< Yoshua 12 >

1 Basi hawa ndio wafalme wa nchi, ambao watu wa Israeli walishindwa. Waisraeli walichukua miliki ya nchi katika upande wa mashariki mwa Yordani sehemu ambako jua huchomoza, kutoka bonde la Mto Arnoni hadi Mlima Hermoni, na nchi yote ya Araba kuelekea kusini.
Now these [are] the kings of the land, which the children of Israel smote, and possessed their land on the other side Jordan toward the rising of the sun, from the river Arnon unto mount Hermon, and all the plain on the east:
2 Sihoni, mfalme wa Waamori, aliishi katika Heshiboni. Alitawala kutoka Aroeri, ambayo iko juu ya bonde la Arnoni kutoka katikati ya bonde, na nusu ya Geleadi kushuka mpaka Mto Yaboki katika mpaka wa Waamori.
Sihon king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, [and] ruled from Aroer, which [is] upon the bank of the river Arnon, and from the middle of the river, and from half Gilead, even unto the river Jabbok, [which is] the border of the children of Ammon;
3 Sihoni pia alitawala juu ya Araba mpaka Bahari ya Kinerethi, kwenda mashariki, kuelekea Bahari ya Araba (Bahari ya Chumvi) upande wa mashariki, hadi huko Bethi Yeshimothi na upande wa kusini, kuelekea chini ya miteremko wa Mlima Pisiga.
And from the plain to the sea of Chinneroth on the east, and unto the sea of the plain, [even] the salt sea on the east, the way to Beth-jeshimoth; and from the south, under Ashdoth-pisgah:
4 Ogu, mfalme wa Bashani, mmoja kati ya mabaki ya Rephaimu, aliyeishi huko Shatarothi na Edrei.
And the coast of Og king of Bashan, [which was] of the remnant of the giants, that dwelt at Ashtaroth and at Edrei,
5 Alitawala juu ya Mlima Hermoni, Saleka, na Bahani yote, hadi mpaka wa watu wa Geshuri na Wamakathi, na nusu ya Gleadi, hadi kufika mpaka wa Sihohi, mfalme wa Heshboni.
And reigned in mount Hermon, and in Salcah, and in all Bashan, unto the border of the Geshurites and the Maachathites, and half Gilead, the border of Sihon king of Heshbon.
6 Musa mtumishi wa Yahweh, na watu wa Israeli walikuwa wamewashinda, na Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa nchi kama mali ya Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.
Them did Moses the servant of the LORD and the children of Israel smite: and Moses the servant of the LORD gave it [for] a possession unto the Reubenites, and the Gadites, and the half tribe of Manasseh.
7 Hawa ndio wafalme wa nchi ambayo Yoshua na watu wa Israeli waliwashinda katika upande wa magharibi mwa mto Yordani, kutoka Baali Gadi katika bonde karibu na Lebanoni hadi Mlima Halaki karibu na Edom. Yoshua aliyapa nchi makabila ya Israeli ili yaimiliki.
And these [are] the kings of the country which Joshua and the children of Israel smote on this side Jordan on the west, from Baal-gad in the valley of Lebanon even unto the mount Halak, that goeth up to Seir; which Joshua gave unto the tribes of Israel [for] a possession according to their divisions;
8 Aliwapa nchi ya milima, tambarare, Araba, sehemu za milima, nyika na Negevu, nchi ya Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.
In the mountains, and in the valleys, and in the plains, and in the springs, and in the wilderness, and in the south country; the Hittites, the Amorites, and the Canaanites, the Perizzites, the Hivites, and the Jebusites:
9 Wafalme hawa walikuwa ni mfalme wa Yeriko, mfalme wa Ai iliyo karibu na Betheli,
The king of Jericho, one; the king of Ai, which [is] beside Beth-el, one;
10 mfalme wa Yerusalemu, mfalme wa Enaimu,
The king of Jerusalem, one; the king of Hebron, one;
11 mfalme wa Yarmuthi, mfalme wa Lakishi,
The king of Jarmuth, one; the king of Lachish, one;
12 mfalme wa Egloni, mfalme wa Gezeri,
The king of Eglon, one; the king of Gezer, one;
13 mfalme wa Debiri, mfalme wa Gederi,
The king of Debir, one; the king of Geder, one;
14 mfalme wa Horima, mfalme wa Aradi,
The king of Hormah, one; the king of Arad, one;
15 mfalme wa Libna, mfalme wa Adula,
The king of Libnah, one; the king of Adullam, one;
16 mfalme wa Makeda, mfalme wa Betheli,
The king of Makkedah, one; the king of Beth-el, one;
17 mfalme wa Tapua, mfalme wa Heferi,
The king of Tappuah, one; the king of Hepher, one;
18 mfalme wa Afeki, mfalme wa Lasharoni,
The king of Aphek, one; the king of Lasharon, one;
19 mfalme wa Madoni, mfalme wa Hazori,
The king of Madon, one; the king of Hazor, one;
20 mfalme wa Shimroni - Meroni, mfalme wa Akshafu.
The king of Shimron-meron, one; the king of Achshaph, one;
21 mfalme wa Taanaki, mfalme wa Megido,
The king of Taanach, one; the king of Megiddo, one;
22 mfalme wa Kedeshi, mfalme wa Jokineamu katika Karmeli,
The king of Kedesh, one; the king of Jokneam of Carmel, one;
23 mfalme wa Dori katika Nafutali Dori, mfalme Goyimu katika Giligali, na
The king of Dor in the coast of Dor, one; the king of the nations of Gilgal, one;
24 mfalme Tiriza. Hesabu ya wafalme ilikuwa ni thelathini na moja kwa ujumla wake.
The king of Tirzah, one: all the kings thirty and one.

< Yoshua 12 >