< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came to pass in the eleventh year, on the first of the month, that the word of Yahweh came unto me, saying:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
Son of man, Because Tyre hath said concerning Jerusalem. Aha! She is broken that was the doors of the peoples. She is turned unto me, — I shall be filled, She is laid waste,
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
Therefore, Thus, saith My Lord Yahweh, Behold me! against thee O Tyre, — So then I will bring up against thee many nations, As the sea bringeth up its rolling waves;
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
And they shall destroy the walls of Tyre. And break down her towers, And I will scrape clean her dust from off her, —And make of her the glaring face of a cliff:
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
A place for the spreading of nets, shall she become, in the midst of the sea, For, I, have spoken Declareth My Lord. Yahweh, -And she shall become a prey to the nations.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
And her daughters that are in the field: with the sword shall be slain: So shall they know that I am Yahweh.
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
For thus saith My Lord. Yahweh, Behold me! bringing against Tyre. Nebuchadrezzar king of Babylon out of the North. a king of kings, —with horses and with chariots and with horsemen, and a gathered host, and much people.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
Thy daughters in the field—with the sword, shall he slay, - And shall set against thee a siege-wall And cast up against thee an earthwork, And set up against thee a large shield;
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
And the stroke of his attacking-engine, will he direct against thy walls, — And thy towers, will he break down with his axes.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
By reason of the multitude of his horses, their dust shall cover thee, — At the noise of horseman and wheel and chariot, shall thy walls tremble, when he entereth into thy gates Just as they do who enter a city broken open.
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
With the hoofs of his horses, shall he tread down all thy streets, — Thy people-with the sword, shall he slay, And thy pillars of strength to the earth, shall go down.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
And they shall spoil thy wealth And make a prey of thy merchandise, And break down thy walls And thy pleasant houses, shall they lay in ruins; And thy stones and thy timber and thy dust—in the midst of the waters, shall they lay.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
And I will cause to cease the hum of thy songs; And the sound of thy lyres, shall not be heard any more.
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And I will make of thee the glaring face of a cliff. A place for the spreading of nets, shalt thou become, Thou shalt not be but any more, For I. Yahweh have spoken it, Declareth My Lord Yahweh.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
Thus saith My Lord. Yahweh, to Tyre: Shall it not be that. At the sound of thy fall. With the groan of thy pierced one. With the slaughter made in thy midst, The Coastlands shall tremble?
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
Then shall come down from off their thrones all the princes of the sea, And shall lay aside their robes. And their embroidered garments, shall strip off, — With tremblings, shall they clothe them. selves Upon the ground, shall they sit, And shall tremble every moment and be astonished over thee.
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
Then shall they take up over thee a dirge, And say to thee, - How hast thou perished, And ceased from the seas, - The city renowned which was strong in the sea She and they who dwelt in her, Who imparted their terror To all who dwelt in her.
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Now, shall tremble the Coastlands, In the day of thy fall, - And shall shudder the isles that are in the sea. At thine exit!
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
For thus saith My Lord Yahweh, When I make thee a desolate city, Like cities which cannot be dwelt in, - When I bring up over thee the roaring deep, And the mighty waters cover thee,
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
Then will I bring thee down with them that go down into the pit. Unto the people of age-past times And cause thee to dwell in the earth below Among the desolations from age-past times With them that go down into the pit That thou mayest not be dwelt in, Nor yet present thyself in the land of the living.
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
A terror, will I make thee And thou shalt not be: Though thou be sought for, Thou shalt not be found any more To times age-abiding, Declareth My Lord, Yahweh.

< Ezekieli 26 >