< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Then answered Bildad the Shuhite, and saide,
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Howe long wilt thou talke of these things? and howe long shall the wordes of thy mouth be as a mightie winde?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Doeth God peruert iudgement? or doeth the Almightie subuert iustice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
If thy sonnes haue sinned against him, and he hath sent them into the place of their iniquitie,
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Yet if thou wilt early seeke vnto God, and pray to the Almightie,
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
If thou be pure and vpright, then surely hee will awake vp vnto thee, and he wil make the habitation of thy righteousnesse prosperous.
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
And though thy beginning be small, yet thy latter ende shall greatly encrease.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Inquire therefore, I pray thee, of the former age, and prepare thy selfe to search of their fathers.
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(For we are but of yesterday, and are ignorant: for our dayes vpon earth are but a shadowe)
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Shall not they teach thee and tell thee, and vtter the wordes of their heart?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Can a rush grow without myre? or can ye grasse growe without water?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Though it were in greene and not cutte downe, yet shall it wither before any other herbe.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
So are the paths of al that forget God, and the hypocrites hope shall perish.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
His confidence also shalbe cut off, and his trust shalbe as the house of a spyder.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
He shall leane vpon his house, but it shall not stand: he shall holde him fast by it, yet shall it not endure.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
The tree is greene before the sunne, and the branches spread ouer the garden thereof.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
The rootes thereof are wrapped about the fountaine, and are folden about ye house of stones.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
If any plucke it from his place, and it denie, saying, I haue not seene thee,
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
Beholde, it will reioyce by this meanes, that it may growe in another molde.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Behold, God will not cast away an vpright man, neither will he take the wicked by the hand,
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Till he haue filled thy mouth with laughter, and thy lippes with ioy.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
They that hate thee, shall be clothed with shame, and the dwelling of the wicked shall not remaine.

< Ayubu 8 >