< Yohana 3 >

1 Basi kulikuwa na Farisayo ambaye jina lake Nikodemo, mmoja wa wajumbe wa baraza la Wayahudi.
There was a man of the Pharisees, named Nicodemus, a ruler of the Jews:
2 Mtu huyu alimwendea Bwana Yesu usiku na akamwambia, “Rabi, tunajua ya kuwa u mwalimu kutoka kwa Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kutenda ishara hizi zote Mungu asipokuwa pamoja naye.”
The same came to Jesus by night, and said to him, Rabbi, we know that you are a teacher come from God: for no man can do these miracles that you do, except God be with him.
3 Yesu akamjibu, “Amini, amini, mtu hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”
Jesus answered and said to him, Truly, truly, I say to you, Except a man be born again, he cannot see the kingdom of God.
4 Nikodemo akasema,” Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili na kuzaliwa, je anaweza?”
Nicodemus says to him, How can a man be born when he is old? can he enter the second time into his mother’s womb, and be born?
5 Yesu akajibu, “Amini, amini mtu sipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
Jesus answered, Truly, truly, I say to you, Except a man be born of water and of the Spirit, he cannot enter into the kingdom of God.
6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili, na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.
That which is born of the flesh is flesh; and that which is born of the Spirit is spirit.
7 Usishangae kwa sababu nilikuwambia, 'ni lazima kuzaliwa mara ya pili.'
Marvel not that I said to you, You must be born again.
8 Upepo huvuma popote upendapo na sauti yake mwaisikia, lakini hamjui utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo hali ya kila aliyezaliwa na roho.
The wind blows where it wants, and you hear the sound thereof, but can not tell from where it comes, and where it goes: so is every one that is born of the Spirit.
9 Nikodemo akajibu, kwa kusema, “Mambo haya yawezekanaje?”
Nicodemus answered and said to him, How can these things be?
10 Yesu akamjibu, “Wewe u mwalimu wa Israeli, hata hauyajui mambo haya?
Jesus answered and said to him, Are you a master of Israel, and know not these things?
11 Amini, amini, nakuambia, kile tunachokifahamu twakishuhudia kwa kile tulichokiona. Lakini hampokei ushuhuda wetu.
Truly, truly, I say to you, We speak that we do know, and testify that we have seen; and you receive not our witness.
12 Kama nimewambia mambo ya hapa duniani na hamuamini, mtawezaje kuamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni?
If I have told you earthly things, and you believe not, how shall you believe, if I tell you of heavenly things?
13 Maana hakuna aliyepanda juu kutoka mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka, Mwana wa Adamu.
And no man has ascended up to heaven, but he that came down from heaven, even the Son of man which is in heaven.
14 Kama vile Musa alivyomwinua nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu lazima ainuliwe,
And as Moses lifted up the serpent in the wilderness, even so must the Son of man be lifted up:
15 ili kwamba wote watakaomwamini wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
That whoever believes in him should not perish, but have eternal life. (aiōnios g166)
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, kwamba akamtoa mwanae wa pekee, ili kwamba mtu yeyote amwaminiye asiangamie bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
For God so loved the world, that he gave his only begotten Son, that whoever believes in him should not perish, but have everlasting life. (aiōnios g166)
17 Kwa sababu Mungu hakumtuma mwanae duniani ili auhukumu ulimwengu, bali kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye.
For God sent not his Son into the world to condemn the world; but that the world through him might be saved.
18 Amwaminiye Yeye hatahukumiwa. Yeye asiyemwamini tayari ameshahukumiwa kwa sababu hajaliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
He that believes on him is not condemned: but he that believes not is condemned already, because he has not believed in the name of the only begotten Son of God.
19 Hii ndiyo sababu ya hukumu, ya kwamba nuru imekuja ulimwenguni, lakini wanadamu wakapenda giza zaidi ya nuru kwa sababu matendo yao yalikuwa maovu.
