< Ezekieli 23 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
I doszło do mnie słowo PANA mówiące:
2 “Mwanadamu, Kulikuwa na wanawake wawili, binti za mama mmoja.
Synu człowieczy, były dwie kobiety, córki jednej matki;
3 Walifanya ukahaba katika Misri katika kipindi cha ujana wao. Walitenda kama makahaba huko. Maziwa yao yalikuwa yamebana na ubikira wa chuchu zao zilipapaswa huko.
One uprawiały nierząd w Egipcie, w swojej młodości uprawiały nierząd; tam ściskano ich piersi i tam przygniatano piersi ich dziewictwa.
4 Majina yao yalikuwa Ohola-dada mkubwa-na Oholiba-dada yake mdogo. Kisha wakawa wangu na kuzaa wana na binti. Majina yao yalikuwa yakimaanasha hivi: Ohola maana yake Samaria, na Oholiba maana yake Yerusalemu.
A ich imiona: starsza Ohola, a jej siostra – Oholiba. One były moje i urodziły synów i córki. Ich imiona: Samaria to Ohola, a Jerozolima to Oholiba.
5 Lakini Ohola alifanya kama kahaba hata alipokuwa wangu; aliwatamani wapenzi wake, kwa kuwa Waashuri na nguvu,
Ohola uprawiała nierząd, będąc moją, zapałała namiętnością do swoich kochanków, do Asyryjczyków, sąsiadów;
6 liwali aliyekuwa amevaa urijuana, na kwa ajili ya maafisa wake, waliokuwa hodari na wanaume wa kuvutia, wote walikuwa waendesha farasi.
Którzy byli odziani w błękit, dowódcy i rządcy, wszyscy oni to powabni młodzieńcy, jeźdźcy dosiadający koni;
7 Hivyo akajitoa yeye mwenyewe kama kahaba kwao, kwa watu bora wa Ashuru, na alijitia mwenyewe uchafu pamoja na kila mmoja aliyekuwa amemtamani-pamoja na sanamu zake zote.
Popełniała z nimi nierząd, ze wszystkimi najlepszymi synami Asyrii i ze wszystkimi, do których pałała namiętnością; plamiła się wszystkimi ich bożkami.
8 Kwa kuwa hakuacha tabia zake za kihaba nyuma katika Misri, wakati walipolala naye wakati alipokuwa msichana mdogo, wakati walipoanza kwanza kupapasa ubikira wa maziwa yake, wakati walipoanza kummwagia tabia ya uzinzi wao juu yake.
Nie porzuciła też swego nierządu z Egiptu, bo spali z nią w jej młodości, przygniatali piersi jej dziewictwa i wylali na nią swój nierząd.
9 Kwa hiyo nilimtia kwenye mkono wa wapenzi wake, kwenye mkono wa Waashuru kwa kuwa aliwatamani.
Dlatego wydałem ją w ręce jej kochanków, w ręce Asyryjczyków, do których pałała namiętnością.
10 Wakamfunua uchi wake. Wakawachukua wana wake na binti, na wakamuua kwa upanga, na akawa aibu kwa wanawake wengine, hivyo wakapitisha hukumu juu yake.
Oni odsłonili jej nagość, zabrali jej synów i córki, a ją samą zabili mieczem. I stała się osławiona wśród kobiet, gdy wykonano na niej sąd.
11 Dada yake Oholiba akaliona hili, lakini aliyatamani zaidi na kufanya kama kahaba hata zaidi kuliko dada yake.
A choć widziała to jej siostra Oholiba, bardziej niż ona zapałała [rozwiązłą] miłością, a jej nierząd był [jeszcze] większy niż nierząd jej siostry.
12 Aliwatamanai Waashuru, mabosi na watawala waliokuwa wamevaa ngua za ushawishi, walikuwa watu waendesha farasi. Wote walikuwa hodari, wote vijana wa kuvutia.
Do swych sąsiadów Asyryjczyków pałała namiętnością, do dowódców i rządców, i władców, ubranych w kosztowne szaty, do jeźdźców dosiadających konie, wszyscy oni to powabni młodzieńcy.
13 Nikaona kwamba alikuwa amefanya uchafu mwenyewe. Ilikuwa kama kwa wadada wote.
I widziałem, że się hańbiła [i że] obydwie [kroczyły] tą samą drogą.
