< Yeremia 23 >

1 “Ole wao wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu-hii ndiyo ahadi ya Bwana.”
Alas for the shepherds who are destroying and scattering the sheep of my pasture Declareth Yahweh.
2 Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi juu ya wachungaji ambao wanawachunga watu wake, “Ninyi mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza. Hamuwajali hata kidogo. Tambueni hili! Mimi nitawalipiza uovu wa matendo yenu-hili ni tamko la Bwana.
Therefore, Thus, saith Yahweh God of Israel, Concerning the shepherds who are tending my people, —Ye have scattered my flock and have driven them away, and have not visited them, —Behold me! visiting upon you the wickedness of your doings Declareth Yahweh.
3 Mimi mwenyewe nitakusanya mabaki ya kondoo wangu kutoka nchi zote nilizowafukuza, nami nitawarejesha kwenye eneo la malisho, ambako watazaa na kuongezeka.
I myself, therefore will gather the remnant of my flock, out of all the lands whither I have driven them, —And will bring them back unto their own fold, And they shall be fruitful and multiply;
4 Ndipo nitawainua wachungaji juu yao ambao watawachunga hivyo hawataogopa tena au kupotezwa. Hakuna hata mmoja atakayepotea-hili ni tamko la Bwana.
And I will raise up over them shepherds who will tend them, —So shall they not be afraid any more, nor be dismayed nor be missing, Declareth Yahweh.
5 Angalia, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-nitakapomuinulia Daudi tawi la haki. Atatawala kama mfalme; atatenda kwa busara na kusababisha hukumu na haki katika nchi.
Lo! days are coming, Declareth Yahweh, when I will raise up to David A righteous Bud, And he shall reign as king, and prosper, And shall execute justice and righteousness in the land.
6 Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama. Na jina lake atakayeitwa Bwana ni haki yetu.
In his days, Shall Judah be saved, And Israel abide securely, —And, this, is his name whereby he shall be called Yahweh, our Righteousness.
7 Kwa hiyo, tazama, siku zinakuja-hili ndilo tamko la Bwana-hawatasema tena, 'Kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya Misri.'
Therefore, lo! days are coming, Declareth Yahweh, When it shall not be said any more As Yahweh liveth, who brought up the sons of Israel out of the land of Egypt;
8 Badala yake watasema, 'Kama Bwana aishivyo, ambaye aliwaleta na ambaye aliwaongoza wana wa nyumba ya Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa.' Nao watakaa katika nchi yao wenyewe.”
but—As Yahweh liveth who hath brought up and who hath brought in the seed of the house of Israel out of the land of the North, and out of all the lands whither I have driven them, —And they shall remain upon their own soil.
9 Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka. Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
As for the prophets, —Broken is my heart within me Trembled have all my bones, I have become as a drunken man, And as a strong man whom wine hath overcome, —Because of Yahweh, And because of his holy words.
10 Kwa maana nchi imejaa wazinzi. Kwa sababu ya hayo nchi imeuka. Milima katika jangwa imekauka. Njia hizi za manabii ni mbaya; nguvu zao hazitumiwi kwa namna sahihi.
For with adulterers, is the land filled, Yea because of cursing, doth the land mourn, Dried up are the oases of the desert, —And, their oppression hath become wicked, And, their might is not right.
11 Kwa maana manabii na makuhani wote wamekufuru. Nimeona uovu wao ndani ya nyumba yangu! - hili ndilo tamko la Bwana;
For both prophet and priest, are profane, —Even in my house, have I found their wickedness, Declareth Yahweh.
12 kwa hiyo njia yao itakuwa kama mahali pa kupumzika katika giza. Watasukumwa chini. Wao wataanguka ndani yake. Kwa maana nitawatuma mabaya juu yao katika mwaka wa adhabu yao; hili ndilo tamko la Bwana.
Therefore, shall their way become to them like slippery places in darkness, They shall be driven on and shall fall therein, —For I will bring in upon them calamity—The year of their visitation, Declareth Yahweh.
13 kwa maana nimeona uchungu kati ya manabii huko Samaria. Walitabiri kwa Baali na wakawaongoza watu wangu Israeli kwenye njia sahihi.
Even among the prophets of Samaria, had I seen a foolish thing, —They prophesied by Baal, And led astray my people Israel.