And this is the condemnation, that light is come into the world, and men loved darkness rather than light, because their deeds were evil.
20 kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru wala haji nuruni ili matendo yake yasije yakawekwa wazi.
For every one that does evil hates the light, neither comes to the light, lest his deeds should be reproved.
21 Lakini, yeye atendaye kweli huja kwenye nuru ili matendo yake yaonekane kwamba yametendwa kwa utiifu wa Mungu.
But he that does truth comes to the light, that his deeds may be made manifest, that they are worked in God.
22 Baada ya haya, Yesu pamoja na wanafunzi walienda katika nchi ya Yudea. Huko alitumia muda pamoja nao na alikuwa akibatiza.
After these things came Jesus and his disciples into the land of Judaea; and there he tarried with them, and baptized.
23 Sasa Yohana pia alikuwa akibatiza huko Ainea karibu na Salim maana kulikuwa na maji mengi pale. Watu walikuwa wakija kwake na kubatizwa,
And John also was baptizing in Aenon near to Salim, because there was much water there: and they came, and were baptized.
24 kwa kuwa Yohana alikuwa hajatupwa gerezani.
For John was not yet cast into prison.
25 Kisha palitokea mabishano kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi kuhusu sikukuuu za utakaso.
Then there arose a question between some of John’s disciples and the Jews about purifying.
26 Wakaenda kwa Yohana wakamwambia, “Rabi, yeye uliyekuwa naye ng'ambo ya Mto Yorodani, yeye uliyeshuhudia habari zake, tazama, anabatiza na wote wanaenda wanamfuata.”
And they came to John, and said to him, Rabbi, he that was with you beyond Jordan, to whom you bore witness, behold, the same baptizes, and all men come to him.
27 Yohana akajibu mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa kama amepewa kutoka mbinguni.
John answered and said, A man can receive nothing, except it be given him from heaven.
28 Ninyi wenyewe mwashuhudia kuwa nalisema kuwa, 'mimi sio Kristo', badala yake nilisema, 'nimetumwa mbele yake.'
You yourselves bear me witness, that I said, I am not the Christ, but that I am sent before him.
29 Yeye aliye na bibi arusi ni bwana harusi. Sasa rafiki wa bwana arusi, asimamaye na kusikiliza hufurahia sana kwa sababu ya sauti ya bwana arusi. Hii sasa ni furaha yangu iliyotimilika.
He that has the bride is the bridegroom: but the friend of the bridegroom, which stands and hears him, rejoices greatly because of the bridegroom’s voice: this my joy therefore is fulfilled.
30 Anapaswa kuzidi, nami napaswa kupungua.
He must increase, but I must decrease.
31 Yeye atokaye juu, yu juu ya yote. Yeye aliye wa ulimwengu anatoka ulimwenguni na huongea mambo ya ki ulimwengu. Yeye atokaye mbinguni yuko juu ya yote.
He that comes from above is above all: he that is of the earth is earthly, and speaks of the earth: he that comes from heaven is above all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna apokeaye ushuhuda wake.
And what he has seen and heard, that he testifies; and no man receives his testimony.
33 Yeye aliye pokea ushuhuda wake amehakikisha kuwa Mungu ni mkweli.
He that has received his testimony has set to his seal that God is true.
34 Kwa sababu yeye aliyetumwa na Mungu huongea maneno ya Mungu. Kwa kuwa hampi Roho kwa kipimo.
For he whom God has sent speaks the words of God: for God gives not the Spirit by measure to him.
35 Baba humpenda Mwana na amempa vitu vyote mikononi mwake.
The Father loves the Son, and has given all things into his hand.
36 Yeye amwaminiye Mwana anao uzima wa milele, lakini kwa yeye asiye mtii Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hushikamana juu yake. (aiōnios g166)
He that believes on the Son has everlasting life: and he that believes not the Son shall not see life; but the wrath of God stays on him. (aiōnios g166)

< Yohana 3 >