< Mwanzo 10 >

1 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
Voici les descendants des fils de Noé: Sem, Cham et Japhet, auxquels naquirent des enfants après le déluge.
2 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
Les fils de Japhet sont Gomer, Magog, Madaï, Javan, Tubal, Méshec, et Tiras.
3 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
Et les fils de Gomer, Ashkénas, Riphath, et Togarma.
4 Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
Et les fils de Javan, Elisha et Tarsis, Kittim et Dodanim.
5 Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
Par eux furent peuplées les îles des nations, dans leurs terres, chacun selon sa langue, selon leurs familles, selon leurs nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
Et les fils de Cham, sont Cush, Mitsraïm, Put et Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
Et les fils de Cush, Seba, Havila, Sabta, Raema et Sabteca. Et les fils de Raema, Sheba et Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
Et Cush engendra Nimrod, qui commença à être puissant sur la terre.
9 Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
Il fut un puissant chasseur devant l'Éternel. C'est pour cela qu'on dit: Comme Nimrod, puissant chasseur devant l'Éternel.
10 Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
Et le commencement de son royaume fut Babel, Érec, Accad et Calné, dans le pays de Shinear.
11 Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
De ce pays-là il sortit en Assyrie, et il bâtit Ninive, Rehoboth-Ir, Calach,
12 na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
Et Résen, entre Ninive et Calach; c'est la grande ville.
13 Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
Et Mitsraïm engendra les Ludim, les Anamim, les Lehabim, les Naphtuhim,
14 Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
Les Pathrusim, les Casluhim (d'où sont sortis les Philistins) et les Caphtorim.
15 Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
Et Canaan engendra Sidon, son premier-né, et Heth;
16 pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
Les Jébusiens, les Amoréens, les Guirgasiens;
17 Mhivi, Mwarki, Msini,
Les Héviens, les Arkiens, les Siniens;
18 Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
Les Arvadiens, les Tsemariens, les Hamathiens. Ensuite les familles des Cananéens se dispersèrent.
19 Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
Et la limite des Cananéens fut depuis Sidon, en venant vers Guérar, jusqu'à Gaza, en venant vers Sodome, Gomorrhe, Adma, et Tseboïm, jusqu'à Lésha.
20 Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
Ce sont là les fils de Cham, selon leurs familles, selon leurs langues, dans leurs terres, dans leurs nations.
21 Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
Il naquit aussi des fils à Sem, père de tous les fils d'Héber, et frère aîné de Japhet.
22 Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
Les fils de Sem sont Élam, Assur, Arpacshad, Lud et Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
Et les fils d'Aram, Uts, Hul, Guéther et Mash.
24 Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
Et Arpacshad engendra Shélach, et Shélach engendra Héber.
25 Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
Et à Héber il naquit deux fils: le nom de l'un est Péleg (partage), car en son temps la terre fut partagée; et le nom de son frère, Jockthan.
26 Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
Et Jockthan engendra Almodad, Sheleph, Hatsarmaveth, et Jérach;
27 Hadoram, Uzali, Dikla,
Hadoram, Uzal, Dikla,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
Obal, Abimaël, Sheba,
29 Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
Ophir, Havila, et Jobab. Tous ceux-là sont fils de Jockthan.
30 Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
Et leur demeure était depuis Mésha, en venant vers Sephar, vers la montagne d'Orient.
31 Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
Ce sont là les fils de Sem, selon leurs familles, selon leurs langues, selon leurs terres, selon leurs nations.
32 Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.
Telles sont les familles des fils de Noé, selon leurs générations, dans leurs nations; et c'est d'eux que sont sorties les nations de la terre après le déluge.

< Mwanzo 10 >