< Mwanzo 21 >

1 Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
E o Senhor visitou a Sarah, como tinha dito; e fez o Senhor a Sarah como tinha falado.
2 Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
E concebeu Sarah, e pariu a Abraão um filho na sua velhice, ao tempo determinado, que Deus lhe tinha dito.
3 Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
E chamou Abraão o nome de seu filho que lhe nascera, que Sarah lhe parira, Isaac.
4 Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
E Abraão circuncidou o seu filho Isaac, quando era da idade de oito dias, como Deus lhe tinha ordenado.
5 Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
E era Abraão da idade de cem anos, quando lhe nasceu Isaac seu filho.
6 Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
E disse Sarah: Deus me tem feito riso: todo aquele que o ouvir, se rirá comigo.
7 Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
Disse mais: Quem diria a Abraão que Sarah daria de mamar a filhos? porque pari-lhe um filho na sua velhice.
8 Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
E cresceu o menino, e foi desmamado; então Abraão fez um grande banquete no dia em que Isaac foi desmamado.
9 Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
E viu Sarah que zombava o filho de Hagar a egípcia, o qual tinha parido a Abraão.
10 Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
E disse a Abraão: Deita fora esta serva e o seu filho; porque o filho desta serva não herdará com meu filho, com Isaac.
11 Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
E pareceu esta palavra mui má aos olhos de Abraão, por causa de seu filho.
12 Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
Porém Deus disse a Abraão: Não te pareça mal aos teus olhos acerca do moço, e acerca da tua serva; em tudo o que Sarah te diz, ouve a sua voz; porque em Isaac será chamada a tua semente
13 Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
Mas também do filho desta serva farei uma nação, porquanto é tua semente.
14 Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
Então se levantou Abraão pela manhã de madrugada, e tomou pão, e um odre d'água, e os deu a Hagar, pondo-os sobre o seu ombro; também lhe deu o menino, e despediu-a; e ela foi-se, andando errante no deserto de Berseba.
15 Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
E consumida a água do odre, lançou o menino debaixo de uma das árvores.
16 Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
E foi-se, e assentou-se em frente, afastando-se a distância dum tiro de arco; porque dizia: Que não veja morrer o menino. E assentou-se em frente, e levantou a sua voz, e chorou.
17 Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
E ouviu Deus a voz do menino, e bradou o anjo de Deus a Hagar desde os céus, e disse-lhe: Que tens, Hagar? não temas, porque Deus ouviu a voz do moço desde o lugar onde está.
18 Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
Ergue-te, levanta o moço, e pega-lhe pela mão, porque dele farei uma grande nação.
19 Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
E abriu-lhe Deus os olhos, e viu um poço d'água: e foi-se, e encheu o odre d'água, e deu de beber ao moço.
20 Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
E era Deus com o moço, que cresceu; e habitou no deserto, e foi flecheiro.
21 Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
E habitou no deserto de Paran; e sua mãe tomou-lhe mulher da terra do Egito.
22 Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
E aconteceu naquele mesmo tempo que Abimelech, com Phichol, príncipe do seu exército, falou com Abraão, dizendo: Deus é contigo em tudo o que fazes;
23 Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
Agora pois, jura-me aqui por Deus que me não mentirás a mim, nem a meu filho, nem a meu neto: segundo a beneficência que te fiz, me farás a mim, e à terra onde peregrinaste.
24 Abraham akasema, “Nina apa.”
E disse Abraão: Eu jurarei.
25 Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
Abraão, porém, repreendeu a Abimelech por causa de um poço d'água, que os servos de Abimelech haviam tomado por força.
26 Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
Então disse Abimelech: Eu não sei quem fez isto; e também tu mo não fizeste saber, nem eu o ouvi senão hoje.
27 Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
E tomou Abraão ovelhas e vacas, e deu-as a Abimelech; e fizeram ambos concerto.
28 Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
Pôs Abraão, porém, à parte sete cordeiras do rebanho.
29 Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
E Abimelech disse a Abraão: Para que estão aqui estas sete cordeiras, que puseste à parte?
30 Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
E disse: Tomarás estas sete cordeiras de minha mão, para que sejam em testemunho que eu cavei este poço.
31 Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
Por isso se chamou aquele lugar Berseba, porquanto ambos juraram ali.
32 Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
Assim fizeram concerto em Berseba. Depois se levantou Abimelech e Phichol, príncipe do seu exército, e tornaram-se para a terra dos philisteus.
33 Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
E plantou um bosque em Berseba, e invocou lá o nome do Senhor, Deus eterno.
34 Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.
E peregrinou Abraão na terra dos philisteus muitos dias.

< Mwanzo 21 >