< Mwanzo 13 >

1 Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
So Abram came up out of Egypt he and his wife and all that he had and Lot with him, towards the South.
2 Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
Now, Abram, was very rich, —in cattle, in silver and in gold.
3 Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
And he went his way, by his removals, from the South even as far as to Bethel, —as far as the place where his tent was at the beginning, between Bethel and Ai:
4 Akaenda mahali ambapo madhabahu ilikuwa imejengwa mwanzoni. Hapa akaliitia jina la Yahwe.
unto the place of the altar, which he made there at first, —and Abram called there, on the name of Yahweh.
5 aliyekuwa anasafiri na Abram, alikuwa pia na ngo'mbe, makundi ya mifugo, na mahema.
Now, Lot also, who was going with Abram, had flocks and herds and tents.
6 Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
And the land suffered them not to dwell together, —because their substance had become, great, so that they could not dwell together.
7 Pia, kulikuwa na ugomvi kati ya wachunga wanyama wa Abram na wachunga wanyama wa Lutu. Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo.
And there arose a strife betwixt the herdmen of Abram, and the herdmen of Lot. Now the Canaanite and the Perizzite, were then dwelling in the land.
8 Kwa hiyo Abram akamwambia Lutu, “Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi, na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu; licha ya hayo sisi ni familia.
So then Abram said unto Lot Pray let not cause of strife arise betwixt me and thee, or betwixt my herdmen and thy herdmen; for brethren, are we.
9 Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
Is not, all the land, before thee? I pray thee, separate thyself from me, —if to the left hand, then I will go to the right, if to the right hand, then I will go to the left.
10 Kwa hiyo Lutu akatazama, na akaona kuwa nchi yote tambarare ya Yorodani ilikuwa na maji kila mahali hadi Zoari, kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri. Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora.
So Lot lifted up his eyes and beheld all the circuit of the Jordan, that the whole of it, was well-watered, —before Yahweh destroyed Sodom and Gomorrah, like the Garden of Yahweh, like the land of Egypt, as thou enterest into Zoar.
11 Kwa hiyo Lutu akajichagulia yeye mwenyewe nchi tambarare ya Yorodani na akasafiri mashariki, na ndugu hawa wakatengana wao kwa wao.
And Lot chose for himself all the circuit of the Jordan, so Lot brake up eastwards, —and they separated themselves, each man from his brother:
12 Abram akaishi katika nchi ya Kanaani, na Lutu akaishi katika miji ya tambarare. Akatandaza hema zake hadi Sodoma.
Abram, fixed his dwelling in the land of Canaan, —but, Lot, fixed his dwelling among the cities, of the circuit, and moved his tent as far as Sodom.
13 Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
Now, the men of Sodom were base and sinful, —against Yahweh, exceedingly.
14 Yahwe akamwambia Abram baada ya Lutu kuondoka kwake, “Angalia kuanzia mahali ulipo simama hadi kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.
And, Yahweh, said unto Abram after that Lot had separated himself from him, Lift up, I pray thee thine eyes and look, from the place where thou art, —northward and southward and eastward and westward;
15 Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
for all the land which thou art beholding—to thee, will I give it, and to thy seed unto times age-abiding;
16 Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
and I will make thy seed as the dust of the earth, —so that if a man can number the dust of the earth, thy seed also, may be numbered.
17 Inuka, tembea katika urefu na upana wa nchi hii, kwa kuwa nitakupatia.”
Rise! go up and down in the land, to the length thereof and to the breadth thereof, for to thee, will I give it.
18 Kwa hiyo Abram akachukua hema yake, akaja na kukaa katika mwaloni wa Mamre, ambao uko Hebroni, na pale akajenga Madhabahu ya Yahwe.
So Abram moved his tent and came in and dwelt among the oaks of Mamre, which were in Hebron, —and built there an altar to Yahweh.

< Mwanzo 13 >