14 Na miongoni mwa manabii huko Yerusalemu nimeona mambo ya kutisha: wanafanya uzinzi na huenda kwa udanganyifu. Wanaimarisha mikono ya waovu; hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake. Wote wamekuwa kama Sodoma kwangu na wenyeji wake kama Gomora!”
But among the prophets of Jerusalem, have I seen a horrible thing, —Committing adultery, And walking in falsehood, And so strengthening the hands of doers of wickedness, not to return any man from his wickedness: They have all of them become to me as Sodom, And her inhabitants as Gomorrah.
15 Kwa hiyo, Bwana wa majeshi asema hivi juu ya manabii, “Tazameni, nitawafanya wale magugu na kunywa maji yenye sumu, kwa maana kufuru imetoka kwa manabii wa Yerusalemu na kuingia katika nchi yote.”
Therefore, Thus, saith Yahweh of hosts Concerning the prophets, —Behold me! Feeding them with wormwood, And I will cause them to drink poisoned water, —For from the prophets of Jerusalem, hath there gone forth profanity unto all the land.
16 Bwana wa majeshi asema hivi, “Usisikilize maneno ya manabii wanaokuhubiri. Wamekudanganya! Wanatangaza maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe, si kwa kinywa cha Bwana.
Thus, saith Yahweh of hosts, —Do not hearken unto the words of the prophets who are prophesying unto you, They are filling you, with vain hopes, —The vision of their own hearts, do they speak, Not from the mouth of Yahweh!
17 Wanasema daima kwa wale wanaonidharau mimi, 'Bwana asema kutakuwa na amani kwako.' Na kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake anasema, 'mabaya hayatakuja kwenu.'
They keep on saying to them who despise me, Yahweh, hath spoken, saying, Prosperity, shall ye have! And to every one who is going on in the stubbornness of his own heart, have they said, There shall come on you, no calamity
18 Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?
For who hath stood in the council of Yahweh, that he should see and hear his word? Who hath given ear to his word and heard it?
19 Tazama, kuna dhoruba inayotoka kwa Bwana! Hasira yake inatoka, na dhoruba inazunguka. Inazunguka vichwa vya waovu.
Lo! the tempest of Yahweh! Indignation, hath come forth, Even a tempest whirling along: On the head of the lawless, shall it hurl itself down.
20 Hasira za Bwana hazitarejea mpaka zitakapotimiza nia ya moyo wake. Katika siku za mwisho, utaelewa.
The anger of Yahweh, wilt not return, Until he hath executed nor Until he hath established The purposes of his heart, —In the afterpart of the days, shall ye understand it perfectly.
21 Sikuwatuma manabii hawa. Wao tu walionekana. Sikuwahubiri jambo lolote kwao, lakini bado wanatabiri.
I sent not the prophets yet they, ran, I spake not unto them yet, they, prophesied.
22 Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza, wangeweza kuwasababisha watu wangu kusikia neno langu; wangewafanya wapate kuacha maneno yao mabaya na mazoea mabaya.
But if they had stood in my council, Then might they have announced my words unto my people, And have turned them from their wicked way and from the wickedness of their doings.
23 Mimi ni Mungu aliye karibu-hili ni tamko la Bwana-mimi sio Mungu aliye mbali?
Am I, a God at hand, Demandeth Yahweh, And not a God afar off?
24 Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona? -Hili ndilo tamko la Bwana-Je mbingu na nchi hazikujawa nami? -hili Ndilo tamko la Bwana.
Can any hide himself in secret places that I, shall not see him? Demandeth Yahweh, —The heavens and the earth, do I not fill? Demandeth Yahweh.
25 Nimesikia yale waliyosema manabii, wale waliokuwa wanatabiri uongo kwa jina langu. Wakisema, 'Nilikuwa na ndoto!
I have heard what the prophets have said, who prophesy in my name falsely, saying, —I have dreamed! I have dreamed!
26 Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?
How long shall it be in the heart of the prophets, To be prophets of falsehood, —And prophets of the deceit of their own heart?
27 Wana mpango wa kuwafanya watu wangu kusahau jina langu kwa ndoto ambazo wanazoripoti, kila mmoja kwa jirani yake, kama vile babu zao walivyosahau jina langu kwa ajili ya jina la Baali.
Who lay a plot to cause my people to forget my name by their dreams which they relate every man to his neighbour, —Just as their fathers forgat, my name, for Baal.
