< Kutoka 31 >

1 Yahweh akasema na Musa,
L'Éternel parla aussi à Moïse, en disant:
2 “Angalia, nimemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila ya Yuda
Vois, j'ai appelé par son nom Betsaléel, fils d'Uri, fils de Hur, de la tribu de Juda;
3 Nami nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na mambo ya kazi ya kila aina,
Et je l'ai rempli de l'esprit de Dieu, en intelligence, en industrie et en science, et pour toutes sortes d'ouvrages;
4 ili abuni kazi za ustadi, kuwa fundi wa dhahabu, na wa fedha, na wa shaba,
Pour faire des inventions, pour travailler l'or, l'argent et l'airain,
5 na kukata vito kwa kutiwa mahali, na kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
Pour tailler et enchâsser des pierreries, pour tailler le bois et exécuter toutes sortes d'ouvrages.
6 Tena, nimemchagua, awe pamoja naye Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila ya Dani. Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima, ili wapate kufanya vyote nilivyokuagiza. Hii ni,
Et voici, je lui ai donné pour compagnon Oholiab, fils d'Ahisamac, de la tribu de Dan; et j'ai mis de l'industrie dans le cœur de tout homme intelligent, afin qu'ils fassent tout ce que je t'ai commandé de faire:
7 hema ya kukutania na sanduku la ushuhuda, na kiti cha rehema kilicho juu yake, na vyombo vyote vya Hema;
Le tabernacle d'assignation, l'arche pour le Témoignage et le propitiatoire qui sera dessus, et tous les ustensiles du tabernacle;
8 na meza, na vyombo vyake, na kinara cha taa safi pamoja na vyombo vyake vyote,
La table et ses ustensiles, le chandelier d'or pur et tous ses ustensiles, l'autel du parfum,
9 na madhabahu ya kufukizia uvumba; na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, na birika na tako lake.
L'autel de l'holocauste et tous ses ustensiles, la cuve et sa base;
10 Pia mavazi yenye kufumwa kwa uzuri, na mavazi matakatifu ya Haruni kuhani, na mavazi ya wanawe, ili kutumika katika kazi ya ukuhani.
Les vêtements du service, les vêtements sacrés pour Aaron le sacrificateur, et les vêtements de ses fils pour exercer la sacrificature;
11 Pia mafuta ya kutiwa, na uvumba wa manukato mazuri, kwa ajili ya mahali patakatifu; sawasawa na yote niliyokuagiza ndivyo watakavyofanya wao.
L'huile de l'onction, et le parfum d'aromates pour le sanctuaire. Ils feront selon tout ce que je t'ai commandé.
12 akasema na Musa,
L'Éternel parla encore à Moïse, en disant:
13 “Waambie wana wa Israeli, 'Hakika mtazishika Sabato zangu, kwa kuwa ni ishara kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote; ili mpate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA niwatakasaye ninyi.
Et toi, parle aux enfants d'Israël, et dis: Seulement, vous observerez mes sabbats. Car c'est un signe entre moi et vous, dans toutes vos générations, afin qu'on sache que c'est moi, l'Éternel, qui vous sanctifie.
14 Basi mtaishika hiyo Sabato; kwa kuwa ni takatifu kwenu; kila mtu atakayeitia unajisi hakika yake atauawa; kwa kuwa kila mtu afanyaye kazi katika siku hiyo, nafsi hiyo itakatiliwa mbali na watu wake.
Observez donc le sabbat; car c'est pour vous un jour saint. Ceux qui le profaneront seront punis de mort; si quelqu'un fait une œuvre en ce jour, cette personne-là sera retranchée du milieu de ses peuples.
15 Kazi itafanywa siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, takatifu kwa BWANA; kila mtu atakayefanya kazi yo yote katika siku ya Sabato, hakika yake atauawa.
On travaillera pendant six jours; mais, au septième jour, ce sera le sabbat du repos, consacré à l'Éternel; quiconque fera une œuvre le jour du sabbat, sera puni de mort.
16 Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato. Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele.
Ainsi les enfants d'Israël observeront le sabbat, pour célébrer le sabbat dans toutes leurs générations, comme une alliance perpétuelle.
17 Ni ishara kati ya mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Yahweh alifanya mbingu na nchi, akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.
C'est un signe entre moi et les enfants d'Israël à perpétuité; car l'Éternel a fait en six jours les cieux et la terre, mais au septième jour il a cessé et s'est reposé.
18 Hapo Mungu alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa mkono wake.
Et quand Dieu eut achevé de parler avec Moïse, sur la montagne du Sinaï, il lui donna les deux tables du Témoignage, tables de pierre, écrites du doigt de Dieu.

< Kutoka 31 >