< Ayubu 30 >

1 Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
但如今,比我年少的人戏笑我; 其人之父我曾藐视, 不肯安在看守我羊群的狗中。
2 Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
他们壮年的气力既已衰败, 其手之力与我何益呢?
3 Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
他们因穷乏饥饿,身体枯瘦, 在荒废凄凉的幽暗中啃干燥之地,
4 Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
在草丛之中采咸草, 罗腾的根为他们的食物。
5 Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
他们从人中被赶出; 人追喊他们如贼一般,
6 Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
以致他们住在荒谷之间, 在地洞和岩穴中;
7 Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
在草丛中叫唤, 在荆棘下聚集。
8 Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
这都是愚顽下贱人的儿女; 他们被鞭打,赶出境外。
9 Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
现在这些人以我为歌曲, 以我为笑谈。
10 Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
他们厌恶我,躲在旁边站着, 不住地吐唾沫在我脸上。
11 Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
松开他们的绳索苦待我, 在我面前脱去辔头。
12 Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
这等下流人在我右边起来, 推开我的脚,筑成战路来攻击我。
13 Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
这些无人帮助的, 毁坏我的道,加增我的灾。
14 Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
他们来如同闯进大破口, 在毁坏之间滚在我身上。
15 Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
惊恐临到我, 驱逐我的尊荣如风; 我的福禄如云过去。
16 Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
现在我心极其悲伤; 困苦的日子将我抓住。
17 Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
夜间,我里面的骨头刺我, 疼痛不止,好像啃我。
18 Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
因 神的大力,我的外衣污秽不堪, 又如里衣的领子将我缠住。
19 Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
神把我扔在淤泥中, 我就像尘土和炉灰一般。
20 Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
主啊,我呼求你,你不应允我; 我站起来,你就定睛看我。
21 Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
你向我变心,待我残忍, 又用大能追逼我,
22 Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
把我提在风中,使我驾风而行, 又使我消灭在烈风中。
23 Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
我知道要使我临到死地, 到那为众生所定的阴宅。
24 Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
然而,人仆倒岂不伸手? 遇灾难岂不求救呢?
25 Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
人遭难,我岂不为他哭泣呢? 人穷乏,我岂不为他忧愁呢?
26 Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
我仰望得好处,灾祸就到了; 我等待光明,黑暗便来了。
27 Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
我心里烦扰不安, 困苦的日子临到我身。
28 Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
我没有日光就哀哭行去 ; 我在会中站着求救。
29 Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
我与野狗为弟兄, 与鸵鸟为同伴。
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
我的皮肤黑而脱落; 我的骨头因热烧焦。
31 Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.
所以,我的琴音变为悲音; 我的箫声变为哭声。

< Ayubu 30 >