< Ayubu 34 >

1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
ויען אליהוא ויאמר
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
שמעו חכמים מלי וידעים האזינו לי
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
כי-אזן מלין תבחן וחך יטעם לאכל
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
משפט נבחרה-לנו נדעה בינינו מה-טוב
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
כי-אמר איוב צדקתי ואל הסיר משפטי
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
על-משפטי אכזב אנוש חצי בלי-פשע
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
מי-גבר כאיוב ישתה-לעג כמים
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
וארח לחברה עם-פעלי און וללכת עם-אנשי-רשע
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
כי-אמר לא יסכן-גבר-- ברצתו עם-אלהים
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
לכן אנשי לבב-- שמעו-לי חללה לאל מרשע ושדי מעול
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
כי פעל אדם ישלם-לו וכארח איש ימצאנו
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
אף-אמנם אל לא-ירשיע ושדי לא-יעות משפט
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
מי-פקד עליו ארצה ומי שם תבל כלה
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
אם-ישים אליו לבו רוחו ונשמתו אליו יאסף
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
יגוע כל-בשר יחד ואדם על-עפר ישוב
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
ואם-בינה שמעה-זאת האזינה לקול מלי
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
האף שונא משפט יחבוש ואם-צדיק כביר תרשיע
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
האמר למלך בליעל-- רשע אל-נדיבים
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
אשר לא-נשא פני שרים ולא נכר-שוע לפני-דל כי-מעשה ידיו כלם
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
רגע ימתו-- וחצות לילה יגעשו עם ויעברו ויסירו אביר לא ביד
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
כי-עיניו על-דרכי-איש וכל-צעדיו יראה
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
אין-חשך ואין צלמות-- להסתר שם פעלי און
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
כי לא על-איש ישים עוד-- להלך אל-אל במשפט
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
ירע כבירים לא-חקר ויעמד אחרים תחתם
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
לכן--יכיר מעבדיהם והפך לילה וידכאו
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
תחת-רשעים ספקם-- במקום ראים
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
אשר על-כן סרו מאחריו וכל-דרכיו לא השכילו
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
להביא עליו צעקת-דל וצעקת עניים ישמע
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
והוא ישקט ומי ירשע-- ויסתר פנים ומי ישורנו ועל-גוי ועל-אדם יחד
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
ממלך אדם חנף-- ממקשי עם
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
כי-אל-אל האמר נשאתי-- לא אחבל
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
בלעדי אחזה אתה הרני אם-עול פעלתי לא אסיף
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
המעמך ישלמנה כי-מאסת--כי-אתה תבחר ולא-אני ומה-ידעת דבר
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
אנשי לבב יאמרו לי וגבר חכם שמע לי
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
איוב לא-בדעת ידבר ודבריו לא בהשכיל
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
אבי--יבחן איוב עד-נצח על-תשבת באנשי-און
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
כי יסיף על-חטאתו פשע בינינו יספוק וירב אמריו לאל

< Ayubu 34 >