< Mwanzo 42 >

1 Basi Yakobo akafahamu kwamba kuna nafaka huko Misri. Akawambia wanawe, “Kwa nini mnatazamana?
Forsothe Jacob herde that foodis weren seeld in Egipt, and he seide to hise sones, Whi ben ye necgligent?
2 Akasema, “Tazama, nimesikia kwamba kuna nafaka huko Misri. Shukeni huko mkatununulie chakula ili tuishi wala tusife.”
Y herde that wheete is seeld in Egipt, go ye doun, and bie ye necessaries to vs, that we moun lyue, and be not wastid bi nedynesse.
3 Ndugu kumi wa Yusufu wakashuka Misri kununua chakula.
Therfor ten britheren of Joseph yeden doun to bie wheete in Egipt,
4 Lakini Benjamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumtuma na ndugu zake, kwani alihofu kwamba madhara yaweza kumpata.
and Beniamyn was withholdun of Jacob at hoome, that seide to hise britheren, Lest perauenture in the weie he suffre ony yuel.
5 Wana wa Israeli wakaja kununua miongoni mwao waliokuja, kwani njaa ilikuwapo katika nchi ya Kanaani.
Sotheli thei entriden in to the lond of Egipt, with othere men that yeden to bie; forsothe hungur was in the lond of Canaan.
6 Basi Yusufu alikuwa mtawala juu ya nchi. Ndiye aliyekuwa akiwauzia watu wote wa nchi. Ndugu zake Yusufu wakaja na kumwinamia na nyuso zao hata chini.
And Joseph was prince of Egipt, and at his wille whetis weren seeld to puplis. And whanne hise britheren hadden worschipid hym,
7 Yusufu akawaona ndugu zake na kuwatambua, lakini alijibadili kwao na kuongea nao kwa ukali. Akawambia, “Mmetoka wapi?” Wakasema, “Kutoka nchi ya Kanaani ili kununua chakula.”
and he hadde knowe hem, he spak hardere as to aliens, and axide hem, Fro whennus camen ye? Whiche answeriden, Fro the lond of Canaan, that we bie necessaries to lyiflode.
8 Yusufu akawatambua ndugu zake, lakini wao hawakumtambua.
And netheles he knewe the britheren, and he was not knowun of hem,
9 Yusufu akazikumbuka ndoto aliyoziota kuhusu wao. Akawambia, “Ninyi ni wapelelezi. Mmekuja kuona sehemu za nchi zisizolindwa.”
and he bithouyte on the dremys whiche he seiy sumtyme. And he seide to hem, Ye ben aspieris, ye camen to se the feblere thingis of the lond.
10 Wakamwambia, “Hapana, bwana wangu. Watumishi wako wamekuja kununua chakula.
Whiche seiden, Lord, it is not so, but thi seruauntis camen to bie metis;
11 Sisi sote ni wana wa baba mmoja. Ni watu wa kweli. Watumishi wako siyo wapelelezi.”
alle we ben the sones of o man, we comen pesible, and thi seruauntis ymaginen not ony yuel.
12 Akawambia, “Hapana, mmekuja kuangalia sehemu za nchi zisizolindwa.”
To `whiche he answeride, It is in other maner, ye camen to se the feble thingis of the lond.
13 Wakasema, “Sisi watumishi wako tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba mmoja katika nchi ya Kanaani. Tazama, mdogo yupo na baba yetu, na mwingine hayupo hai tena.”
And thei seiden, `We twelue britheren, thi seruauntis, ben sones of o man in the lond of Canaan; the leeste is with oure fadir, an other is not `on erthe.
14 Yusufu akawambia, “Ndivyo nilivyowambia; ninyi ni wapelelezi.
This it is, he seide, that Y spak to you,
15 Mtajaribiwa kwa njia hii. Kama aishivyo Farao, hamtaondoka hapa, mdogo wenu asipokuja hapa.
ye ben aspieris, riyt now Y schal take experience of you, bi the helthe of Farao ye schulen not go fro hennus, til youre leeste brother come; sende ye oon of you,
16 Mtumeni mmoja wenu amlete mdogo wenu. Mtabaki gerezani, hata maneno yenu yatakapothibitishwa, kwamba kuna ukweli ndani yenu.”
that he brynge hym, forsothe ye schulen be in boondis, til tho thingis that ye seiden ben preued, whether tho ben false ether trewe; ellis, bi the helthe of Farao, ye ben aspieris.
17 Akawaweka kifungoni kwa siku tatu.
Therfor he bitook hem to kepyng thre daies; sotheli in the thridde dai,
18 Katika siku ya tatu Yusufu akaongea nao, “Fanyeni hivi nanyi mtaishi, kwani ninamcha Mungu.
whanne thei weren led out of prisoun, he seide, Do ye that that Y seide, and ye schulen lyue, for Y drede God;
19 Kama ninyi ni watu wa kweli, mmoja wenu atazuiliwa hapa gerezani, lakini ninyi nendeni, chukueni nafaka kwa ajili ya nyumba zenu.
if ye ben pesible, o brother of you be boundun in prisoun; forsothe go ye, and bere wheetis, whiche ye bouyten,
20 Mleteni mdogo wenu kwangu ili kwamba maneno yenu yathibitishwe nanyi hamtakufa.” Wakafanya hivyo.
in to youre housis, and brynge ye youre leeste brother to me, that Y may preue youre wordis, and ye die not. Thei diden as he seide,
21 Wakasemezana wao kwa wao, “Kwa kweli tuna hatia juu ya ndugu yetu kwani tuliona tabu ya nafsi yake alipotusihi nasi hatukusikia. Kwa hiyo taabu hii imeturudia.”
and thei spaken togidere, Skilfuli we suffren these thingis, for we synneden ayens oure brother, and we seiyen the anguysch of his soule, while he preiede vs, and we herden not; herfore this tribulacioun cometh on vs.
