< Ayubu 17 >

1 Roho yangu imemezwa, na siku zangu zimekwisha; kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.
“My spirit is consumed. My days are extinct and the grave is ready for me.
2 Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami; ni lazima daima jicho langu litazame kukasirisha kwao.
Surely there are mockers with me. My eye dwells on their provocation.
3 Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe; nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?
“Now give a pledge. Be collateral for me with yourself. Who is there who will strike hands with me?
4 Kwa kuwa wewe Mungu umemeitunza mioyo yao kutoka katika ufahamu; kwa hiyo, wewe hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.
For you have hidden their heart from understanding, therefore you will not exalt them.
5 Yeye ambaye huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
He who denounces his friends for plunder, even the eyes of his children will fail.
6 Lakini amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu; wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.
“But he has made me a byword of the people. They spit in my face.
7 Jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni; sehemu zangu zote za mwili ni nyembamba kama vivuli.
My eye also is dim by reason of sorrow. All my members are as a shadow.
8 Watu wanyoofu watapendezwa na hiki; mtu asiye na hatia atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi ya watu wasiomcha Mungu.
Upright men will be astonished at this. The innocent will stir himself up against the godless.
9 Mtu mwenye haki ataendelea katika njia yake; yeye ambaye ana mikono iliyo safi ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi.
Yet the righteous will hold to his way. He who has clean hands will grow stronger and stronger.
10 Lakini kama ilivyo kwenu ninyi nyote, njooni sasa; Mimi sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu ninyi.
But as for you all, come back. I will not find a wise man amongst you.
11 Siku zangu zimepita; mipango yangu imenyamazishwa na hivyo ni matumaini ya moyo wangu.
My days are past. My plans are broken off, as are the thoughts of my heart.
12 Watu hawa, wenye kukejeli, badili usiku kuwa mchana; mchana uko karibu kuwa giza.
They change the night into day, saying ‘The light is near’ in the presence of darkness.
13 Tangu mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu; tangu Mimi nimetandaza kiti changu katika giza; (Sheol h7585)
If I look for Sheol as my house, if I have spread my couch in the darkness, (Sheol h7585)
14 tangu Mimi nimesema na shimo 'Wewe ni baba yangu,' na kwa funza, 'Wewe ni mama yangu au dada yangu;
if I have said to corruption, ‘You are my father,’ and to the worm, ‘My mother,’ and ‘My sister,’
15 liko wapi tena tumaini langu? Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?
where then is my hope? As for my hope, who will see it?
16 Tumaini litakwenda pamoja na mimi katika milango ya Kuzimu wakati sisi tutakapokwenda katika mavumbi? (Sheol h7585)
Shall it go down with me to the gates of Sheol, or descend together into the dust?” (Sheol h7585)

< Ayubu 17 >