< Mwanzo 36 >

1 Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edom).
To są dzieje rodu Ezawa, czyli Edomu.
2 Esau akachukua wakeze kutoka kwa Wakanaani. Hawa walikuwa wake zake: Ada binti Eloni Mhiti; Oholibama binti Ana, mjukuu wa Zibeoni Mhivi; na
Ezaw pojął swoje żony z córek Kanaanu: Adę, córkę Elona Chetyty, Oholibamę, córkę Any, córki Sibeona Chiwwity;
3 Basemathi, binti Ishmaeli, dada wa Nebayothi.
I Basmat, córkę Izmaela, siostrę Nebajota.
4 Ada akamzaa Elifazi kwa Esau, na Basemathi akamzaa Reueli.
I Ada urodziła Ezawowi Elifaza, a Basmat urodziła Rehuela.
5 Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu, na Kora. Hawa walikuwa wana wa Esau waliozaliwa kwake katika nchi ya Kananaani.
Oholibama urodziła Jeusza, Jalama i Koracha. To [są] synowie Ezawa, którzy mu się urodzili w ziemi Kanaan.
6 Esau akawachukua wakeze, wanawe, binti zake, na watu wote wa nyumba yake, mifugo wake - wanyama wake wote, na mali yake yote, aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani, na akaenda katika nchi iliyoko mbali kutoka kwa Yakobo nduguye.
I Ezaw wziął swoje żony, synów, córki i wszystkich domowników, swoje stada, wszystkie bydła i całe swoje mienie, które zdobył w ziemi Kanaan, i odszedł od swego brata Jakuba do [innej] ziemi;
7 Alifanya hivi kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana kwa wao kuishi pamoja. Nchi waliyokuwa wamekaa isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao.
Bo ich majątek był tak wielki, że nie mogli mieszkać razem, i ziemia, na której przebywali, nie mogła ich utrzymać z powodu [mnóstwa] ich stad.
8 Hivyo Esau, aliyejulikana pia kama Edomu, akakaa katika nchi ya kilima Seiri.
I Ezaw zamieszkał na górze Seir. Ezaw to Edom.
9 Hivi ndivyo vizazi vya Esau, babu wa Waedomu katika nchi ya mlima Seiri.
A to są dzieje rodu Ezawa, ojca Edomitów, na górze Seir.
10 Haya yalikuwa majina ya wana wa Esau: Elifazi mwana wa Ada, mkewe Esau; Reueli mwana wa Basemathi, mkewe Esau.
I to są imiona synów Ezawa: Elifaz, syn Ady, żony Ezawa, Rehuel, syn Basmat, żony Ezawa.
11 Wana wa Elifazi walikuwa Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi.
Synami zaś Elifaza byli: Teman, Omar, Sefo, Gatam i Kenaz.
12 Timna, suria wa Elifazi, mwana wa Esau, akamzaa Amaleki. Hawa walikuwa wajukuu wa Ada, mkewe Esau.
A Timna była nałożnicą Elifaza, syna Ezawa, i urodziła Elifazowi Amaleka. To [są] synowie Ady, żony Ezawa.
13 Hawa walikuwa wana wa Reueli: Nahathi, Zera, Shama, na Miza. Hawa walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
To [są] synowie Rehuela: Nachat, Zerach, Szamma i Mizza. Byli oni synami Basmat, żony Ezawa.
14 Hawa walikuwa wana wa Oholibama, mkewe Esau, aliyekuwa binti Ana na mjukuu wa Zibeoni. Alimzalia Esau Yeushi, Yalamu, na Kora.
A ci byli synami żony Ezawa Oholibamy, córki Any, córki Sibeona. Urodziła ona Ezawowi Jeusza, Jalama i Koracha.
15 Hizi zilikuwa koo kati ya vizazi vya Esau: uzao wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau: Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora,
To [są] książęta spośród synów Ezawa, synowie Elifaza, pierworodnego Ezawa: książę Teman, książę Omar, książę Sefo, książę Kenaz.
16 Gatamu, na Amaleki. Hivi vilikuwa vizazi vya koo kutoka kwa Elifazi katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Ada.
Książę Korach, książę Gatam, książę Amalek. Ci książęta [pochodzą] z Elifaza, w ziemi Edom, to [są] synowie Ady.
17 Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli, mwana wa Esau: Nahathi, Zera, Shama, Miza. Hizi zilikuwa koo kutoka kwa Reueli katika nchi ya Edomu. Walikuwa wajukuu wa Basemathi, mkewe Esau.
To [są] synowie Rehuela, syna Ezawa: książę Nachat, książę Zerach, książę Szamma, książę Mizza. Ci książęta [pochodzą] z Rehuela, w ziemi Edom. Oni [są] synami Basmat, żony Ezawa.
18 Hizi zilikuwa koo za Oholibama, mkewe Esau: Yeushi, Yalamu, Kora. Hizi ni koo zilizotoka kwa Oholibama mkewe Esau, binti Ana.
A to [są] synowie Oholibamy, żony Ezawa: książę Jeusz, książę Jalam, książę Korach. Ci książęta [pochodzą] z Oholibamy, córki Any, żony Ezawa.
19 Hawa walikuwa wana wa Esau na koo zao.
To [są] synowie Ezawa, czyli Edom, i to [są] ich książęta.
