< Ezekieli 28 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of Jehovah came unto me, saying,
2 “Mwanadamu, waambie watawala wa Tiro, 'Bwana Yahwe asema hivi: Moyo wako unakiburi! Umesema, “mimi ni mungu! Nitakaa kwenye kiti cha miungu katika moyo wa bahari!” Ingawa wewe ni mtu na sio mungu, unaufanya moyo wako kama moyo wa mungu,
Son of man, say unto the prince of Tyre, Thus saith the Lord Jehovah: Because thy heart is lifted up, and thou hast said, I am a god, I sit [in] the seat of God, in the heart of the seas, (and thou art a man, and not God, ) and thou settest thy heart as the heart of God:
3 unafikiri kwamba unahekima kuliko Danieli, na kwamba hakuna siri ikushangazayo!
behold, thou art wiser than Daniel! nothing secret is obscure for thee;
4 Umejitajirisha mwenyewe pamoja na hekima na ujuzi, na kujipatia dhahabu na fedha katika hazina yako!
by thy wisdom and by thine understanding thou hast gotten thee riches, and hast gotten gold and silver into thy treasures;
5 Kwa hekima kubwa na kwa biashara yako, umeongeza utajiri wako, hivyo moyo wako una kiburi kwa sababu ya utajiri yako.
by thy great wisdom thou hast by thy traffic increased thy riches, and thy heart is lifted up because of thy riches.
6 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umetengeza moyo wako kama moyo wa mungu,
Therefore thus saith the Lord Jehovah: Because thou hast set thy heart as the heart of God,
7 kwa hiyo nitaleta wageni juu yako, watu wa kuogofya kutoka mataifa mengine. Wataleta panga zao juu hekima ya uzuri wako, na watauchafua uzuri wako.
therefore behold, I will bring strangers upon thee, the terrible of the nations; and they shall draw their swords against the beauty of thy wisdom, and they shall tarnish thy brightness.
8 Watakupeleka chini hata kwenye shimo, na utakufa kifo cha waliokufa katika Bahari.
They shall bring thee down to the pit, and thou shalt die the deaths of those that are slain in the heart of the seas.
9 Je! kweli utasema, “Mimi ni mungu” mbele ya uso wa yule akuuaye? Wewe ni mwanadamu na sio Mungu, na utakuwa kwenye mkono wa yule akujeruaye.
Wilt thou then say before him that slayeth thee, I am God? but thou shalt be a man, and not God, in the hand of him that pierceth thee.
10 Utakufa kifo cha asiyetahiriwa kwa mkono wa wageni kwa kuwa nimesema hili-asema Bwana Yahwe.
Thou shalt die the deaths of the uncircumcised, by the hand of strangers: for I have spoken [it], saith the Lord Jehovah.
11 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of Jehovah came unto me, saying,
12 “Mwanadamu, inua maombolezo kwa ajili ya mfalme wa Tiro na umwambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Uliumbwa mkamilifu, umejaa hekima na ukamilifu wa hekima.
Son of man, take up a lamentation upon the king of Tyre, and say unto him, Thus saith the Lord Jehovah: Thou, who sealest up the measure of perfection, full of wisdom and perfect in beauty,
13 Ulikuwa katika Edeni, bustani ya Mungu. Kila jiwe la thamani lilikufunika: akiki, yakuti manjano, almasi, zabarajadi, shohamu, yaspi, yakuti samawi, zumaridi, baharamani, na dhahabu. Ilikuwa siku uliyokuwa umeiumba ambayo walikuwa wameiandaa.
thou wast in Eden, the garden of God. Every precious stone was thy covering: the sardius, the topaz, and the diamond, the chrysolite, the onyx, and the jasper, the sapphire, the carbuncle, and the emerald, and gold. The workmanship of thy tambours and of thy pipes was in thee: in the day that thou wast created were they prepared.
14 Nimekuweka juu ya mlima mtakatifu wa Mungu kama kerubi nimekutia mafuta kwa ajili ya kumlinda mwanadamu. Ulikuwa kati ya mawe ya moto ulipozunguka.
Thou wast the anointed covering cherub, and I had set thee [so]: thou wast upon the holy mountain of God; thou didst walk up and down in the midst of stones of fire.
15 Ulikuwa mwadilifu kwenye njia zako kutoka siku ulipoumbwa hadi uovu ulipoonekana ndani yako.
Thou wast perfect in thy ways, from the day that thou wast created, till unrighteousness was found in thee.
