< Mwanzo 30 >

1 Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto, Raheli akamwonea wivu dada yake. Akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, sivyo nitakufa.”
And when Rahel saw that she bare Iaakob no children, Rahel enuied her sister, and said vnto Iaakob, Giue me children, or els I dye.
2 Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli. Akasema, “Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?
Then Iaakobs anger was kindled against Rahel, and he sayde, Am I in Gods steade, which hath withholden from thee the fruite of the wombe?
3 Akasema, “Tazama, kuna mjakazi wangu Bilha. Lala naye, hivyo aweze kuzaa watoto magotini pangu, nami nitapata watoto kwake.
And she said, Behold my maide Bilhah, goe in to her, and she shall beare vpon my knees, and I shall haue children also by her.
4 Hivyo akampa Bilha mjakazi kama mke wake, na Yakobo akalala naye.
Then shee gaue him Bilhah her mayde to wife, and Iaakob went in to her.
5 Bilha akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana.
So Bilhah conceiued and bare Iaakob a sonne.
6 Kisha Raheli akasema, “Mungu ameamua kwa faida yangu. Ameyasikiliza maombi yangu na kunipa mwana.” Kwa sababu hiyo akamwita jina lake Dani
Then said Rahel, God hath giuen sentence on my side, and hath also heard my voyce, and hath giuen mee a sonne: therefore called shee his name, Dan.
7 Bilha, mjakazi wa Raheli, akashika mimba tena na kumzalia Yakobo mwana wa pili.
And Bilhah Rahels maide coceiued againe, and bare Iaakob the second sonne.
8 Raheli akasema, “Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu na kushinda.” Akamwita jina lake Naftali.
Then Rahel said, with excellent wrestlings haue I wrestled with my sister, and haue gotten the vpper hande: and shee called his name, Naphtali.
9 Lea alipoona kwamba ameacha kuzaa, akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake.
And when Leah saw that she had left bearing, shee tooke Zilpah her mayde, and gaue her Iaakob to wife.
10 Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
And Zilpah Leahs mayde bare Iaakob a sonne.
11 Lea akasema, “Hii ni bahati njema!” Hivyo akamwita jina lake Gadi.
Then sayd Leah, A companie commeth: and she called his name, Gad.
12 Kisha Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
Againe Zilpah Leahs mayde bare Iaakob another sonne.
13 Lea akasema, “Nina furaha! Kwa maana mabinti wataniita furaha.” Hivyo akamwita jina lake Asheri.
Then sayde Leah, Ah, blessed am I, for the daughters will blesse me. and she called his name, Asher.
14 Siku za mavuno ya ngano Rubeni akaenda shambani na kuona tunguja. Akazileta kwa mama yake. Kisha Raheli akamwambia Lea, “Nipe baadhi ya tunguja za mwanao.”
Nowe Reuben went in the dayes of the wheateharuest, and founde mandrakes in the fielde and brought them vnto his mother Leah. Then sayde Rahel to Leah, Giue me, I pray thee, of thy sonnes mandrakes.
15 Lea akamwambia, “Je ni jambo dogo kwako, kumchukua mme wangu? Je na sasa unataka kuchukua tunguja za mwanangu pia? Raheli akasema, “Kisha atalala nawe leo usiku, kwa kubadilishana na tunguja za mwanao.
But shee answered her, Is it a small matter for thee to take mine husband, except thou take my sonnes mandrakes also? Then sayde Rahel, Therefore he shall sleepe with thee this night for thy sonnes mandrakes.
16 Jioni Yakobo akaja kutoka uwandani. Lea akaenda kumlaki na kusema, “Leo usiku utalala nami, kwani nimekuajiri kwa tunguja za mwanangu.” Hivyo Yakobo akalala na Lea usiku huo.
And Iaakob came from the fielde in the euening, and Leah went out to meete him, and sayde, Come in to mee, for I haue bought and payed for thee with my sonnes mandrakes: and he slept with her that night.
17 Mungu akamsikia Lea, na akashika mimba na kumzalia Yakobo mwana wa tano.
And God heard Leah and shee conceiued, and bare vnto Iaakob the fift sonne.
18 Lea akasema, “Mungu amenipa ujira wangu, kwa sababu nilimpa mme wangu mjakazi wangu.” Akamwita jina lake Isakari.
Then said Leah, God hath giuen me my reward, because I gaue my mayde to my husband, and she called his name Issachar.
19 Lea akashika mimba tena na kuzaa mwana wa tano kwa Yakobo.
After, Leah conceiued againe, and bare Iaakob the sixt sonne.
20 Lea akasema, “Mungu amenipa zawadi njema. Sasa mme wangu ataniheshimu, kwa sababu nimemzalia wana sita.” Akamwita jina lake Zabuloni.
Then Leah said, God hath endued me with a good dowrie: nowe will mine husband dwell with me, because I haue borne him sixe sonnes: and she called his name Zebulun.
21 Baadaye akazaa binti na kumwita jina lake Dina.
After that, shee bare a daughter, and shee called her name Dinah.
22 Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza. Akampa kushika mimba.
And God remembred Rahel, and God heard her, and opened her wombe.
23 Akashika mimba na kuzaa mwana. Akasema, “Mungu ameiondoa aibu yangu.”
So she conceiued and bare a sonne, and said, God hath taken away my rebuke.
24 Akamwita jina lake Yusufu, akisema, Yahwe ameniongeza mwana mwingine.”
And shee called his name Ioseph, saying, The Lord wil giue me yet another sonne.