20 Hawa walikuwa wana wa Seiri Mhori, wenyeji wa nchi hiyo: Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana,
A to [są] synowie Seira, Choryty, mieszkańcy tej ziemi: Lotan, Szobal, Sibeon i Ana;
21 Dishoni, Ezeri, na Dishani. Hizi zilikuwa koo the Wahori, wenyeji wa Seiri katika nchi ya Edomu.
Diszon, Eser i Diszan. To [są] książęta Chorytów, synowie Seira w ziemi Edom.
22 Wana wa Lotani walikuwa Hori na Hemani, na Timna alikuwa dada wa Lotani.
Synami Lotana byli: Chori i Hemam; a siostrą Lotana była Tamna.
23 Hawa walikuwa wana wa Shobali: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu.
Synowie zaś Szobala: Alwan, Manachat, Ebal, Szefo i Onam.
24 Hawa walikuwa wana wa Zibeoni: Aia na Ana. Huyu ndiye Ana aliyeona chemichemi za moto nyikani, alipokuwa akichunga punda wa Zibeoni babaye.
Synami Sibeona [są] Ajja i Ana. To ten Ana, który znalazł muły na pustyni, gdy pasł osły swego ojca Sibeona.
25 Hawa walikuwa watoto wa Ana: Dishoni na Oholibama, binti Ana.
A to [są] dzieci Any: Diszon i Oholibama, córka Any.
26 Hawa walikuwa wana wa Dishoni: Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani.
I synowie Diszona: Chemdan, Eszban, Jitran i Keran.
27 Hawa walikuwa wana wa Ezeri: Bilhani, Zaavani, na Akani.
To są synowie Esera: Bilhan, Zaawan i Akan.
28 Hawa walikuwa wana wa Dishani: Uzi na Arani.
I synowie Diszana: Us i Aran.
29 Hizi zilikuwa koo za Wahori: Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana,
To są książęta Chorytów: książę Lotan, książę Szobal, książę Sibeon, książę Ana.
30 Dishoni, Ezeri, Dishani: hizi zilikuwa koo za Wahori, kulingana na ukoo ulivyoorodheshwa katika nchi ya Seiri.
Książę Diszon, książę Eser, książę Diszan. [Są] to książęta Chorytów, według ich księstw, w ziemi Seir.
31 Hawa walikuwa wafalme waliomiliki katika nchi ya Edomu kabla ya mfalme yeyote kumilika juu ya Waisraeli:
To [są] królowie, którzy panowali w ziemi Edom, zanim panował król nad synami Izraela.
32 Bela mwana wa Beori, alitawala huko Edomu, na jina la mji wake lilikuwa Dinhaba.
W Edomie panował Bela, syn Beora, a nazwa jego miasta – Dinhaba.
33 Bela alipofariki, kisha Yobabu mwana wa Zera kutoka Bozra, akatawala mahali pake.
I Bela umarł, a w jego miejsce panował Jobab, syn Zeracha z Bosry.
34 Yobabu alipofariki, Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani, akatawala mahali pake.
Jobab umarł, a w jego miejsce panował Chuszam z ziemi Temanitów.
35 Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi aliyewashinda Wamidiani katika nchi ya Moabu, akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Avithi.
Chuszam umarł, a w jego miejsce panował Hadad, syn Bedada, który pokonał Midianitów na polu Moab, a nazwa jego miasta – Awit.
36 Hadadi alipofariki, kisha Samla wa Masreka akatawala mahali pake.
Hadad umarł, a w jego miejsce panował Samla z Masreki.
37 Samla alipofariki, kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake.
Samla umarł, a w jego miejsce panował Saul z Rechobot nad Rzeką.
38 Shauli alipofariki, kisha Baali Hanani mwana wa Akbori akatawala mahali pake.
Saul umarł, a w jego miejsce panował Baalchanan, syn Akbora.
39 Baali Hanani mwana wa Akbori, alipokufa, kisha Hadari akatawala mahali pake. Jina la mji wake lilikuwa Pau. Jina la mkewe lilikuwa Mehetabeli, binti Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.
Baalchanan, syn Akbora, umarł, a w jego miejsce panował Hadar, a nazwa jego miasta – Pahu, a imię jego żony [to] Mehetabel, [była to] córka Matredy, córki Mezahaba.
40 Haya ndiyo yalikuwa majina ya wakuu wa koo kutoka uzao wa Esau, kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao: Timna, Alva, Yethethi,
To [są] imiona książąt Ezawa, według ich rodów i miejscowości i według ich imion: książę Timna, książę Alwa, książę Jetet.
41 Oholibama, Ela, Pinoni,
Książę Oholibama, książę Ela, książę Pinon.
42 Kenazi, Temani, Mbza,
Książę Kenaz, książę Teman, książę Mibsar.
43 Magdieli, na Iramu. Hawa walikuwa wakuu wa ukoo wa Edomu, kwa kufuata makao yao katika nchi waliyomiliki. Nao ni Esau, baba wa Waedomu.
Książę Magdiel, książę Iram. To [są] książęta Edomu według miejsca ich zamieszkania w ziemi ich posiadłości. To [jest] Ezaw, ojciec Edomitów.

< Mwanzo 36 >