14 Kisha akaongeza ukahaba wake tena zaidi. Aliona watu waume waliokuwa wamechorwa juu ya kuta, michoro ya Wakaldayo iliyochorwa kwa rangi nyekundu,
Ale ta posunęła się jeszcze dalej w swoich nierządnych czynach, bo widząc mężczyzn wymalowanych na ścianie, obrazy Chaldejczyków malowane farbami;
15 waliovaa mikanda kuzunguka viuno vyao, na vilemba virefu juu ya vichwa vyao. Wote walikuwa na mwonekano wa maafisa wa jeshi la waendesha farasi, mfano wa wana wa Wababeli, ambao asili ya nchi ni Ukaldayo.
Opasanych wokół bioder pasami, z zawojami ufarbowanymi na głowach – [a] wszyscy oni z wyglądu jak bohaterowie, podobni do Babilończyków pochodzących z ziemi Chaldei;
16 Na mara macho yake yalipowaona, aliwatamani, hivyo akawatuma wajumbe wake kwao katika Ukaldayo.
Pałała do nich namiętnością, jak tylko spojrzała na nich swymi oczami, i wyprawiła do nich posłańców, do Chaldei.
17 Kisha Wababeli wakaja katika kitanda chake cha tamaa, na walimfanya unajisi kwa uzinzi wao. Kwa kile alichokuwa amekifanya alifanya unajisi, basi akageuka mwenyewe kutoka kwao katika karaha.
Wtedy Babilończycy weszli do niej, na łoże miłości, i plamili ją swoim nierządem; a gdy się skalała z nimi, jej dusza odwróciła się od nich.
18 Alionyesha matendo yake ya ukahaba na alionyesha uchi wake, hivyo roho yangu ikagauka kutoka kwake, kama roho yangu ilivyogeuka kutoka kwa dada yake.
I gdy ujawniła swoje czyny nierządne i odsłoniła swoją nagość, moja dusza odwróciła się od niej, tak jak odwróciła się moja dusza od jej siostry.
19 Kisha alifanya matendo mengi zaidi ya ukahaba, akakumbuka na kutafakari siku za ujana wake, wakati alipotenda kama kahaba katika nchi ya Misri.
Lecz ona mnożyła swoje czyny nierządne, przypominając sobie dni swojej młodości, kiedy uprawiała nierząd w ziemi Egiptu.
20 Basi akawatamani wapenzi wake, ambao sehemu zao za siri zilikuwa kama zile za punda, na kile kizaliwacho hutoka kilikuwa kama wale farasi.
I pałała namiętnością do ich kochanków, których ciała [są jak] ciała osłów, a ich wytrysk jak wytrysk koni.
21 Hivi ndivyo ulivyofanya matendo ya aibu ya ujana wako, wakati Wamisri walipopapasa chuchu zako kuyaminya maziwa ya ujana wako.
Tak powróciłaś do rozwiązłości swojej młodości, gdy Egipcjanie przygniatali twoje piersi dla piersi twojej młodości.
22 Kwa hiyo, Oholiba, Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Nitawarudisha wapenzi wako dhidi yako. Wale ambao uliowarudisha, nitawaleta juu yako kutoka kila upande.
Dlatego, Oholibo, tak mówi Pan BÓG: Oto pobudzę przeciwko tobie twoich kochanków, tych, od których odwróciła się twoja dusza, i sprowadzę ich zewsząd przeciwko tobie;
23 Wababeli na Wakaldayo wote, Pekodi, Shoa, na Koa, na Waashuru wote pamoja nao, hodari, vijana wa kutamanika, magavana na maamiri jeshi, wote ni maafisa na watu wote wenye sifa, wote wenye kuendesha farasi.
Babilończyków, wszystkich Chaldejczyków, Pekod, Szoa, Koa, a z nimi wszystkich Asyryjczyków. Oni wszyscy to powabni młodzieńcy, dowódcy i rządcy, dostojnicy i zacni [ludzie], wszyscy jeżdżący na koniach.
24 Watakuja juu yako kwa silaha, na kwa magari ya farasi na mikokoteni, na kundi kubwa la watu. Watapanga ngao kubwa, ngao ndogo, na kofia za chuma juu yako pande zote. Nitawapatia nafasi kukuadhibu, na watakuadhibu kwa matendo yao.
I wyruszą przeciwko tobie na rydwanach, na wozach żelaznych, na furmankach i z gromadą narodów. Zewsząd rozłożą się przeciwko tobie z puklerzami, tarczami i hełmami. I dam im prawo, aby cię sądzili według swoich praw.
