< Ezekieli 27 >

1 Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
Again the word of Yahweh came to me, saying,
2 “Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
“Now you, son of man, begin a lamentation concerning Tyre,
3 na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
and say to Tyre, who lives within the gates of the sea, merchants of peoples to many islands, the Lord Yahweh says this to you: Tyre, you have said, 'I am perfect in beauty.'
4 Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
Your borders are in the heart of the seas; your builders have perfected your beauty.
5 Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
They have made all your planks with cypress from Mount Hermon; they took cedar from Lebanon to make a mast for you.
6 Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
They made your oars from the oaks of Bashan; they made your decks out of cypress wood from Cyprus, and they overlaid them with ivory.
7 Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
Your sails were made from colorful linen from Egypt that served as your banner; the colors of blue and purple from the coasts of Elishah are used for the awning on your boat.
8 Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
Those who were living in Sidon and Arvad were your rowers; the sages of Tyre were within you; they were your pilots.
9 Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
Highly experienced craftsmen from Byblos filled your seams; all the ships of the sea and their sailors among you were carrying your merchandise for trade.
10 Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
Persia, Lydia, and Libya were in your army, your men of war. they hung shield and helmet within you; they showed your splendor.
11 Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
The men of Arvad and Helek in your army were on your walls surrounding you, and the people of Gammad were in your towers. They hung up their shields on your walls all around you! They completed your beauty.
12 Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
Tarshish was a trading partner with you because of your abundant wealth of goods to sell: Silver, iron, tin, and lead. They bought and sold your wares!
13 Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
Javan, Tubal, and Meshech—they traded slaves and in items made of bronze. They handled your merchandise.
14 Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
Beth Togarmah provided horses, stallions, and mules as your merchandise.
15 Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
The men of Rhodes were your traders on many coasts. Merchandise was in your hand; they sent back horn, ivory, and ebony as tribute!
16 Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
Aram was a dealer in your many products; they provided emeralds, purple, colored cloth, fine fabric, pearls, and rubies as your merchandise.
17 Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
Judah and the land of Israel were trading with you. They provided wheat from Minnith, cakes, honey, oil, and balsam as your merchandise.
18 Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
Damascus was a trader of all your products, of all your enormous wealth, and of the wine of Helbon and the wool of Zahar.
19 Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
Dan and Javan from Izal provided you with merchandise of wrought iron, cinnamon, and calamus. This became merchandise for you.
20 Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
Dedan was your dealer in fine saddle blankets.
21 Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia and all the chiefs of Kedar were traders with you; they provided you with lambs, rams and goats.
22 Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
The traders of Sheba and Raamah came to sell you the best of every spice and in all kinds of precious gems; they traded gold for your merchandise.
23 Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
Haran, Kanneh, and Eden were traders with you, along with Sheba, Ashur, and Kilmad.
24 Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
These were your dealers in ornate robes of violet cloths with woven colors, and in blankets of multicolored, embroidered, and well-woven cloth in your marketplaces.
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
The ships of Tarshish were the transporters of your merchandise! So you were filled up, heavily laden with cargo in the heart of the seas!
26 Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
Your rowers have brought you into vast seas; the eastern wind has broken you in the middle of them.
27 Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
Your wealth, merchandise, and trade goods; your sailors and pilots, and ship builders; your traders of merchandise and all the men of war who are in you, and all your crew—they will sink into the depths of the sea on the day of your destruction.
28 Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
Cities at the sea will tremble at the sound of your pilots' cry;
29 Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
All those who handle oars will come down from their ships; mariners and all the pilots on the sea will stand on the land.
30 Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
Then they will make you listen to their voice and will wail bitterly; they will cast dust up on their heads. They will roll about in ashes.
31 Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
They will shave their heads bald for you and bind themselves with sackcloth, and they will weep bitterly over you and they will cry out.
32 Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
They will lift up their wails of lamentation for you and sing dirges over you, Who is like Tyre, who has now been brought to silence in the middle of the sea?
33 Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
When your merchandise went ashore from the sea, it satisfied many peoples; you enriched the kings of the earth with your great wealth and merchandise!
34 Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
But when you were shattered by the seas, by deep waters, your merchandise and all your crew sank!
35 Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
All the inhabitants of the coasts were appalled at you, and their kings shuddered in horror! Their faces trembled!
36 Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”
The merchants of the people hiss at you; you have become a horror, and you will be no more forever.”

< Ezekieli 27 >