< Kutoka 40 >

1 Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
Then spake Yahweh unto Moses, saying—
2 “Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
On the first day of the month, in the first month, shalt thou rear the habitation, of the tent of meeting;
3 Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
and thou shalt put therein, the ark of the testimony, —and shalt screen the ark with the veil;
4 Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
and thou shalt bring in the table, and set in order what is to be arranged thereupon, —and thou shalt bring in the lampstand, and mount the lamps thereof;
5 Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
and thou shalt place the altar of gold for incense, before the ark of the testimony, —and put up the screen for the opening of the habitation;
6 Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
and thou shalt place the altar for the ascending-sacrifice, —before the opening of the habitation of the tent of meeting;
7 Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
and thou shalt place the laver between the tent of meeting, and the altar, and shalt put therein water,
8 Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
And thou shalt put up the court round about, and hang up the screen of the gate of the court.
9 Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
And thou shalt take the oil of anointing, and anoint the habitation and all that is therein, —and shalt hallow it. and all the furniture thereof so shall it be holy.
10 Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
And thou shalt anoint the altar of ascending sacrifice, and all its utensils, —and hallow the altar, so shall the altar be most holy:
11 Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
and thou shalt anoint the laver and its stand, —and shalt hallow it.
12 Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
And thou shalt bring near Aaron and his sons, unto the opening of the tent of meeting, —and shalt bathe them in the water;
13 Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
and thou shalt clothe Aaron with the holy garments, —and shalt anoint him and hallow him so shall he minister as priest unto me.
14 Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
His sons also, shalt thou bring near, —and shalt clothe them with tunics;
15 Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
and shalt anoint them as thou didst anoint their father, and they shall minister as priests unto me, —so shall their anointing remain to them for an age-abiding priesthood, to their generations.
16 Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
And Moses did, —according to all that Yahweh had commanded him, so did he.
17 Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
Thus came it to pass, in the first month, in the second year, on the first of the month, that the habitation was reared.
18 Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
Yea Moses reared the habitation, and placed its sockets, and fixed its boards, and fastened its bars, —and reared its pillars.
19 Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
Then spread he abroad the tent upon the habitation, and put the covering of the tent upon it, above, —As Yahweh commanded Moses.
20 Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
And he took and placed the testimony within the ark, and put the staves upon the ark, —and placed the propitiatory upon the ark, above;
21 Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
and brought in the ark into the habitation, and put up the screening veil, and screened over the ark of the testimony, —As Yahweh commanded Moses.
22 Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
And he placed the table in the tent of meeting, —on the side of the habitation northward, —outside the veil;
23 Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
and set in order thereupon the arrangement of bread before Yahweh, —As Yahweh commanded Moses.
24 Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
And he put the lampstand, in the tent of meeting, over against the table, —on the side of the habitation southward;
25 Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
and mounted the lamps before Yahweh, —As Yahweh commanded Moses.
26 Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
And he put the altar of gold in the tent of meeting, —before the veil;
27 Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
and burned thereupon the fragrant incense, —As Yahweh commanded Moses.
28 Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
And he put up the screen of the entrance pertaining to the habitation;
29 Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
and, the altar of ascending-sacrifice, put he at the entrance of the habitation of the tent of meeting, —and he caused to ascend thereupon the ascending-sacrifice, and the meal-offering, —As Yahweh commanded Moses.
30 Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
And he put the laver, between the tent of meeting, and the altar, —and put therein water for bathing;
31 Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
and Moses and Aaron and his sons thenceforth bathed thereat, —their hands and their feet;
32 muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
when they were entering into the tent of meeting, and when they were drawing near unto the altar, then used they to bathe, —As Yahweh commanded Moses.
33 Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
And he reared the court round about to the habitation and to the altar, and put up the screen of the gate of the court, —and Moses finished the work.
34 Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
Then did the cloud cover the tent of meeting, —and, the glory of Yahweh, filled the habitation;
35 Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
and Moses was not able to enter into the tent of meeting, because the cloud had made its habitation thereupon, —and the glory of Yahweh, filled the habitation.
36 Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
And whensoever the cloud ascended from off the habitation, then did the sons of Israel set forward, in all their journeyings;
37 Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
but if the cloud did not ascend, then did they not set forward—until the day when it did ascend.
38 Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.
For, the cloud of Yahweh, was upon the habitation by day, and, a fire, came to be by night therein, —in the sight of all the house of Israel in all their journeyings.

< Kutoka 40 >