< Mwanzo 39 >

1 Yusufu akaletwa Misri. Potifa, aliyekuwa afisa wa Farao mkuu wa walinzi na Mmisri, akamnunua kutoka kwa Waishmaeli, waliokuwa wamempeleka pale.
And Joseph was brought down to Egypt; and Potiphar, an officer of Pharaoh, captain of the guard, an Egyptian, bought him of the hands of the Ishmeelites, which had brought him down thither.
2 Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na akawa mtu aliyefanikiwa. Aliishi katika nyumba ya Mmisri bwana wake.
And the LORD was with Joseph, and he was a prosperous man; and he was in the house of his master the Egyptian.
3 Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye na kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya.
And his master saw that the LORD [was] with him, and that the LORD made all that he did to prosper in his hand.
4 Yusufu akapata kibali mbele zake. Akamtumikia Potifa. Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki, akakiweka chini ya uangalizi wake.
And Joseph found grace in his sight, and he served him: and he made him overseer over his house, and all [that] he had he put into his hand.
5 Ikawa alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki, Yahwe akaibariki nyumba ya Mmisri kwa sababu ya Yusufu. Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani.
And it came to pass from the time [that] he had made him overseer in his house, and over all that he had, that the LORD blessed the Egyptian’s house for Joseph’s sake; and the blessing of the LORD was upon all that he had in the house, and in the field.
6 Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu. Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu. Basi Yusufu alikuwa kijana mzuri na wa kuvutia.
And he left all that he had in Joseph’s hand; and he knew not ought he had, save the bread which he did eat. And Joseph was [a] goodly [person], and well favoured.
7 Ikawa baada ya hayo mke wa bwana wake akamtamani Yusufu. Akamwambia, “Lala nami.”
And it came to pass after these things, that his master’s wife cast her eyes upon Joseph; and she said, Lie with me.
8 Lakini yeye alikataa na kumwambia mke wa bwana wake, “Tazama, bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani, na ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu.
But he refused, and said unto his master’s wife, Behold, my master wotteth not what [is] with me in the house, and he hath committed all that he hath to my hand;
9 Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi. Hajanidhuiria chochote isipokuwa wewe, kwa sababu wewe ni mkewe. Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?
[There is] none greater in this house than I; neither hath he kept back any thing from me but thee, because thou [art] his wife: how then can I do this great wickedness, and sin against God?
10 Akamwambia Yusufu siku baada ya siku, lakini yeye akakataa kulala naye wala kuwa naye.
And it came to pass, as she spake to Joseph day by day, that he hearkened not unto her, to lie by her, [or] to be with her.
11 Ikawa siku moja aliingia ndani kufanya kazi yake. Hakuna mtu yeyote wa nyumbani aliyekuwepo pale ndani.
And it came to pass about this time, that [Joseph] went into the house to do his business; and [there was] none of the men of the house there within.
12 Akashika nguo zake na kusema, “Lala nami.” Akaacha nguo zake mikononi mwake, akakimbia, na kutoka nje.
And she caught him by his garment, saying, Lie with me: and he left his garment in her hand, and fled, and got him out.
13 Ikawa, alipoona kwamba ameziacha nguo zake mikononi mwake na kwamba amekimbia nje,
And it came to pass, when she saw that he had left his garment in her hand, and was fled forth,
14 akawaita watu wa nyumbani mwake na kuwambia, “Tazama, Potifa ameleta Mwebrania huyu kutudhihaki. Aliingia kulala nami, na nikapiga kelele.
That she called unto the men of her house, and spake unto them, saying, See, he hath brought in an Hebrew unto us to mock us; he came in unto me to lie with me, and I cried with a loud voice:
15 Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha na nguo yake, akakimbia, na kutoka nje.”
And it came to pass, when he heard that I lifted up my voice and cried, that he left his garment with me, and fled, and got him out.
16 Akaweka nguo zake karibu naye hata bwana yake alipokuja nyumbani.
And she laid up his garment by her, until his lord came home.
17 Akamwambia maelelezo haya, “Yule mtumishi Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kunidhihaki.
And she spake unto him according to these words, saying, The Hebrew servant, which thou hast brought unto us, came in unto me to mock me:
18 Ikawa nilipopiga kelele, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.”
And it came to pass, as I lifted up my voice and cried, that he left his garment with me, and fled out.
19 Ikawa, bwana wake aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe, “Hivi ndivyo mtumishi wako alivyonitenda,” alikasirika sana.
And it came to pass, when his master heard the words of his wife, which she spake unto him, saying, After this manner did thy servant to me; that his wrath was kindled.
20 Bwana wa Yusufu akamchukua na kumweka gerezani, mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme. Akawa pale kifungoni.
And Joseph’s master took him, and put him into the prison, a place where the king’s prisoners [were] bound: and he was there in the prison.
21 Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu na kumwonyesha uaminifu wa agano. Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza.
But the LORD was with Joseph, and shewed him mercy, and gave him favour in the sight of the keeper of the prison.
22 Mlinzi wa gereza akawaweka mikononi mwa Yusufu wafungwa wote waliokuwa gerezani. Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu.
And the keeper of the prison committed to Joseph’s hand all the prisoners that [were] in the prison; and whatsoever they did there, he was the doer [of it].
23 Mlinzi wa gereza hakuwa na wasiwasi juu ya chochote kilichokuwa mkononi mwake, kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye. Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.
The keeper of the prison looked not to any thing [that was] under his hand; because the LORD was with him, and [that] which he did, the LORD made [it] to prosper.

< Mwanzo 39 >