, Yahweh! The Mighty One, God, Yahweh!—He knows, and let Israel itself know! If it was in rebellion or in breach of faith against Yahweh, do not spare us on this day
23 kwa ajili ya kujenga madhabahu ili tugeuka na kuacha kumfuata Yahweh. Kama tumejenga madhabahu hii ili kutoa juu yake sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka, au sadaka ya amani, basi Yahweh na atuadhibu.
for having built an altar to turn ourselves away from following Yahweh. If we built that altar in order to offer on it burnt offerings, grain offerings, or peace offerings, then let Yahweh make us pay for it.
24 La hasha, tulifanya hivyo kwa sababu ya hofu kwamba katika siku zijazo watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu, ' Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?
No! We did it for fear that in time to come your children might say to our children, 'What have you to do with Yahweh, the God of Israel?
25 Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani kuwa mpaka kati yetu na ninyi. Ninyi watu wa Rubeni na watu wa Gadi, hamna kitu chochote naYahweh.' Na kwa hali hiyo, watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.
For Yahweh has made the Jordan a border between us and you. You people of Reuben and people of Gad, you have nothing to do with Yahweh.' So your children might make our children cease to worship Yahweh.
26 Basi tukasema, 'Hebu na tujenge sasa madhabahu, si kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa wala si kwa sadaka yoyote ile,
So we said, 'Let us now build an altar, not for burnt offerings nor for any sacrifices,
27 ila iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi, na kati ya kizazi chetu baada yetu, kwamba tutafanya ibada ya Yahweh mbele yake, pamoja na sadaka zetu za kuteketezwa na dhabihu zetu na sadaka zetu za amani, ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, “Hamna sehemu katika Yahweh.”'
but to be a witness between us and you, and between our generations after us, that we will perform the service of Yahweh before him, with our burnt offerings and with our sacrifices and with our peace offerings, so that your children will never say to our children in time to come, “You have no share in Yahweh.”'
28 Hivyo tukasema, 'kama hili litasemwa kwa kwetu au kwa watoto wetu katika siku zijazo, tutasema, “Tazama! Huu ni mfano wa madhabahu ya Yahweh, ambayo mababu zetu waliifanya, si kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, wala si kwa dhabihu, bali kwa ajili ya ushahidi kati yetu ninyi.”
So we said, 'If this should be said to us or to our descendants in time to come, we would say, “Look! This is a copy of the altar of Yahweh, which our ancestors made, not for burnt offerings, nor for sacrifices, but as a witness between us and you.”
29 Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh, na kuacha kumfuata yeye kwa kujenga madhabahu kwa ajili sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka ya nafaka, au kwa dhabihu, badala ya madhabahu ya Yahweh Mungu wetu ambayo iko mbele ya hema la kukutania.'”
May it be far from us that we should rebel against Yahweh, and today turn away from following him by building an altar for burnt offering, for grain offering, or for sacrifice, other than the altar of Yahweh our God that is before his tabernacle.'”
30 Finehasi kuhani na viongozi wa watu, ambao ni wakuu wa koo za Waisraeli ambao walikuwa pamoja naye, waliposikia maneno amabayo watu wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, kwamba yalikuwa ni mazuri machoni pao.
When Phinehas the priest and the leaders of the people, that is, the heads of the clans of Israel who were with him, heard the words that the people of Reuben, Gad, and Manasseh said, that it was good in their eyes.
31 Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani aliwaambia watu wa Rubeni, Gadi na Manase, “Leo tumejua kwambaYahweh yuko miongoni mwetu, kwa kuwa hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye. Sasa, mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.”
Phinehas son of Eleazar the priest said to the people of Reuben, Gad, and Manasseh, “Today we know that Yahweh is among us, because you have not committed this breach of faith against him. Now you have rescued the people of Israel out of the hand of Yahweh.”
32 Kisha Finehasi mwana wa Eliazeri kuhani, na viongozi walirudi kutoka kwa Warubeni na Wagadi, kutoka katika nchi ya Gileadi, na kurudi katika nchi ya Kanaani, kwa watu wa Israeli, na waliwaletea taarifa.
Then Phinehas son of Eleazar the priest, and the leaders returned from the Reubenites and the Gadites, out of the land of Gilead, back to the land of Canaan, to the people of Israel, and brought back word to them.
33 Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu wa Israeli. Watu wa Israeli walimbarikia Mungu na hawakuendelea kusema tena juu ya kuinua vita dhidi ya Warubeni na Wagadi, ili kuiharibu nchi ambayo walikuwa wanaishi.
Their report was good in the eyes of the people of Israel. The people of Israel blessed God and spoke no more about making war against the Reubenites and the Gadites, in order to destroy the land where they had settled.
34 Warubeni na Wagadi waliita ile madhabahu “Ushahidi,” kwa kuwa walisema, “Ni ushahidi miongoni mwetu kuwa Yahweh ni Mungu.”
The Reubenites and the Gadites named the altar “Witness,” for they said, “It is a witness between us that Yahweh is God.”

< Yoshua 22 >