22 Rubeni akawajibu, “Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana,' lakini hamkusikia? Basi, tazama, damu yake inatakiwa juu yetu.”
Of which oon, Ruben, seide, Whether Y seide not to yow, Nyle ye do synne ayens the child, and ye herden not me? lo! his blood is souyt.
23 Lakini hawakuja kwamba Yusufu anawaelewa, kwani kulikuwa na mkalimani kati yao.
Sotheli thei wisten not that Joseph vndirstood, for he spak to hem by interpretour.
24 Akatoka kwao na kulia. Akarudi kwao na kuongea nao. Akamchukua Simoni miongoni mwao na kumfunga mbele ya macho yao.
And he turnede awei hym silf a litil and wepte; and he turnede ayen, and spak to hem.
25 Kisha Yusufu akaagiza watumishi kujaza mifuko yao kwa nafaka, na kurudisha pesa ya kila mmoja katika gunia lake, nakuwapa mahitaji kwa safari. Wakatendewa hivyo.
And he took Symeon, and boond hym, while thei weren present; and he comaundide the mynystris, that thei schulden fille her sackis with wheete, and that thei schulden putte the money `of alle in her baggis, and ouer this yyue metis in the weie; whiche diden so.
26 Hawa ndugu wakapandisha chakula chao juu ya punda zao na kuondoka pale.
And thei `baren wetis on her assis, and yeden forth,
27 Mmoja wao alipofungua gunia lake ili kumlisha punda wao katika sehemu waliyokuwa, akaona pesa yake. Tazama, ilikuwa mdomoni mwa gunia lake.
and whanne the sak of oon was opened that he schulde yyue meete to the werk beeste in the yn, he bihelde the money in the mouth of the bagge,
28 Akawambia ndugu zake, “Pesa yangu imerudishwa. Tazama, imo katika gunia langu.”Mioyo yao ikazimia na wakageukiana kila mmoja huku wakitetemeka. Wakasema, “Ni nini hiki alichotutendea Mungu?”
and seide to his britheren, My monei is yoldun to me, lo! it is had in the bagge; and thei weren astonyed, and troblid, and seiden togidere, What thing is this that God hath doon to us.
29 Wakaenda kwa Yakobo, baba yao katika nchi ya Kanaani na kumwambia yote yaliyowapata.
And thei camen to Jacob, her fadir, in the loond of Canaan, and telden to hym alle thingis that bifelden to hem, and seiden,
30 Wakasema, “Yule mtu, bwana wa nchi, aliongea nasi kwa ukali na kutudhania kuwa wapelelezi katika nchi.
The lord of the lond spak harde to vs, and gesside that we weren aspieris of the prouynce;
31 Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi.
to whom we answeriden, We ben pesible, nether we purposen ony tresouns;
32 Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena, na mdogo yupo na baba yetu katika nchi ya Kanaani.”
we ben twelue britheren, gendrid of o fadir, oon is not `on erthe, the leeste dwellith with the fadir in the lond of Canaan.
33 Yule mtu, bwana wa nchi, akatwambia, 'Kwa hili nitajua kwamba ni watu wa kweli ninyi. Mwacheni mmojawapo wa ndugu zenu, chukueni chakula kwa ajili ya njaa katika nyumba zenu, na mwondoke.
And he seide to vs, Thus Y schal preue that ye ben pesible; leeffe ye o brother of you with me, and take ye metis nedeful to youre housis, and go ye, and brynge ye to me youre leeste brother,
34 Mleteni mdogo wenu kwangu. Ndipo nitakapojua kwamba ninyi si wapelelezi, lakini ni watu wa kweli. Kisha nitamwachilia ndugu yenu, na mtafanya biashara katika nchi.”
that Y wite that ye ben not aspieris, and that ye moun resseyue this brother which is holdun in boondis, and that fro thennus forth ye haue licence to bie what thingis ye wolen.
35 Ikawa walipoyafungua magunia yao, na tazama, kila mfuko wa fedha wa mmojawao ulikuwa katika gunia lake. Wakati wao na baba yao walipoona mifuko yao ya fedha, wakaogopa.
While these thingis weren seide, whanne alle schedden out wheetis, thei founden money boundun in `the mouth of sackis. And whanne alle togidere weren aferd,
36 Yakobo baba yao akawambia, “Mmeniharibia watoto wao. Yusufu hayupo hai tena, Simoni ameondoka, nanyi mmpeleke Benjamini naye. Mambo haya yote ni kunyume changu.”
the fadir Jacob seide, Ye han maad me to be with out children; Joseph is not alyue, Symeon is holdun in bondis, ye schulen take a wey fro me Beniamyn; alle these yuels felden in me.
37 Rubeni akamwambia baba yake, kusema, “Unaweza kuwaua wanangu wawili nisipomrudisha Benjamini kwako. Mweke mikononi mwangu, nami nitamrudisha tena kwako.”
To whom Ruben answeride, Sle thou my twei sones, if Y shal not brynge hym ayen to thee; take thou hym in myn hond, and Y schal restore hym to thee.
38 Yakobo akasema, “Mwanangu atashuka pamoja nanyi. Kwani ndugu yake amekufa na yeye peke yake amebaki. Ikiwa madhara yatampata katika njia mnayoiendea, ndipo mtakapozishusha mvi zangu kaburini kwa huzuni.” (Sheol h7585)
And Jacob seide, My sone schal not go doun with you; his brother is deed, he aloone is left; if ony aduersite schal bifalle `to hym in the lond to which ye schulen go, ye schulen lede forth myn hoore heeris with sorewe to hellis. (Sheol h7585)

< Mwanzo 42 >