< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said,
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
I know [it is] so of a truth: but how should man be just with God?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
If he will contend with him, he cannot answer him one of a thousand.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
[He is] wise in heart, and mighty in strength: who hath hardened [himself] against him, and hath prospered?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Which removeth the mountains, and they know not: which overturneth them in his anger.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Which shaketh the earth out of her place, and the pillars thereof tremble.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Which commandeth the sun, and it riseth not; and sealeth up the stars.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Which alone spreadeth out the heavens, and treadeth upon the waves of the sea.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Which maketh Arcturus, Orion, and Pleiades, and the chambers of the south.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Which doeth great things past finding out; yea, and wonders without number.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Lo, he goeth by me, and I see [him] not: he passeth on also, but I perceive him not.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Behold, he taketh away, who can hinder him? who will say unto him, What doest thou?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
[If] God will not withdraw his anger, the proud helpers do stoop under him.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
How much less shall I answer him, [and] choose out my words [to reason] with him?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Whom, though I were righteous, [yet] would I not answer, [but] I would make supplication to my judge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
If I had called, and he had answered me; [yet] would I not believe that he had hearkened unto my voice.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
For he breaketh me with a tempest, and multiplieth my wounds without cause.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
He will not suffer me to take my breath, but filleth me with bitterness.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
If [I speak] of strength, lo, [he is] strong: and if of judgment, who shall set me a time [to plead]?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
If I justify myself, mine own mouth shall condemn me: [if I say], I [am] perfect, it shall also prove me perverse.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
[Though] I [were] perfect, [yet] would I not know my soul: I would despise my life.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
This [is] one [thing], therefore I said [it], He destroyeth the perfect and the wicked.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
If the scourge slay suddenly, he will laugh at the trial of the innocent.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
The earth is given into the hand of the wicked: he covereth the faces of the judges thereof; if not, where, [and] who [is] he?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Now my days are swifter than a post: they flee away, they see no good.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
They are passed away as the swift ships: as the eagle [that] hasteth to the prey.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
If I say, I will forget my complaint, I will leave off my heaviness, and comfort [myself: ]
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
I am afraid of all my sorrows, I know that thou wilt not hold me innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
[If] I be wicked, why then labour I in vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
If I wash myself with snow water, and make my hands never so clean;
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Yet shalt thou plunge me in the ditch, and mine own clothes shall abhor me.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
For [he is] not a man, as I [am, that] I should answer him, [and] we should come together in judgment.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Neither is there any daysman betwixt us, [that] might lay his hand upon us both.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Let him take his rod away from me, and let not his fear terrify me:
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
[Then] would I speak, and not fear him; but [it is] not so with me.

< Ayubu 9 >