< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
Moreover the Spirit took me up, and brought me to the front gate of the house of the Lord, that looks eastward: and behold at the entrance of the gate were about five and twenty men; and I saw in the midst of them Jechonias the son of Ezer, and Phaltias the son of Banaeas, the leaders of the people.
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
And the Lord said to me, Son of man, these are the men that devise vanities, and take evil counsel in this city:
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
who say, Have not the houses been newly built? This is the caldron, and we are the flesh.
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
Therefore prophesy against them, prophesy, son of man.
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
And the Spirit of the Lord fell upon me, and said to me, say; Thus saith the Lord; Thus have ye said, O house of Israel: and I know the devices of your spirit.
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
Ye have multiplied your dead in this city, and ye have filled your ways with slain men.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Therefore thus saith the Lord; Your dead whom ye have smitten in the midst of it, these are the flesh, and this[city] is the caldron: but I will bring you forth out of the midst of it.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
Ye fear the sword; and I will bring a sword upon you, saith the Lord.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
And I will bring you forth out of the midst of it, and will deliver you into the hands of strangers, and will execute judgments among you.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Ye shall fall by the sword; I will judge you on the mountains of Israel; and ye shall know that I am the Lord.
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
And it came to pass, while I was prophesying, that Phaltias the son of Banaeas died. And I fell upon my face, and cried with a loud voice, and said, Alas, alas, O Lord! wilt thou utterly destroy the remnant of Israel?
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of the Lord came to me, saying,
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
Son of man, thy brethren, and the men of thy captivity, and all the house of Israel are come to the full, to whom the inhabitants of Jerusalem said, Keep ye far away from the Lord: the land is given to us for an inheritance.
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
Therefore say thou, Thus saith the Lord; I will cast them off among the nations, and will disperse them into every land, yet will I be to them for a little sanctuary in the countries which they shall enter.
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
Therefore say thou, Thus saith the Lord; I will also take them from the heathen, and gather them out of the lands wherein I have scattered them, and will give them the land of Israel.
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
And they shall enter in there, and shall remove all the abominations of it, and all its iniquities from it.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
And I will give them another heart, and will put a new spirit within them; and will extract the heart of stone from their flesh, and give them a heart of flesh:
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
that they may walk in my commandments, and keep mine ordinances, and do them: and they shall be to me a people, and I will be to them a God.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
And as for the heart [set upon] their abominations and their iniquities, as their heart went [after them], I have recompensed their ways on their heads, saith the Lord.
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Then the cherubs lifted up their wings, and the wheels beside them; and the glory of the God of Israel was over them above.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
And the glory of the Lord went up from the midst of the city, and stood on the mountain which was in front of the city.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
And the Spirit took me up, and brought me to the land of the Chaldeans, to the captivity, in a vision by the Spirit of God: and I went up after the vision which I saw.
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
And I spoke to the captivity all the words of the Lord which he had shewed me.

< Ezekieli 11 >