25 Baada ya Raheli kumzaa Yusufu, Yakobo akamwambia Labani, “Niache niande, ili kwamba niende nyumbani kwetu na katika nchi yangu.
And assoone as Rahel had borne Ioseph, Iaakob said to Laban, Sende me away that I may go vnto my place and to my countrey.
26 Nipe wake zangu na watoto wangu niliokutumikia kwa ajili yao, na uniache niondoke, kwani unafahamu nilivyokutumikia.
Giue me my wiues and my children, for whom I haue serued thee, and let me go: for thou knowest what seruice I haue done thee.
27 Labani akamwambia, “Ikiwa nimepata kibali machoni pako, subiri, kwa sababu nimejifunza kwa kutumia uaguzi kwamba Yahwe amenibariki kwa ajili yako.”
To whom Laban answered, If I haue nowe found fauour in thy sight tarie: I haue perceiued that the Lord hath blessed me for thy sake.
28 Kisha akasema, “Taja ujira wako, nami nitalipa.”
Also he said, Appoynt vnto me thy wages, and I will giue it thee.
29 Yakobo akamwambia, “Unajua nilivyokutumikia, na jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami.
But he sayd vnto him, Thou knowest, what seruice I haue done thee, and in what taking thy cattell hath bene vnder me.
30 Kwani walikuwa wachache kabla sijaja, na wameongezeka kwa wingi. Popote nilipokutumikia Mungu amekubariki. Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?”
For the litle, that thou haddest before I came, is increased into a multitude: and the Lord hath blessed thee by my comming: but nowe when shall I trauell for mine owne house also?
31 Hivyo Labani akasema, “Je nikulipe nini? Yakobo akasema, 'Usinipe chochote. Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu, nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza.
Then he saide, What shall I giue thee? And Iaakob answered, Thou shalt giue mee nothing at all: if thou wilt doe this thing for mee, I will returne, feede, and keepe thy sheepe.
32 Niache nipite kati ya kundi lako lote leo, kwa kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi. Hawa watakuwa ujira wangu.
I wil passe through all thy flockes this day, and separate from them all the sheepe with litle spots and great spots, and al blacke lambes among the sheepe, and the great spotted, and litle spotted among the goates: and it shalbe my wages.
33 Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye, utakapokuja kuangalia ujira wangu. Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa.”
So shall my righteousnesse answere for me hereafter, when it shall come for my rewarde before thy face, and euery one that hath not litle or great spots among the goates, and blacke among the sheepe, the same shalbe theft with me.
34 Labani akasema, “Nakubali. Na iwe kama yalivyo maneno yako.”
Then Laban sayde, Goe to, woulde God it might be according to thy saying.
35 Siku hiyo Labani akaondoa mabeberu yaliyokuwa na milia na madoa, na majike ya mbuzi yaliyokuwa na milia na madoa, kila aliyekuwa mweupe, na weusi wote katika mbuzi, akawakabidhi katika mikono ya wanaye.
Therefore he tooke out the same day the hee goates that were partie coloured and with great spots, and all the shee goates with litle and great spots, and all that had white in them, and all the blacke among the sheepe, and put them in the keeping of his sonnes.
36 Pia Labani akaweka safari ya siku tatu kati yake na Yakobo. Hivyo Yakobo akabaki kuchunga wale kondoo wa Labani waliosalia.
And hee set three dayes iourney betweene himselfe and Iaakob. And Iaakob kept the rest of Labans sheepe.
37 Yakobo akachukua matawi mabichi yaliyokatwa ya mipopla, mlozi na mwaramoni mbichi akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane.
Then Iaakob tooke rods of greene popular, and of hasell, and of the chesnut tree, and pilled white strakes in them, and made the white appeare in the rods.
38 Kisha akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji. Wakashika mimba walipokuja kunywa maji.
Then he put the rods, which he had pilled, in the gutters and watering troughes, when the sheepe came to drink, before the sheepe. (for they were in heate, when they came to drinke)
39 Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa.
And the sheepe were in heate before the rods, and afterward brought forth yong of partie colour, and with small and great spots.
40 Yakobo akawatenga hawa wanakondoo, lakini akawafanya waliosalia kuelekea wanyama wenye milia na kondoo weusi wote katika kundi la Labani. Kisha akayatenga makundi yake mwenyewe pekee na hakuwaweka pamoja na wale wa Labani.
And Iaakob parted these lambes, and turned the faces of the flocke towardes these lambes partie coloured and all maner of blacke, among the sheepe of Laban: so hee put his owne flockes by themselues, and put them not with Labans flocke.
41 Pindi kondoo wenye nguvu katika kundi walipopandana, Yakobo alilaza fito katika mabirika ya maji mbele ya macho ya kundi, ili kwamba washike mimba kati ya fito.
And in euery ramming time of the stronger sheepe, Iaakob layde the rods before the eyes of the sheepe in the gutters, that they might conceiue before the rods.
42 Lakini wakati waliodhaifu walipokuja, hakuweka fito mbele yao. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo.
But when the sheepe were feeble, hee put them not in: and so the feebler were Labans, and the stronger Iaakobs.
43 Mtu huyo akastawi sana. Akawa na kundi kubwa la kondoo, wajakazi na wajoli, ngamia na punda.
So the man increased exceedingly, and had many flockes, and maide seruantes, and men seruants, and camels and asses.

< Mwanzo 30 >