< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Vai tu levijatanu vari ķert ar makšķeri, jeb viņa mēli ar dziļi iemestu virvi?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Vai tu viņam riņķi māki likt nāsīs un ar asmeni izdurt viņa žaunas?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Vai tu domā, ka tas tevis daudz lūgsies un labus vārdus uz tevi runās?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Vai viņš derēs derību ar tevi, ka tu viņu vari ņemt par mūžīgu vergu?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Vai tu ar viņu varēsi spēlēties kā ar putniņu, jeb viņu saistīsi savām meitām?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Vai zvejnieku biedrībā viņu pārdod, vai viņu izdala pircējiem?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Vai tu viņa ādu vari piedurt pilnu ar šķēpiem, jeb viņa galvu ar žebērkļiem?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Kad tu savu roku viņam pieliksi, tad pieminēsi, kāds tas karš, un vairs to nedarīsi.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Redzi, tāda cerība ir velti; jau viņu ieraugot krīt gar zemi.
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Neviens nav tik drošs, viņu kaitināt, - kas tad būtu, kas Man varētu celties pretim?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Kas Man ko laba papriekš darījis, ka Man to bija atmaksāt? Kas ir apakš visām debesīm, tas Man pieder.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Un lai vēl pieminu viņa locekļus, stiprumu un viņa vareno augumu.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Kas drīkstētu viņa bruņas atsegt, kas līst viņa zobu starpā?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Kas viņa vaiga žokļus var atplēst? Ap viņa zobiem ir briesmas.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Lepni ir viņa bruņu zvīņas, cieti kā ar zieģeli saspiesti kopā.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
Viens tik tuvu pie otra, ka ne vējš netiek starpā.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Tie līp viens pie otra, un turas kopā, ka nešķiras.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Viņš šķauda ugunis, un viņa acis ir kā rīta blāzmas stari.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
No viņa mutes šaujās ugunis, degošas dzirksteles no tās izlec.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
No viņa nāsīm iziet dūmi kā no verdoša poda un katla.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Viņa dvaša varētu iededzināt ogles, un liesmas iziet no viņa mutes.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Viņa kakls ir visai stiprs, un viņa priekšā lec bailes.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Viņa miesas locekļi kā sakalti, tie turas cieti kopā, ka nevar kustināt.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Viņa sirds ir cieta kā akmens un cieta kā apakšējais dzirnu akmens.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Kad viņš ceļas, tad stiprie izbīstas, no bailēm tie paģībst.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Kad viņam cērt ar zobenu, tas nekož, nedz šķēps, ne bulta, ne žebērklis.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Dzelzs priekš viņa kā salmi, un varš kā sapraulējis koks.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
Bulta viņu neaiztrieks; lingas akmeņi viņam ir kā pelus.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Lielas bozes viņam ir kā pelus, viņš smejas, kad šķēps svelpj.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Viņa pavēderē asi kasīkļi, un kā ar ecešām viņš brauc pa dubļiem.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Viņš dara, ka dziļumi verd kā pods, un sajauc jūru kā zalves virumu.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Kur viņš gājis ceļš spīd; tie ūdens viļņi ir kā sudraboti.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Virs zemes cits viņam nav līdzinājams, viņš tāds radīts, ka nebīstas.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Viss, kas ir augsts, viņam nav nekas; viņš visu lepno zvēru ķēniņš.

< Ayubu 41 >