25 Kwa kuwa nitaweka hasira yangu ya wivu juu yako, na watashughulika na wewe kwa hasira. Watakukatilia mbali pua zako na masikio yako, na masalia yako wataanguka kwa upanga. Watawachukua wana wako na binti zako, na masalia yako watateketea kwa moto.
I wyleję na ciebie swoją zazdrość, i obejdą się z tobą z gniewem. Odetną ci nos i uszy, a twoja resztka polegnie od miecza. Wezmą twoich synów i twoje córki, a to, co z ciebie zostanie, strawi ogień.
26 Watakuvua nguo zako na kuchukua mapambo yako ya vito.
I zdejmą z ciebie twoje szaty, i zabiorą ci twoje piękne klejnoty.
27 Hivyo nitaiondoa tabia yako ya aibu kutoka kwako na matendo yako ya kikahaba kutoka nchi ya Misri. Hutainua macho yako kuwaelekea kwa sahauku, na hutaikumbuka Misri tena.'
Tak położę kres twojej rozwiązłości i twojemu nierządowi, [które przyniosłaś] z ziemi Egiptu. Nie podniesiesz [już] ku nim swych oczu ani nie będziesz więcej wspominać Egiptu.
28 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Nitakutia katika mkono wa wale uwachukiao, kukurudisha kwenye mkono wa wale ambao uliokuwa umewarudisha.
Tak bowiem mówi Pan BÓG: Oto wydam cię w ręce tych, których nienawidzisz, w ręce tych, od których odwróciła się twoja dusza.
29 Watashughulika pamoja nawe kwa chuki; watachukua milki zako zote na kukutelekeza uchi na kukuweka wazi. Uchi wa aibu ya ukahaba wako utafunuliwa, tabia yako ya aibu na uzinzi wako.
I postąpią z tobą z nienawiścią, zabiorą ci cały twój dorobek, zostawią cię nagą i obnażoną i zostaną odkryte nagość twego nierządu, twoja rozwiązłość i twoje czyny nierządne.
30 Haya mambo yatafanyika kwako kwa kuwa umetenda kama kahaba, tamaa za mataifa kwazo umetiwa unajisi kwa sanamu zao.
To ci się przydarzy, dlatego że uprawiałaś nierząd, naśladując pogan; dlatego że skalałaś się ich bożkami.
31 Umetembea katika njia za dada yako, hivyo nitaweka kikombe chake cha adhabu kwenye mkono wako.'
Chodziłaś drogą swojej siostry, dlatego dam jej kielich w twoją rękę.
32 Bwana Yahwe asema hivi, 'Utakinywea kikombe cha dada yako ambacho ni kirefu na kikubwa. Utakuwa dhihaka na kutawaliwa na dharau-hiki kikombe kimejaa kiasi kikubwa.
Tak mówi Pan BÓG: Będziesz pić z kielicha swojej siostry, głębokiego i szerokiego, będziesz pośmiewiskiem i szyderstwem, bo on wiele zmieści.
33 Utajazwa kwa ulevi na huzuni, kikombe cha ushangao na uharibifu; kikombe cha dada yako Samaria.
Będziesz napełniona pijaństwem i bólem, kielichem spustoszenia i smutku, kielichem twojej siostry Samarii.
34 Utakinywea na kubakia kitupu; kisha utakivunja vunja na kuyararua maziwa yako kuwa vipande vipande. Kwa kuwa nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
Wypijesz go i wychylisz do dna, potem go rozbijesz na kawałki, a swoje piersi poobrywasz. Ja bowiem to powiedziałem, mówi Pan BÓG.
35 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu umenisahau na kunitupa mbali nyumba ya mgongo wako, basi pia utachukua matokeo ya tabia zako za aibu na matendo ya uasherati.”'
Dlatego tak mówi Pan BÓG: Ponieważ zapomniałaś o mnie i rzuciłaś mnie za swoje plecy, ty także znoś swoją rozwiązłość i swój nierząd.
36 Yahwe akanambia, “Mwanadamu, Je! utamhukumu Ohola na Oholiba? Basi waambie matendo yao ya machukizo,
I PAN powiedział do mnie: Synu człowieczy, czy będziesz sądził Oholę i Oholibę? Uświadom im ich obrzydliwości;
37 kwa kuwa wamefanya uzinzi, na kwa kuwa kuna damu juu ya vichwa vyao. Wamefanya uzinzi na sanamu zao, na wamewaweka hata wana wao kwenye moto, kama chakula cha sanamu zao.
Że cudzołożyły i krew jest na ich rękach; z bożkami cudzołożyły, także swych synów, których mi urodziły, przeprowadziły [przez ogień], by byli strawieni.
