< Ayubu 36 >

1 Elihu aliendelea na kusema,
Elihu continued on and said,
2 “Niruhusu niseme kidogo zaidi, nami nitakuonesha baadhi ya mambo kwasababu nina maneno machache ya kusema kwa ajili ya Mungu.
“Permit me to speak a little longer, and I will show you some things because I have a little more to say in defense of God.
3 Nitapata maarifa yangu kutoka mbali; nitatambua kwamba haki ni ya Muumba wangu.
I will obtain my knowledge from far off; I will acknowledge that righteousness belongs to my Maker.
4 Kwa kweli, maneno yangu hayatakuwa ya uongo; mtu fulani aliyekomaa katika maarifa yu pamoja nawe.
For indeed, my words will not be false; someone who is mature in knowledge is with you.
5 Angalia, Mungu ni mwenye nguvu, na hamdharau mtu yeyote; yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu.
See, God is mighty, and despises no one; he is mighty in strength of understanding.
6 Yeye huwa hayahifadhi maisha ya watu waovu bali badala yake hufanya yaliyo ya haki kwa wale wanaoteseka.
He does not preserve the life of wicked people but instead does what is right for those who suffer.
7 Haondoi macho yake kwa wenye haki bali badala yake huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme milele, nao wameinuliwa juu.
He does not withdraw his eyes from righteous people but instead sets them on thrones like kings forever, and they are lifted up.
8 Ikiwa wamefungwa minyororo na kunaswa katika kamba za mateso,
If they are bound in chains and trapped in cords of suffering,
9 kisha huwafunulia kile walichokifanya, na maovu yao na kiburi chao.
then he reveals to them what they have done, and their transgressions and their pride.
10 Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake, na huwaamuru wageuke kutoka katika uovu.
He also opens their ears to his instruction, and commands them to turn back from iniquity.
11 Ikiwa watamsikiliza na kumwabudu yeye, wataishi katika mafanikio katika siku zao, na miaka yao katika hali ya kuridhika.
If they listen to him and worship him, they will spend their days in prosperity, their years in contentment.
12 Hata hivyo, kama hawatasikiliza, wataangamia kwa upanga; watakufa kwasababu hawana maarifa.
However, if they do not listen, they will perish by the sword; they will die because they have no knowledge.
13 Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo; hawaombi msaada hata wakati ambapo Mungu huwafunga.
Those who are godless in heart store up their anger; they do not cry out for help even when God ties them up.
14 Hawa hufa katika ujana wao; na maisha yao hukoma kati ya makahaba.
They die in their youth; their lives end among the cultic prostitutes.
15 Mungu huwainua watu walioonewa kwa njia ya mateso yao; hufungua masikio yao kwa njia ya uonevu wao.
God rescues afflicted people by means of their afflictions; he opens their ears by means of their oppression.
16 Kwa hakika, yeye angependa kuwatoa ninyi katika mateso na kuwaweka katika sehemu pana ambapo hakuna masumbufu na mahali ambapo meza yenu ingewekwa ikiwa na chakula kilichojaa mafuta.
Indeed, he would like to draw you out of distress into a broad place where there is no hardship and where your table would be set with food full of fatness.
17 Lakini wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu; hukumu na haki umeziachilia.
But you are full of judgment on wicked people; judgment and justice have laid hold of you.
18 Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu; na sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.
Do not let your anger entice you to mockery, or the greatness of a ransom to turn you aside.
19 Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?
Can your wealth benefit you, so that you will not be in distress, or can all the force of your strength help you?
20 Usiutamani usiku ili utende dhambi dhidi ya wengine wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao.
Do not desire the night, to commit sin against others, when peoples are cut off in their place.
21 Uwe mwangalifu ili kwamba usigeukie dhambi kwasababu unajaribiwa kwa mateso ili kwamba ukae mbali na dhambi.
Be careful that you do not turn to sin because you are being tested by suffering so that you will stay away from sinning.
22 Angalia, Mungu ameinuliwa katika nguvu zake; ni nani aliye mwalimu kama yeye?
See, God is exalted in his power; who is a teacher like him?
23 Ni nani alishamwalekeza njia yake? Nani anayeweza kumwambia, 'Wewe umetenda mambo yasiyo ya haki?'
Who has ever instructed him about his way? Who can ever say to him, 'You have committed unrighteousness?'
24 Kumbuka kuyasifu matendo yake, ambayo watu wameyaimba.
Remember to praise his deeds, of which people have sung.
25 Watu wote wameshayatazama hayo matendo, lakini wanayaona tu matendo hayo kwa mbali sana.
All people have looked on those deeds, but they see those deeds only from far away.
26 Tazama, Mungu ni mkuu, lakini sisi hatumfahamu yeye vizuri; hesabu ya miaka yake haihesabiki.
See, God is great, but we do not understand him well; the number of his years is incalculable.
27 Kwa kuwa yeye huvuta matone ya maji ili kuyachuja kama mvua katka mvuke wake,
For he draws up the drops of water that he distills as rain from his vapor,
28 ambayo mawingu yake huyamwaga chini na kuyandondosha kwa wingi kwa mwanadamu.
which the clouds pour down and drop in abundance on mankind.
29 Hakika, kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?
Indeed, can anyone understand the extensive spread of the clouds and the thunder from his hut?
30 Angalia, hueneza mwanga wake kumzunguka na kufunika mizizi ya bahari.
See, he spreads his lightning around him and covers the roots of the sea.
31 Kwa namna hii huyahukumu mataifa na kuwapa chakula kwa wingi.
In this way he judges the peoples and gives food in abundance.
32 Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga mpaka pale anapouamuru kupiga shabaha yake.
He fills his hands with the lightning until he commands it to strike its mark.
33 Na muungurumo wake huonya kwa dhoruba, wanyama wanaweza kusikia kuja kwake.
Its thunder warns of the storm, the cattle can also hear it is coming.

< Ayubu 36 >