< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
Erat autem terra labii unius, et sermonum eorumdem.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
Cumque proficiscerentur de oriente, invenerunt campum in terra Sennaar, et habitaverunt in eo.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
Dixitque alter ad proximum suum: Venite, faciamus lateres, et coquamus eos igni. Habueruntque lateres pro saxis, et bitumen pro cæmento:
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
et dixerunt: Venite, faciamus nobis civitatem et turrim, cujus culmen pertingat ad cælum: et celebremus nomen nostrum antequam dividamur in universas terras.
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
Descendit autem Dominus ut videret civitatem et turrim, quam ædificabant filii Adam,
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
et dixit: Ecce, unus est populus, et unum labium omnibus: cœperuntque hoc facere, nec desistent a cogitationibus suis, donec eas opere compleant.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Venite igitur, descendamus, et confundamus ibi linguam eorum, ut non audiat unusquisque vocem proximi sui.
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
Atque ita divisit eos Dominus ex illo loco in universas terras, et cessaverunt ædificare civitatem.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
Et idcirco vocatum est nomen ejus Babel, quia ibi confusum est labium universæ terræ: et inde dispersit eos Dominus super faciem cunctarum regionum.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
Hæ sunt generationes Sem: Sem erat centum annorum quando genuit Arphaxad, biennio post diluvium.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sem, postquam genuit Arphaxad, quingentis annis: et genuit filios et filias.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
Porro Arphaxad vixit triginta quinque annis, et genuit Sale.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Arphaxad, postquam genuit Sale, trecentis tribus annis: et genuit filios et filias.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
Sale quoque vixit triginta annis, et genuit Heber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sale, postquam genuit Heber, quadringentis tribus annis: et genuit filios et filias.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
Vixit autem Heber triginta quatuor annis, et genuit Phaleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Et vixit Heber postquam genuit Phaleg, quadringentis triginta annis: et genuit filios et filias.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
Vixit quoque Phaleg triginta annis, et genuit Reu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Phaleg, postquam genuit Reu, ducentis novem annis: et genuit filios et filias.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
Vixit autem Reu triginta duobus annis, et genuit Sarug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixit quoque Reu, postquam genuit Sarug, ducentis septem annis: et genuit filios et filias.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
Vixit vero Sarug triginta annis, et genuit Nachor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Sarug, postquam genuit Nachor, ducentis annis: et genuit filios et filias.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
Vixit autem Nachor viginti novem annis, et genuit Thare.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
Vixitque Nachor, postquam genuit Thare, centum decem et novem annis: et genuit filios et filias.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
Vixitque Thare septuaginta annis, et genuit Abram, et Nachor, et Aran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
Hæ sunt autem generationes Thare: Thare genuit Abram, Nachor et Aran. Porro Aran genuit Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
Mortuusque est Aran ante Thare patrem suum, in terra nativitatis suæ, in Ur Chaldæorum.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
Duxerunt autem Abram et Nachor uxores: nomen uxoris Abram, Sarai: et nomen uxoris Nachor, Melcha filia Aran, patris Melchæ, et patris Jeschæ.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
Erat autem Sarai sterilis, nec habebat liberos.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
Tulit itaque Thare Abram filium suum, et Lot filium Aran, filium filii sui, et Sarai nurum suam, uxorem Abram filii sui, et eduxit eos de Ur Chaldæorum, ut irent in terram Chanaan: veneruntque usque Haran, et habitaverunt ibi.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
Et facti sunt dies Thare ducentorum quinque annorum, et mortuus est in Haran.

< Mwanzo 11 >