< Hosea 4 >

1 Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
Heare the worde of the Lord, ye children of Israel: for the Lord hath a controuersie with the inhabitants of the lande, because there is no trueth nor mercie nor knowledge of God in the lande.
2 Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
By swearing, and lying, and killing, and stealing, and whoring they breake out, and blood toucheth blood.
3 Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
Therefore shall the land mourne, and euery one that dwelleth therein, shall be cut off, with the beasts of the fielde, and with the foules of the heauen, and also the fishes of the sea shall be taken away.
4 Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
Yet let none rebuke, nor reproue another: for thy people are as they that rebuke the Priest.
5 Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
Therefore shalt thou fall in the day, and the Prophet shall fall with thee in the night, and I will destroy thy mother.
6 Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
My people are destroyed for lacke of knowledge: because thou hast refused knowledge, I will also refuse thee, that thou shalt be no Priest to me: and seeing thou hast forgotten the Lawe of thy God, I will also forget thy children.
7 Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
As they were increased, so they sinned against me: therefore will I chaunge their glorie into shame.
8 Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
They eate vp the sinnes of my people, and lift vp their mindes in their iniquitie.
9 Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
And there shalbe like people, like Priest: for I wil visite their wayes vpon them, and reward them their deedes.
10 Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
For they shall eate, and not haue ynough: they shall commit adulterie, and shall not increase, because they haue left off to take heede to ye Lord.
11 Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
Whoredome, and wine, and newe wine take away their heart.
12 Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
My people aske counsell at their stockes, and their staffe teacheth them: for the spirite of fornications hath caused them to erre, and they haue gone a whoring from vnder their God.
13 Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
They sacrifice vpon the toppes of ye mountaines, and burne incense vpon the hilles vnder the okes, and the poplar tree, and the elme, because the shadow thereof is good: therefore your daughters shall be harlots, and your spouses shall be whores.
14 Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
I will not visite your daughters when they are harlots: nor your spouses when they are whores: for they themselues are separated with harlots, and sacrifice with whores: therefore the people that doeth not vnderstand, shall fall.
15 Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
Though thou, Israel, play the harlot, yet let not Iudah sinne: come not ye vnto Gilgal, neither goe ye vp to Beth-auen, nor sweare, The Lord liueth.
16 Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
For Israel is rebellious as an vnruly heyfer. Nowe the Lord will feede them as a lambe in a large place.
17 Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
Ephraim is ioyned to idoles: let him alone.
18 Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
Their drunkennes stinketh: they haue committed whoredome: their rulers loue to say with shame, Bring ye.
19 Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.
The winde hath bounde them vp in her wings, and they shalbe ashamed of their sacrifices.

< Hosea 4 >