< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
"However, Job, Please hear my speech, and listen to all my words.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
See now, I have opened my mouth. My tongue has spoken in my mouth.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
My words shall utter the uprightness of my heart. That which my lips know they shall speak sincerely.
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
The Spirit of God has made me, and the breath of Shaddai gives me life.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
If you can, answer me. Set your words in order before me, and stand forth.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Look, I am toward God even as you are. I am also formed out of the clay.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Look, my terror shall not make you afraid, neither shall my pressure be heavy on you.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
"Surely you have spoken in my hearing, I have heard the voice of your words, saying,
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
'I am clean, without disobedience. I am innocent, neither is there iniquity in me.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Look, he finds occasions against me. He counts me for his enemy.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
He puts my feet in the stocks. He marks all my paths.'
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
"Look, I will answer you. In this you are not just, for God is greater than man.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
Why do you strive against him, because he doesn't give account of any of his matters?
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
For God speaks once, yes twice, though man pays no attention.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
In a dream, in a vision of the night, when deep sleep falls on men, in slumbering on the bed;
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Then he opens the ears of men, and seals their instruction,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
That he may withdraw man from his purpose, and hide pride from man.
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
He keeps back his soul from the pit, and his life from perishing by the sword.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
He is chastened also with pain on his bed, with continual strife in his bones;
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
So that his life abhors bread, and his soul choicest food.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
His flesh is so consumed away, that it can't be seen. His bones that were not seen stick out.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Yes, his soul draws near to the pit, and his life to the destroyers.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
"If there is beside him an angel, an interpreter, one among a thousand, to show to man what is right for him;
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
then he is gracious to him, and says, 'Deliver him from going down to the pit, I have found a ransom.'
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
His flesh shall be fresher than a child's. He returns to the days of his youth.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
He prays to God, and he is favorable to him, so that he sees his face with joy. He restores to man his righteousness.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
He sings before men, and says, 'I have sinned, and perverted that which was right, and it did not profit me.
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
He has redeemed my soul from going into the pit. My life shall see the light.'
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
"Look, God works all these things, twice, yes three times, with a man,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
to bring back his soul from the pit, that he may be enlightened with the light of the living.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Mark well, Job, and listen to me. Hold your peace, and I will speak.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
If you have anything to say, answer me. Speak, for I desire to justify you.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
If not, listen to me. Hold your peace, and I will teach you wisdom."

< Ayubu 33 >