16 Kupitia biashara yako kubwa uliyokuwa umeijaza kwa udhalimu, hivyo umetenda dhambi. Hivyo nimekutupilia mbali ya mlima wa Mungu, kama mmoja wao wa aliyekuwa ameninajisi, na nimekuharibu, kerubi mlinzi, na kukutoa miongono mwa mawe ya moto.
By the abundance of thy traffic they filled the midst of thee with violence, and thou hast sinned; therefore have I cast thee as profane from the mountain of God, and have destroyed thee, O covering cherub, from the midst of the stones of fire.
17 Moyo wako ulikuwa na kiburi kwa uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya fahari yako. Nimekupeleka chini kwenye dunia. Nimekuweka mbele ya wafalme ili waweze kukuona.
Thy heart was lifted up because of thy beauty; thou hast corrupted thy wisdom by reason of thy brightness: I have cast thee to the ground, I have laid thee before kings, that they may behold thee.
18 Kwa sababu ya wingi wa dhambi zako na biashara za udanganyifu, umepanajisi mahali pako patakatifu. Basi nimetengeneza moto kutoka ndani yako; utakula wewe. Nitakugeuza kwenye majivu juu ya dunia katika macho ya wote wakutazamao.
By the multitude of thine iniquities, by the unrighteousness of thy traffic, thou hast profaned thy sanctuaries: and I have brought forth a fire out of the midst of thee — it hath consumed thee; and I have brought thee to ashes upon the earth, in the sight of all them that behold thee.
19 Wale wote waliokujua miongoni mwa watu watakao kutetemekewa; watakuwa watu wa kutisha, na hutakuwepo tena milele.”'
All they that know thee among the peoples shall be amazed at thee: thou art become a terror, and thou shalt never be any more.
20 Kisha neno la Bwana Yahwe likanijia, kusema,
And the word of Jehovah came unto me, saying,
21 “Mwanadamu, elekeza uso wako Sidoni na toa utabiri juu yake.
Son of man, set thy face towards Zidon, and prophesy against it,
22 Sema, Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Niko juu yako, Sidoni! Kwa kuwa nitatukuzwa kati yako hivyo watu wako watajua kwamba mimi ni Yahwe wakati nitakapokuwa nimezitekeleza hukumu ndani yako. Nitaonyesha utakatifu ndani yako.
and say, Thus saith the Lord Jehovah: Behold, I am against thee, Zidon, and I will be glorified in the midst of thee; and they shall know that I [am] Jehovah, when I shall have executed judgments in her, and shall be hallowed in her.
23 Nitapeleka tauni juu yako na tazama mitaa yako, na walioua wataanguka kati yako. Wakati upanga utakapokuja juu yao kutoka pande zote, kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
And I will send into her the pestilence, and blood in her streets; and the wounded shall fall in the midst of her, by the sword upon her on every side: and they shall know that I [am] Jehovah.
24 Kisha hakutakuwa na mtemba uchomao na maumivu ya miba kwa ajili ya nyumba ya Israeli kutoka wale wote waliomzunguka wanaowadharau watu wake, hivyo watajua kwamba mimi ni Bwana Yahwe!'
And there shall be no more a wounding sting for the house of Israel, nor any grieving thorn, among all that were round about them, that despised them: and they shall know that I [am] the Lord Jehovah.
25 Bwana Yahwe asema hivi, Nitakapowakusanya nyumba ya Israeli kutoka miongni mwa watu waliokuwa wamekusanyika, na wakati nilipokuwa nimewatenga miongoni mwao, hivyo mataifa aanaweza kuona, kisha watafanya nyumba zao katika nchi nitakayo mpatia mtumishi wangu Yakobo.
Thus saith the Lord Jehovah: When I shall have gathered the house of Israel from the peoples among whom they are scattered, and shall be hallowed in them in the sight of the nations, then shall they dwell in their land which I have given to my servant Jacob.
26 Kisha wataishi salama ndani yake na kujenga nyumba, kulima mizabibu, na kuishi salama wakati nitakapo zitekeleza hukumu juu ya wote wale ambao sasa wanawadharau kutoka sehemu zote; basi watajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao!”'
They shall dwell in it in safety, and shall build houses and plant vineyards; and they shall dwell in safety, when I have executed judgments upon all those that despised them round about them: and they shall know that I [am] Jehovah their God.

< Ezekieli 28 >