38 Kisha waliendelea kufanya hivi kwa ajili yangu: Wamepafanya patakatifu pangu unajisi, na katika siku hiyo hiyo wakainajisi Sabato zangu.
I jeszcze to mi uczyniły, że moją świątynię splugawiły w tym samym dniu i zbezcześciły moje szabaty.
39 Kwa kuwa walipokuwa wamewachinjia watoto wao kwa ajili ya sanamu zao, kisha wakaja hata patakatifu pangu siku hiyo hiyo kupanajisi! Hivyo tazama! Hivi ndivyo walivyofanya kati ya nyumba yangu.
Gdy bowiem zabiły swoje dzieci dla swoich bożków, wchodziły do mojej świątyni w tym samym dniu, aby ją zbezcześcić; oto tak czyniły wewnątrz mego domu.
40 Mmewatuma watu kutoka mbali, ambao wajumbe waliwatuma-sasa tazama. Wakaja kweli, ambao uliojiosha kwa ajili yao, uliweka rangi macho yako, na kujipamba kwa mapambo ya vito.
Ponadto posyłały po mężczyzn, aby przyszli z daleka; wysłano więc posłańca, a oni przyszli. Dla nich się myłaś, barwiłaś swoje oczy i stroiłaś się w ozdoby;
41 Huko ulikaa kwenye kitanda kizuri na kwenye meza iliyokuwa imepangwa mbele yake ulikuwa umeweka ubani na mafuta yangu.
Siadałaś na wspaniałym łożu, przed którym był przygotowany stół i na którym kładłaś moje kadzidło i mój olejek.
42 Hivyo sauti za watu zilikuwa zimemzunguka; pamoja na watu wa kila aina, hata walevi waliletwa kutoka jangwani, na wakawavalisha vikuku mikononi mwao na mataji mazuri juu ya vichwa vyao.
I rozległ się u niej głos beztroskiego tłumu, a wraz z ludem pospolitym przyprowadzono z pustyni Sabejczyków, którzy wkładali bransolety na ich ręce i ozdobne korony na ich głowy.
43 Kisha nikasema juu yake aliyekuwa ameonywa kwa uzinzi, 'Sasa watazini pamoja naye, na yeye pamoja nao.'
I powiedziałem do tej cudzołożnicy zestarzałej: Czy oni będą uprawiać nierząd z nią, a ona z nimi?
44 Wakamwingilia na kulala naye kama watu wamwingiliavyo kahaba. Katika njia hii walilala Ohola na Oholiba, waliokuwa wanawake wazinzi.
I obcowali z nią, jak się obcuje z nierządnicą. Tak właśnie obcowali z Oholą i Oholibą, kobietami rozwiązłymi.
45 Lakini watu wenye haki watapitisha hukumu na kuwaadhibu kama wazinzi, na watawaadhibu kwa hukumu kwa wale wamwagao damu, kwa sababu wao ni wazinzi na damu iko mikononi mwao.
Dlatego mężowie sprawiedliwi będą je sądzić, jak się sądzi cudzołożnice i jak się sądzi przelewających krew, gdyż one są cudzołożnicami, a krew jest na ich rękach.
46 Hivyo Bwana Yahwe asema hivi: Nitainua kundi la watu juu yao na kuwatoa kuwa kitisho na kuteka nyara.
Tak bowiem mówi Pan BÓG: Sprowadzę na nie wojsko i wydam je na wysiedlenie i na łup.
47 Kisha hilo kundi la watu litawapiga kwa mawe na kuwakatilia chini kwa panga zao. Watawaua wana wao na binti na kuzichoma nyumba zao.
I ta gromada ukamienuje je, i rozsiecze swymi mieczami, zabije ich synów i córki, a ich domy spali ogniem.
48 Kwa kuwa nitaondoa tabia ya aibu kutoka kwenye nchi na nidhamu wanawake wote hivyo hawatatenda kama makahaba.
Tak usunę rozwiązłość z tej ziemi, aby wszystkie kobiety otrzymały ostrzeżenie i nie czyniły według waszej rozwiązłości.
49 Hivyo wataweka tabia yenu ya aibu juu yenu. Mtachukua hatia ya dhambi zenu pamoja na sanamu zenu, na kwa njia hii mtajua yakuwa mimi ni Bwana Yahwe.”
I będzie nałożona na was wasza rozwiązłość, i poniesiecie grzechy waszych bożków. I poznacie, że ja jestem Panem BOGIEM.

< Ezekieli 23 >