< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na kusema,
ヨブまた語をつぎて曰く
2 Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
嗚呼過にし年月のごとくならまほし 神の我を護りたまへる日のごとくならまほし
3 taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
かの時には彼の燈火わが首の上に輝やき彼の光明によりて我黑暗を歩めり
4 Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
わが壯なりし日のごとくならまほし 彼時には神の恩惠わが幕屋の上にありき
5 wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
かの時には全能者なほ我とともに在し わが子女われの周圍にありき
6 wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
乳ながれてわが足跡を洗ひ 我が傍なる磐油を灌ぎいだせり
7 Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
かの時には我いでて邑の門に上りゆき わが座を街衢に設けたり
8 vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
少き者は我を見て隱れ 老たる者は起あがりて立ち
9 Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
牧伯たる者も言談ずしてその口に手を當て
10 Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
貴き者も聲ををさめてその舌を上顎に貼たりき
11 Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
我事を耳に聞る者は我を幸福なりと呼び 我を目に見たる者はわがために證據をなしぬ
12 kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
是は我助力を求むる貧しき者を拯ひ 孤子および助くる人なき者を拯ひたればなり
13 Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
亡びんとせし者われを祝せり 我また寡婦の心をして喜び歌はしめたり
14 Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
われ正義を衣また正義の衣る所となれり 我が公義は袍のごとく冠冕のごとし
15 Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
われは盲目の目となり跛者の足となり
16 Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
貧き者の父となり知ざる者の訴訟の由を究め
17 Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
惡き者の牙を折り その齒の間より獲物を取いだせり
18 Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
我すなはち言けらく 我はわが巣に死ん 我が日は砂の如く多からん
19 Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
わが根は水の邊に蔓り 露わが枝に終夜おかん
20 Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
わが榮光はわが身に新なるべくわが弓はわが手に何時も強からんと
21 Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
人々われに聽き默して我が敎を俟ち
22 Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
わが言し後は彼等言を出さず 我説ところは彼等に甘露のごとく
23 Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
かれらは我を望み待つこと雨のごとく 口を開きて仰ぐこと春の雨のごとくなりき
24 Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
われ彼等にむかひて笑ふとも彼等は敢て眞實とおもはず我面の光を彼等は除くことをせざりき
25 Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.
われは彼等のために道を擇び その首として座を占め 軍中の王のごとくして居り また哀哭者を慰さむる人のごとくなりき

< Ayubu 29 >