28 Nabii aliye na ndoto, aseme ndoto hiyo. Lakini yule ambaye nimemwambia kitu fulani, basi aseme neno langu kwa kweli. Je, majani yanahusiana na nafaka? - hili ni tamko la Bwana-
The prophet with whom is a dream, Let him relate it as a dream, And he with whom is my word, Let him speak my word as truth, —What is the chaff to the wheat? Demandeth Yahweh:
29 Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?
Is not my word, like this, Like fire? Demandeth Yahweh, —And like a hammer, that breaketh in pieces a cliff?
30 Tazameni, ninapingana na nabii-hii ndiyo ahadi ya Bwana-yeyote anayeiba maneno kutoka kwa mtu mwingine na anasema yanatoka kwangu.
Therefore! behold me! against the prophets, Declareth Yahweh, —who steal my words, every man from his neighbour:
31 Tazama, ninapingana na manabii-hili ndilo tamko la Bwana-ambao hutumia lugha zao kutabiri maneno.
Behold me! against the prophets, Declareth Yahweh, who presume with their tongue and declare He declareth:
32 Tazameni, ninapingana na manabii wanaoota ndoto-hii ndiyo ahadi ya Bwana-na kisha kuwahubiri na kwa njia hii kuwadanganya watu wangu kwa udanganyifu wao na kujivunia. Mimi ni juu yao, kwa kuwa sikuwatuma wala kuwapa amri. Kwa hivyo hawatawasaidia watu hawa - hili ndilo tamko la Bwana.
Behold me! against such as prophesy the dreams of falsehood, Declareth Yahweh, who have related them and led astray my people, with their falsehoods and with their recklessness, —whereas, I, had not sent them nor commanded them, so that they could be of no, profit, to this people, Declareth Yahweh.
33 Watu hawa au nabii au kuhani wakakuuliza, 'Je, ni nini tamko la Bwana?' basi lazima uwaambie, 'Ni tamko gani? Kwa maana nimekuacha wewe-hili ndilo tamko la Bwana.
But when this people or a prophet or a priest shall ask thee saying What is the oracle of Yahweh? Then shalt thou say unto them Ye, yourselves, are the oracle, Therefore will I reject you Declareth Yahweh;
34 Kwa habari ya manabii, makuhani, na watu wanaosema, 'Hili ndilo tamko la Bwana,' nitamuadhibu mtu huyo na nyumba yake.
But the prophet, or the priest or the people who shall say—the oracle of Yahweh, I will bring punishment upon that man and upon his house.
35 Endelea kusema, kila mtu kwa jirani yake na kila mtu kwa ndugu yake, 'Bwana alijibu nini?' na 'Bwana alitangaza nini?'
Thus, shall ye say—every man unto his neighbour and every man unto his brother, —What hath Yahweh, answered? or, What hath Yahweh, spoken?
36 Lakini usizungumze tena juu ya tamko la Bwana, kwa kuwa kila tamko kutoka kwa kila mtu limekuwa ujumbe wake mwenyewe, na umepotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana wa majeshi, Mungu wetu.
but the oracle of Yahweh, shall ye not mention, any more, —for, every man’s oracle, shall be his own word, because ye have perverted the words of a Living God, Yahweh of hosts our God.
37 Utamuuliza nabii hivi, 'Bwana alikujibu nini? Je, Bwana alisema nini? Kisha unasema tamko kutoka kwa Bwana;
Thus, shalt thou say unto the prophet, —What hath Yahweh, answered thee? or What hath Yahweh, spoken?
38 lakini Bwana asema hivi, Sema hivi, “Hili ni tamko la Bwana” ingawa nimekuagiza na kusema, “Usiseme: Hili ni tamko kutoka kwa Bwana.”
But, since ye keep on saying, The Oracle of Yahweh, therefore, Thus saith Yahweh, Because ye have said this word, The oracle of Yahweh, whereas I had sent unto you saying, Ye shall not say, The oracle of Yahweh
39 Kwa hiyo, angalia, nitawachukua na kukutupa mbali na mimi, pamoja na jiji ambalo nilikupa wewe na baba zako.
therefore, behold me! I will lift you up, —and carry you away, and the city which I gave to you and to your fathers from before my face;
40 Ndipo nitaweka aibu ya milele na fedheha juu yenu ambayo haitasahauliwa.'”
and will give unto you reproach age-abiding, —and disgrace age-abiding, which shall not be forgotten.

< Yeremia 23 >