< Ayubu 29 >

1 Ayubu akaendelea na kusema,
Moreover Job continued his parable, and said,
2 Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
Oh that I were as in months past, as in the days when God preserved me;
3 taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
When his candle shined upon my head, and when by his light I walked through darkness;
4 Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
As I was in the days of my youth, when the friendship and counsel of God was upon my tabernacle;
5 wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
When the Almighty was yet with me, when my children were about me;
6 wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
When I washed my steps with butter, and the rock poured me out rivers of oil;
7 Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
When I went out to the gate through the city, when I prepared my seat in the street!
8 vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
The young men saw me, and hid themselves: and the aged arose, and stood up.
9 Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
The princes refrained talking, and laid their hand on their mouth.
10 Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
The nobles held their peace, and their tongue cleaved to the roof of their mouth.
11 Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
When the ear heard me, then it blessed me; and when the eye saw me, it gave witness to me:
12 kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
Because I delivered the poor that cried, and the fatherless, and him that had none to help him.
13 Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
The blessing of him that was ready to perish came upon me: and I caused the widow’s heart to sing for joy.
14 Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
I put on righteousness, and it clothed me: my judgment was as a robe and a diadem.
15 Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
I was eyes to the blind, and feet was I to the lame.
16 Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
I was a father to the poor: and the cause which I knew not I searched out.
17 Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
And I brake the jaws of the wicked, and plucked the spoil out of his teeth.
18 Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
Then I said, I shall die in my nest, and I shall multiply my days as the sand.
19 Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
My root was spread out by the waters, and the dew lay all night upon my branch.
20 Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
My glory was fresh in me, and my bow was renewed in my hand.
21 Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
Unto me men gave ear, and waited, and kept silence at my counsel.
22 Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
After my words they spake not again; and my speech dropped upon them.
23 Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
And they waited for me as for the rain; and they opened their mouth wide as for the latter rain.
24 Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
If I laughed on them, they believed it not; and the light of my countenance they cast not down.
25 Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.
I chose out their way, and sat chief, and dwelt as a king among his troops, as one that comforteth the mourners.

< Ayubu 29 >