< Kutoka 7 >

1 Yahweh akasema na Musa, “Ona, nimekufanya kama mungu kwa Farao. Aruni kaka yako atakuwa nabii wako.
Yahweh said to Moses, “See, I have made you like a god to Pharaoh. Aaron your brother will be your prophet.
2 Utasema kila kitu nitacho kuamuru kusema. Aruni kaka yako ata sema na Farao iliawaachie watu wa Israeli watoke kwenye nchi yake.
You will say everything that I command you to say. Aaron your brother will speak to Pharaoh so that he will let the people of Israel go from his land.
3 Lakini nitaufanya moyo wa Farao mgumu, na nitaonyesha ishara nyingi za nguvu zangu, maajabu mengi, katika nchi ya Misri.
But I will harden Pharaoh's heart, and I will display many signs of my power, many wonders, in the land of Egypt.
4 Lakini Farao hata kusikiliza, kwahiyo nitaueka mkono wangu juu ya Misri na kutoa makundi yangu ya wanaume wapiganaji, watu wangu, wazao wa Israeli, watoke nchi ya Misri kwa matendo makubwa ya hukumu.
But Pharaoh will not listen to you, so I will put my hand on Egypt and bring out my groups of fighting men, my people, the descendants of Israel, out of the land of Egypt by great acts of punishment.
5 Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitapo nyoosha mkono wangu kwa Misri na kuwatoa Waisraeli kutoka miongoni mwao.”
The Egyptians will know that I am Yahweh when I reach out with my hand on Egypt and bring out the Israelites from among them.”
6 Musa na Aruni wakafanya hivyo; walifanya kama Yahweh alivyo waamuru.
Moses and Aaron did so; they did just as Yahweh commanded them.
7 Musa alikuwa na miaka themanini, na Aruni miaka themanini na tatu walipo ongea na Farao.
Moses was eighty years old, and Aaron eighty-three years old when they spoke to Pharaoh.
8 Yahweh akamwambia Musa na Aruni,
Yahweh said to Moses and to Aaron,
9 “Wakati Farao atakapo waambia, 'Fanya muujiza,' utamwambia Aruni, 'Chukuwa gongo lako na ulirushe chini mbele ya Farao, ililigeuke nyoka.”'
“When Pharaoh says to you, 'Do a miracle,' then you will say to Aaron, 'Take your staff and throw it down before Pharaoh, so that it may become a snake.'”
10 Kisha Musa na Aruni wakaenda kwa Farao, na wakafanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni akarusha chini gongo lake mbele ya Farao na watumishi wake, na likageuka nyoka.
Then Moses and Aaron went to Pharaoh, and they did just as Yahweh had commanded. Aaron threw down his staff before Pharaoh and his servants, and it became a snake.
11 Kisha naye Farao akawaita wazee wenye hekima na wachawi. Wakafanya jambo hilo hilo kwa uchawi wao.
Then Pharaoh also called for his wise men and sorcerers. They did the same thing by their magic.
12 Kila mtu akarusha chini gongo lake, na magongo yakawa nyoka. Lakini gongo la Aruni lilimeza nyoka zao.
Each man threw down his staff, and the staffs became snakes. But Aaron's staff swallowed up their snakes.
13 Moyo wa Farao ulikuwa mgumu, na akusikiliza, kama Yahweh alivyo tabiri.
Pharaoh's heart was hardened, and he did not listen, just as Yahweh had foretold.
14 Yahweh akasema na Musa, “Moyo wa Farao ni mgumu, na anakataa kuacha watu waende.
Yahweh said to Moses, “Pharaoh's heart is hard, and he refuses to let the people go.
15 Nenda kwa Farao asubui anapoenda kwenye maji. Simama kwenye chanzo cha mto kukutana naye, na uchukuwe mkononi mwako gongo ambalo liligeuka nyoka.
Go to Pharaoh in the morning when he goes out to the water. Stand on the riverbank to meet him, and take in your hand the staff that had turned into a snake.
16 Mwambie, 'Yahweh, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, “Acha watu wangu waende, iliwaniabudu nyikani. Mpaka sasa haujanisikiliza.”
Say to him, 'Yahweh, the God of the Hebrews, has sent me to you to say, “Let my people go, so that they may worship me in the wilderness. Until now you have not listened.”
17 Yahweh anasema hili: “Kwa hili utajua kuwa mimi ni Yahweh. Ninaenda kupiga maji ya mto wa Misri kwa gongo langu lililo mikono mwangu, na mto utageuzwa kuwa damu.
Yahweh says this: “By this you will know that I am Yahweh. I am going to strike the water of the Nile River with the staff that is in my hand, and the river will be turned to blood.
18 Samaki walio kwenye mto watakufa, na mto utanuka. Wa Misri Hawataweza kunywa maji yalio kwenye mto.”'''
The fish that are in the river will die, and the river will stink. The Egyptians will not be able to drink water from the river.”'”
19 Kisha Yahweh akasema na Musa, “Mwambie Aruni, 'Chukuwa gongo lako na unyooshe mkono kwenye maji ya Misri, na juu ya mito yake, mifereji, visima, na madimbwi yote, ili maji yao ya damu. Fanya hivi ilikuwe na damu nchi nzima ya Misri, hadi kwenye vyombo vyote vya mbao na mawe.”'
Then Yahweh said to Moses, “Say to Aaron, 'Take your staff and reach out with your hand over the waters of Egypt, and over their rivers, streams, pools, and all their ponds, so that their water may become blood. Do this so that there will be blood throughout all the land of Egypt, even in containers of wood and stone.'”
20 Musa na Aruni walifanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni alinyanyua gongo na kupiga maji ya mto, machoni pa Farao na watumishi wake. Maji yote kwenye mto yaligeuga damu.
Moses and Aaron did as Yahweh commanded. Aaron raised the staff and struck the water in the river, in the sight of Pharaoh and his servants. All the water in the river turned to blood.
21 Samaki kwenye mto wakafa, na mto ukaanza kunuka. Wamisri hawakuweza kunywa maji kwenye mto, na damu ilikuwa kila mahali katika nchii ya Misri.
The fish in the river died, and the river began to stink. The Egyptians could not drink water from the river, and the blood was everywhere in the land of Egypt.
22 Lakini wachawi walifanya vivyo hivyo na uchawi wao. Kwaiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, na akakataa kuwasikiliza Musa na Aruni, kama Yahweh alivyo sema itatokea.
But the magicians of Egypt did the same thing with their magic. So Pharaoh's heart was hardened, and he refused to listen to Moses and Aaron, just as Yahweh had said would happen.
23 Kisha Farao akarudi na kwenda nyumbani kwake. Wala hakutilia maanani hili.
Then Pharaoh turned and went into his house. He did not even pay attention to this.
24 Wamisri wote walichimba pembeni ya mto kwa ajili ya maji ya kunywa, lakini hawakuweza kunywa maji ya mto.
All the Egyptians dug around the river for water to drink, but they could not drink the water of the river itself.
25 Siku saba zilipita baada ya Yahweh kushambulia mto.
Seven days passed after Yahweh had attacked the river.

< Kutoka 7 >