< Ayubu 14 >

1 Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke, huishi siku chache tu na amejaa mahangaiko.
“Man, who is born of a woman, is of few days, and full of trouble.
2 Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini; yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.
He grows up like a flower, and is cut down. He also flees like a shadow, and does not continue.
3 Je, wewe unatazama chochote katika hivi? Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?
Do you open your eyes on such a one, and bring me into judgment with you?
4 Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.
Who can bring a clean thing out of an unclean? Not one.
5 Siku za mwanadamu zimeamriwa. Idadi ya miezi yake unayo wewe; umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka.
Seeing his days are determined, the number of his months is with you, and you have appointed his bounds that he cannot pass.
6 Tazama mbali kutoka kwake kwamba yeye aweze kupumzika, ili kwamba aweze kufurahia siku yake kama mtu aliyekodishwa kama yeye anaweza kufanya hivyo.
Look away from him, that he may rest, until he accomplishes, as a hireling, his day.
7 Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti; kama ukikatwa chini, unaweza kuchipua tena, hivyo chipukizi lake halitapotea.
“For there is hope for a tree if it is cut down, that it will sprout again, that the tender branch of it will not cease.
8 Japokuwa mizizi yake inakua na kuzeeka katika ardhi, na shina lake kufa katika udongo,
Though its root grows old in the earth, and its stock dies in the ground,
9 hata kama bado lina harufu ya maji pekee, litachipua tena na kutoa nje matawi kama mche.
yet through the scent of water it will bud, and sprout boughs like a plant.
10 Lakini mwanadamu hufa; yeye huwa dhaifu; haswaa, mwanadamu hukoma kupumua, na tena yuko wapi yeye?
But man dies, and is laid low. Yes, man gives up the spirit, and where is he?
11 Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,
As the waters fail from the sea, and the river wastes and dries up,
12 vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena. Mpaka pale mbingu zitakapokuwa hazipo tena, hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.
so man lies down and does not rise. Until the heavens are no more, they will not awake, nor be roused out of their sleep.
13 Laiti, kwamba ungenificha mimi mbali katika kuzimu mbali kutoka katika mahangaiko, na kwamba ungenitunza mimi katika siri hadi hasira yake imalizike, kwamba ungeniwekea mimi muda maalumu wa kukaa huko na kisha kuniita mimi katika fahamu! (Sheol h7585)
"Oh that you would hide me in Sheol (Sheol h7585), that you would keep me secret until your wrath is past, that you would appoint me a set time and remember me!
14 Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena? Ikiwa hivyo, ningependa kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja.
If a man dies, will he live again? I would wait all the days of my warfare, until my release should come.
15 Wewe ungeita, na mimi ningekujibu wewe. Wewe ungekuwa na shauku ya kazi ya mikono yako.
You would call, and I would answer you. You would have a desire for the work of your hands.
16 Wewe ungehesabu na kutunza nyayo zangu; Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu.
But now you count my steps. Do not you watch over my sin?
17 Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba; wewe ungeufunga uovu wangu.
My disobedience is sealed up in a bag. You fasten up my iniquity.
18 Lakini hata milima huanguka na kuwa si chochote; hata miamba huhamishwa kutoka mahali pake;
“But the mountain falling comes to nothing. The rock is removed out of its place.
19 maji yaliyokuwa chini ya mawe; kufurika kwake huondoa mbali mavumbi ya nchi. Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.
The waters wear the stones. The torrents of it wash away the dust of the earth. So you destroy the hope of man.
20 Ninyi daima humshinda yeye, na yeye hupita mbali; Ninyi mnabadilisha uso wake na kumtuma yeye mbali kufa.
You forever prevail against him, and he departs. You change his face, and send him away.
21 Kama watoto wake wa kiume ni wa kuheshimiwa, yeye, hatambui hicho; na kama wakishushwa chini, yeye haoni hicho.
His sons come to honor, and he does not know it. They are brought low, but he does not perceive it of them.
22 Yeye hujisikia tu maumivu ya mwili wake mwenyewe, na hujiombolezea yeye mwenyewe.
But his flesh on him has pain, and his soul within him mourns.”

< Ayubu 14 >