< Ayubu 20 >

1 Ndipo Sofari, Mnaamathi alijibu na kusema,
Then answered Zophar the Naamathite, and said,
2 “Mawazo yangu yananifanya mimi nijibu kwa haraka kwa sababu ya mashaka yaliyomo ndani yangu mimi.
Therefore do my thoughts cause me to answer, and for this I make haste.
3 Mimi ninasikia kukemewa ambako kunaniondolea heshima mimi, lakini roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.
I have heard the check of my reproach, and the spirit of my understanding causeth me to answer.
4 Je, unafahamu kwamba ukweli huu kutoka enzi za kale, wakati Mungu alipomweka mwanadamu juu ya nchi:
Knowest thou not this of old, since man was placed upon earth,
5 ushindi wa mtu mwovu ni mfupi, na furaha ya mtu asiyemcha Mungu hudumu kwa kitambo tu?
That the triumphing of the wicked is short, and the joy of the hypocrite but for a moment?
6 Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu, na kichwa chake yeye kufikia kwenye mawingu,
Though his excellency mount up to the heavens, and his head reach unto the clouds;
7 bado mtu huyo atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe; wale waliokuwa wamemuona yeye watasema, 'Yuko wapi yeye'?
Yet he shall perish for ever like his own dung: they which have seen him shall say, Where is he?
8 Yeye atapaa mbali kama ndoto na hataonekana; ndivyo ilivyo, yeye atakuwa amefukuzwa mbali kama ono la
He shall fly away as a dream, and shall not be found: yea, he shall be chased away as a vision of the night.
9 usiku. Jicho ambalo lilimuona yeye halitamuona yeye tena; mahali pake hapatamuona yeye tena.
The eye also which saw him shall see him no more; neither shall his place any more behold him.
10 Watoto wake wataomba msamaha kwa watu maskini, mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.
His children shall seek to please the poor, and his hands shall restore their goods.
11 Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani, lakini zitalala naye chini katika mavumbi.
His bones are full of the sin of his youth, which shall lie down with him in the dust.
12 Japokuwa uovu ni mtamu katika mdomo wake yeye, japokuwa yeye anauficha chini ya ulimi wake yeye,
Though wickedness be sweet in his mouth, though he hide it under his tongue;
13 japokuwa anaushikilia pale na hauruhusu kwenda lakini bado huushikilia katika mdomo wake yeye -
Though he spare it, and forsake it not; but keep it still within his mouth:
14 chakula katika koromeo lake yeye hugeuka kuwa uchungu; hugeuka kuwa sumu ya majoka ndani yake yeye.
Yet his meat in his bowels is turned, it is the gall of asps within him.
15 Yeye humeza chini utajiri, lakini yeye atautapika tena; Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake yeye.
He hath swallowed down riches, and he shall vomit them up again: El shall cast them out of his belly.
16 Yeye atamumunya sumu ya majoka; ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.
He shall suck the poison of asps: the viper's tongue shall slay him.
17 Yeye hatafurahia vijito vya maji, wingi wa asali na siagi.
He shall not see the rivers, the floods, the brooks of honey and butter.
18 Yeye atayarudisha matunda ya kazi yake na hataweza kuyala; yeye hatafurahia utajiri alioupata kwa biashara zake yeye.
That which he laboured for shall he restore, and shall not swallow it down: according to his substance shall the restitution be, and he shall not rejoice therein.
19 Kwa kuwa yeye amewakandamiza na kuwasahau watu maskini; yeye kwa uonevu, amezichukua mbali nyumba ambazo hakuzijenga yeye.
Because he hath oppressed and hath forsaken the poor; because he hath violently taken away an house which he builded not;
20 Kwa sababu yeye mwenyewe hakujua utoshelevu wowote, yeye hataweza kuokoa kitu chochote katika kile ambacho alijifurahisha.
Surely he shall not feel quietness in his belly, he shall not save of that which he desired.
21 Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza; kwa hiyo mafanikio yake yeye hayatakuwa ya kudumu.
There shall none of his meat be left; therefore shall no man look for his goods.
22 katika wingi wa utajiri wake yeye ataanguka katika mahangaiko; mkono wa kila mmoja ambaye yuko katika umaskini utakuja kinyume chake yeye.
In the fulness of his sufficiency he shall be in straits: every hand of the wicked shall come upon him.
23 Wakati akiwa katika kulijaza tumbo lake, Mungu atatupa hasira ya ghadhabu yake juu yake yeye; Mungu ataunyeshea chini juu yake yeye wakati yeye anakula.
When he is about to fill his belly, Elohim shall cast the fury of his wrath upon him, and shall rain it upon him while he is eating.
24 Ingawa mtu huyo atakimbia kutoka katika silaha ya chuma, upinde wa shaba utampiga yeye.
He shall flee from the iron weapon, and the bow of steel shall strike him through.
25 Mshale utatoboa kupitia mgongoni mwake na utatokezea; ni dhahiri, ncha inayong'ra itatokezea nje kupitia ini lake yeye; watesi huja tena juu yake.
It is drawn, and cometh out of the body; yea, the glittering sword cometh out of his gall: terrors are upon him.
26 Giza lliilo kamilika limetunzwa kwa akiba zake; moto usiopulizwa utamla yeye kwa haraka; utameza kile kilichoachwa katika hema yake.
All darkness shall be hid in his secret places: a fire not blown shall consume him; it shall go ill with him that is left in his tabernacle.
27 Mbingu zitauweka wazi uovu wake, na nchi itainuka juu dhidi yake yeye kama shahidi.
The heaven shall reveal his iniquity; and the earth shall rise up against him.
28 Utajiri wa nyumba yake utatoweka; bidhaa zake zitamwagika mbali siku ya ghadhabu ya Mungu.
The increase of his house shall depart, and his goods shall flow away in the day of his wrath.
29 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu, urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye.”
This is the portion of a wicked man from Elohim, and the heritage appointed unto him by El.

< Ayubu 20 >