< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it was doon in the enleuenthe yeer, in the firste dai of the monethe, the word of the Lord was maad to me, and he seide,
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
Thou, sone of man, for that that Tire seide of Jerusalem, Wel! the yatis of puplis ben brokun, it is turned to me; Y schal be fillid, it is forsakun;
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
therfor the Lord God seith these thingis, Lo! Tire, Y on thee; and Y schal make many folkis to stie to thee, as the see flowynge stieth.
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
And thei schulen distrie the wallis of Tire, and thei schulen distrie the touris therof; and Y schal rase the dust therof fro it, and Y schal yyue it in to a `moost clere stoon.
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
Driyng of nettis schal be in the myddis of the see, for Y spak, seith the Lord God. And Tire schal be in to rauysching to hethene men.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
And the douytris therof that ben in the feeld, schulen be slayn bi swerd; and thei schulen wite, that Y am the Lord.
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
For whi the Lord God seith these thingis, Lo! Y schal brynge to Tire Nabugodonosor, the king of Babiloyne, fro the north, the kyng of kyngis, with horsis, and charis, and knyytis, and with a cumpeny, and greet puple.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
He schal sle bi swerd thi douytris that ben in the feeld, and he schal cumpasse thee with strengthingis, and he schal bere togidere erthe in cumpas. And he schal reise a scheeld ayens thee,
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
and he schal tempre engynes lijc vineres, and engines `that ben clepid wetheris ayens thi wallis; and he schal distrie thi touris bi his armure.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
Bi flowynge of his horsis, the dust of tho schal hile thee; thi wallis schulen be mouyd of the soun of knyytis, and of wheelis, and of charis; whanne he schal entre bi the yatis, as bi entryngis of a citee distried,
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
with the clees of hise horsis he schal defoule alle thi stretis. He shal sle bi swerd thi puple, and thi noble ymagis schulen falle doun in to erthe.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
Thei schulen waste thi richessis, thei schulen rauysche thi marchaundies; and thei schulen distrie thi wallis, and thei schulen distrie thin housis ful clere, and thi stoonys, and thi trees, and thei schulen putte thi dust in the myddis of watris.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
And Y schal make to reste the multitude of thi syngeris, and the sown of thin harpis schal no more be herd;
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
and Y schal yyue thee in to a moost cleer stoon. Thou schalt be driyng of nettis, and thou schalt no more be bildid, for Y the Lord spak, seith the Lord God.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
The Lord God seith these thingis of Tire, Whether ilis schulen not be moued of the sown of thi fal, and of weiling of thi slayn men, whanne thei ben slayn in the myddis of thee?
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
And alle the princis of the see schulen go doun of her seetis, and thei schulen do awei her mentils, ether spuylis of slayn enemyes, and thei schulen caste awei her dyuerse clothis, and shulen be clothid with wondring. Thei shulen sitte in the erthe, and thei shulen be astonyed, and thei shulen wondre of thi sodeyn fal.
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
And thei shulen take weilyng on thee, and schule seie to thee, Hou perischidist thou, noble citee, that dwellist in the see, that were strong in the see with thi dwelleris, whiche dwelleris alle men dredden?
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Now schippis schulen wondre in the dai of thi drede, and ilis in the see schulen be disturblid, for noon goith out of thee.
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
For the Lord God seith these thingis, Whanne Y schal yyue thee a citee desolat, as the citees that ben not enhabitid, and Y schal bringe on thee the depthe of watris, and many watris schulen hile thee.
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
And Y schal drawe thee doun with hem that goon doun in to a lake, to the puple euerlastynge; and Y schal sette thee in the laste lond, as elde wildirnessis, with hem that ben led doun in to a lake, that thou be not enhabited. Certis whanne Y schal yyue glorye in the lond of lyueris,
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
Y schal dryue thee in to nouyt, and thou schalt not be; and thou schalt be souyt, and thou schalt no more be foundun with outen ende, seith the Lord God.

< Ezekieli 26 >