< Ayubu 37 >

1 Hakika, moyo wangu hutetemeka kwa hili; umeondolewa kutoka katika sehemu yake.
A ESTO también se espanta mi corazón, y salta de su lugar.
2 Sikia, Ee, Sikia kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.
Oid atentamente su voz terrible, y el sonido que sale de su boca.
3 Huiagiza sauti chini ya mbingu yote, na huutuma mwanga wake katika mipaka ya dunia.
Debajo de todos los cielos lo dirige, y su luz hasta los fines de la tierra.
4 Sauti huunguruma baada yake; yeye huunguruma kwa sauti ya ukuu wake; hauzuii mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika.
Después de ella bramará el sonido, tronará él con la voz de su magnificencia; y aunque sea oída su voz, no los detiene.
5 Mungu huunguruma kwa sauti yake kwa namna ya ajabu; yeye hufanya mambo makubwa ambayo sisi hatuwezi kuyafahamu.
Tronará Dios maravillosamente con su voz; él hace grandes cosas, que nosotros no entendemos.
6 Kwa kuwa huiambia theluji, 'Angukeni juu ya dunia'; hali kadhalika kwa manyunyu ya mvua, 'Iweni manyunyu makubwa ya mvua.'
Porque á la nieve dice: Desciende á la tierra; también á la llovizna, y á los aguaceros de su fortaleza.
7 Huuzuia mkono wa kila mtu usifanye kazi, ili kwamba watu wote aliowaumba wataona matendo yake.
Así hace retirarse á todo hombre, para que los hombres todos reconozcan su obra.
8 Kisha hayawani huenda na kujificha na kukaa katika mapango yake.
La bestia se entrará en su escondrijo, y estaráse en sus moradas.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.
Del mediodía viene el torbellino, y el frío de los vientos del norte.
10 Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu; upana wa maji umeganda kama chuma.
Por el soplo de Dios se da el hielo, y las anchas aguas son constreñidas.
11 Hakika, huyapima mawingu manene yenye unyevu; yeye huusambaza mwanga wake katika mawingu.
Regando también llega á disipar la densa nube, y con su luz esparce la niebla.
12 Yeye huyazungusha mawingu kwa uongozi wake, ili yafanye chochote anayoyaagiza juu ya uso wote wa ulimwengu.
Asimismo por sus designios se revuelven las nubes en derredor, para hacer sobre la haz del mundo, en la tierra, lo que él les mandara.
13 Huyafanya haya yote yatokee; wakati mwingine hutokea kwa ajili ya kusahihisha, wakati mwingine kwa ajili ya nchi yake, na wakati mwingine ni kwa matendo ya agano la uaminifu.
Unas veces por azote, otras por causa de su tierra, otras por misericordia las hará parecer.
14 Yasikilize haya, Ayubu; acha na ufikiri juu matendo ya ajabu ya Mungu.
Escucha esto, Job; repósate, y considera las maravillas de Dios.
15 Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?
¿Supiste tú cuándo Dios las ponía en concierto, y hacía levantar la luz de su nube?
16 Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?
¿Has tú conocido las diferencias de las nubes, las maravillas del Perfecto en sabiduría?
17 Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?
¿Por qué están calientes tus vestidos cuando se fija el [viento del] mediodía sobre la tierra?
18 Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?
¿Extendiste tú con él los cielos, firmes como un espejo sólido?
19 Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye, kwa kuwa hatuwezi kutoa hoja zetu katika mpangilio kwasababu ya kiza katika akili zetu.
Muéstranos qué le hemos de decir; [porque] nosotros no podemos componer [las ideas] á causa de las tinieblas.
20 Je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye? Je mtu angependa kumezwa?
¿Será preciso contarle cuando yo hablaré? Por más que el hombre razone, quedará como abismado.
21 Sasa, watu hawawezi kulitazama jua wakati linang'aa katika anga baada ya upepo kupita katikati yake na umelisafisha kwa mawingu yake.
He aquí aún: no se puede mirar la luz esplendente en los cielos, luego que pasa el viento y los limpia,
22 Kutoka upande wa kaskazini hutokea fahari ya dhahabu - juu ya Mungu kuna ukuu wa kutisha.
Viniendo de la parte del norte la dorada claridad. En Dios hay una majestad terrible.
23 Na kuhusu Mwenye nguvu, hatuwezi kumpata; yeye ni mkuu katika nguvu na haki. Yeye hatesi watu.
El [es] Todopoderoso, al cual no alcanzamos, grande en potencia; y en juicio y en multitud de justicia no afligirá.
24 Hivyo basi, watu humwogopa. Yeye huwa hawajali wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.”
Temerlo han por tanto los hombres: él no mira á los sabios de corazón.

< Ayubu 37 >