< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
But Job answered and said,
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
Oh that my grief were throughly weighed, and my calamity laid in the balances together!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now it would be heavier than the sand of the sea: therefore my words are swallowed up.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty [are] within me, the poison whereof drinketh up my spirit: the terrors of God do set themselves in array against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Doth the wild ass bray when he hath grass? or loweth the ox over his fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Can that which is unsavoury be eaten without salt? or is there [any] taste in the white of an egg?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
The things [that] my soul refused to touch [are] as my sorrowful meat.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
Oh that I might have my request; and that God would grant [me] the thing that I long for!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
Even that it would please God to destroy me; that he would let loose his hand, and cut me off!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Then should I yet have comfort; yea, I would harden myself in sorrow: let him not spare; for I have not concealed the words of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What [is] my strength, that I should hope? and what [is] mine end, that I should prolong my life?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
[Is] my strength the strength of stones? or [is] my flesh of brass?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
[Is] not my help in me? and is wisdom driven quite from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
To him that is afflicted pity [should be shewed] from his friend; but he forsaketh the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
My brethren have dealt deceitfully as a brook, [and] as the stream of brooks they pass away;
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Which are blackish by reason of the ice, [and] wherein the snow is hid:
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
What time they wax warm, they vanish: when it is hot, they are consumed out of their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
The paths of their way are turned aside; they go to nothing, and perish.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The troops of Tema looked, the companies of Sheba waited for them.
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They were confounded because they had hoped; they came thither, and were ashamed.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For now ye are nothing; ye see [my] casting down, and are afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Did I say, Bring unto me? or, Give a reward for me of your substance?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
Or, Deliver me from the enemy’s hand? or, Redeem me from the hand of the mighty?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Teach me, and I will hold my tongue: and cause me to understand wherein I have erred.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How forcible are right words! but what doth your arguing reprove?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Do ye imagine to reprove words, and the speeches of one that is desperate, [which are] as wind?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Yea, ye overwhelm the fatherless, and ye dig [a pit] for your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Now therefore be content, look upon me; for [it is] evident unto you if I lie.
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Return, I pray you, let it not be iniquity; yea, return again, my righteousness [is] in it.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there iniquity in my tongue? cannot my taste discern perverse things?

< Ayubu 6 >