< Isaya 3 >

1 Ona, Bwana, Yahwe wa majeshi, anakaribia kuwachukua kutoka Yerusalema na Yudawasaidizi na wafanyakazi: wasambazaji wote wa mikate, wasambazaji wote wa maji;
For, behold, the Lord, the LORD of hosts, doth take away from Jerusalem and from Judah stay and staff, every stay of bread, and every stay of water;
2 mtu mwenye nguvu, shuja, hakimu, nabii, dalili za msomaji, na mzee;
The mighty man, and the man of war; the judge, and the prophet, and the diviner, and the elder;
3 naodha wa hamsini, raia husika, mshauri, fundi mtarajiwa, na mchawi stadi.
The captain of fifty, and the man of rank, and the counsellor, and the cunning charmer, and the skilful enchanter.
4 Nitamuweka kijana tu kama kiongozi wenu, kijana atawaongoza wao.
And I will give children to be their princes, and babes shall rule over them.
5 Watu watanyanyasika, kila mmoja mmoja na kila mmoja na jirani yake; watoto watawatusi wazee, na mivutano itawapa changamoto waheshimiwa.
And the people shall oppress one another, every man his fellow, and every man his neighbour; the child shall behave insolently against the aged, and the base against the honourable,
6 Mwanaume atamshikilia ndugu yake katika nyumba ya baba yake na kusema, 'Unayo kanzu; uwe kiongozi wetu, na uharibifu huu uwe mikononi mwako.
For a man shall take hold of his brother of the house of his father: 'Thou hast a mantle, be thou our ruler, and let this ruin be under thy hand.'
7 'Siku hiyo atapaza sauti na kusema, 'hautakuwa mganga; sina mkate wala mavazi. Hatanifanya kuwa kiongozi wa watu.
In that day shall he swear, saying: 'I will not be a healer; for in my house is neither bread nor a mantle; ye shall not make me ruler of a people.'
8 Kwa maana Yerusalemu kuna mashaka, na Yuda imeanguka, kwa sababu mazungumzo yao na matendo yao yako kinyume na Yahwe, wanayapinga macho ya utukufu wake.
For Jerusalem is ruined, and Judah is fallen; because their tongue and their doings are against the LORD, to provoke the eyes of His glory.
9 Angalia nyuso zao zinashudia kinyume nao; na watasema dhambi zao kama Sodoma; hawatazificha, Ole wao! Maana wanakamilisha janga lao wenyewe.
The show of their countenance doth witness against them; and they declare their sin as Sodom, they hide it not. Woe unto their soul! for they have wrought evil unto themselves.
10 Mwambie mtu mwenye haki kwamba itakuwa vizuri, maana watakula matunda ya matendo yao.
Say ye of the righteous, that it shall be well with him; for they shall eat the fruit of their doings.
11 Ole kwa wakosaji! itakuwa vibaya kwa yeye, maana malipo ya mikono yake yatafanyika kwake pia.
Woe unto the wicked! it shall be ill with him; for the work of his hands shall be done to him.
12 Watu wangu-watoto wangu wanawakandamiza, na wanawake wanawaongoza wao. Watu wangu, wale wanaowaongoza wanawaongoza vibaya na kuchanganya muelekeo wa nja yenu.
As for My people, a babe is their master, and women rule over them. O My people, they that lead thee cause thee to err, and destroy the way of thy paths.
13 Yahwe simama juu ya mashitaka; yeye amesimama kuwashaki watu.
The LORD standeth up to plead, and standeth to judge the peoples.
14 Yahwe atakuja na hukumu juu ya wazee na watu wao na viongozi wao: ''Umeharibu shamba; nyara kutoka kwa masikni ziko kwenye nyumba zako.
The LORD will enter into judgment with the elders of His people, and the princes thereof: 'It is ye that have eaten up the vineyard; the spoil of the poor is in your houses;
15 Kwa nini unaponda watu wangu na kusaga nyuso za masikini?'' Hili ni tamko Bwana, Yahwe wa majeshi.
What mean ye that ye crush My people, and grind the face of the poor?' saith the Lord, the GOD of hosts.
16 Yahwe anasema hivyo kwa sababu mabinti wa Sayuni wanajigamba, wanatembea pekee yao vichwa vyao vikiwa juu, na kutaniana kwa macho yao, na kutakata kokote waendako na kuamua upatu kwa miguu yao,
Moreover the LORD said: Because the daughters of Zion are haughty, and walk with stretched-forth necks and wanton eyes, walking and mincing as they go, and making a tinkling with their feet;
17 Kwa hiyo Bwana atafanya magonjwa ya mapele kwenye kishwa cha mabinti wa Sayuni, na Yahwe atawafanya upaa.
Therefore the Lord will smite with a scab the crown of the head of the daughters of Zion, and the LORD will lay bare their secret parts.
18 Siku hiyo Bwana ataondoa mapambo mazuri yaliyoko kwenye kifundo cha miguu, bendi za kichwa chao, kaya zao; bangili za masikio,
In that day the Lord will take away the bravery of their anklets, and the fillets, and the crescents;
19 bangili za miguu na taji zao;
the pendants, and the bracelets, and the veils;
20 kitambaa cha kichwa, chaini za miguu, mafurungu na maboksi ya marashi na na haiba ya bahati.
the headtires, and the armlets, and the sashes, and the corselets, and the amulets;
21 Atatoa bangili na kipini kwenye pua;
the rings, and the nose-jewels;
22 sherehe za mavazi, mapazia na mabegi ya mkononi;
the aprons, and the mantelets, and the cloaks, and the girdles;
23 vioo vya mkononi, sanda nzuri, vilemba vya kichwa na taji.
and the gauze robes, and the fine linen, and the turbans, and the mantles.
24 Badala ya manukato mazuri kutakuwa na arufu mbaya; na badala ya ukunda, kamba, kufunika kwa vazi la gunia; kitia alama mwilini kwa moto badala ya uzuri. wanaume wao wataanguka kwa upanga,
And it shall come to pass, that instead of sweet spices there shall be rottenness; and instead of a girdle rags; and instead of curled hair baldness; and instead of a stomacher a girding of sackcloth; branding instead of beauty.
25 na wanaume wenye nguvu wataanguka kwenye vita.
Thy men shall fall by the sword, and thy mighty in the war.
26 Lango la Yerusalemu litaomboleza na kuomboleza; na atakuwa peke yake amekaa chini ya ardhi.
And her gates shall lament and mourn; and utterly bereft she shall sit upon the ground.

< Isaya 3 >