< Kutoka 28 >

1 Umuite Aruni kaka yako na wana wake - Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari - miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Fais aussi approcher de toi, d'entre les enfants d'Israël, Aaron ton frère, avec ses fils, pour exercer devant moi la sacrificature: Aaron, Nadab et Abihu, Éléazar et Ithamar, fils d'Aaron.
2 Nawe utamfanyia Aruni ndugu yako mavazi matakatifu, kwa utukufu na kwa uzuri.
Et tu feras à Aaron, ton frère, des vêtements sacrés, pour sa gloire et pour son ornement.
3 Nawe utawaambia watu wote wenye moyo wa hekima, niliowajaza na roho ya hekima wamfanyie Aruni mavazi ili kumtakasa anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et tu parleras à tous ceux qui sont intelligents, que j'ai remplis d'un esprit de sagesse, et ils feront les vêtements d'Aaron pour le consacrer, pour qu'il exerce la sacrificature devant moi.
4 Na mavazi watakayoyafanya ni kifuko cha kifuani, na naivera, na joho, na kanzu ya kazi ya urembo, na kilemba, na mshipi; nao watawafanyia Aruni nduguye, na wanawe, mavazi matakatifu ili anitumikie katika kazi ya ukuhani.
Et voici les vêtements qu'ils feront: Le pectoral, l'éphod, la robe, la tunique brodée, la tiare et la ceinture. Ils feront donc des vêtements sacrés à Aaron, ton frère, et à ses fils, pour qu'ils exercent devant moi la sacrificature.
5 Nao wataitwaa dhahabu, na nguo ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu.
Et ils prendront de l'or, de la pourpre, de l'écarlate, du cramoisi et du fin lin.
6 Nao waifanye naivera kwa nyuzi za dhahabu, na za samawi, na za zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa kwa kazi ya mstadi.
Et ils feront l'éphod d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors, en ouvrage d'art.
7 Lazima itakuwa na vipande viwili vya mabegani, vilivyoungana kwenye ncha zake mbili; ili ipate kuunganywa.
Il y aura à ses deux extrémités deux épaulettes qui se joindront; et c'est ainsi qu'il sera joint.
8 Na mshipi wa kazi ya ustadi ulio juu yake, ili kuifunga mahali pake; utakuwa wa kazi kama ile ya naivera, ya vitu vile vile ya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na ya zambarau, na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa.
La ceinture pour l'attacher, qui se mettra par-dessus, sera du même ouvrage et de la même pièce; elle sera d'or, de pourpre, d'écarlate et de fin lin retors.
9 Nawe utatwaa vito viwili vya shohamu, ya rangi ya chani-kiwiti, nawe utachora juu yake majina ya wana wa Israeli;
Et tu prendras deux pierres d'onyx, et tu graveras sur elles les noms des enfants d'Israël:
10 Majina yao sita katika kito kimoja, na majina sita yaliyosalia katika kile kito cha pili, kwa utaratibu wa kuzaliwa kwao.
Six de leurs noms sur une pierre, et les six autres noms sur la seconde pierre, d'après l'ordre de leurs naissances.
11 Kwa kazi mtu mwenye kuchora mawe kama vile muhuri ichorwavyo, utavichora hivi vito viwili, sawasawa na majina ya wana wa Israeli, nawe utavitia katika vijalizo vya dhahabu.
Tu graveras sur les deux pierres, en travail de lapidaire, en gravure de cachet, les noms des enfants d'Israël; tu les enchâsseras dans des chatons d'or.
12 Nawe utavitia vile vito viwili juu ya vipande vya mabegani vya hiyo naivera, viwe vito vya ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli. Naye Aruni atayachukua majina yao mbele za Yahweh juu ya mabega yake mawili ili kuwa ukumbusho.
Et tu mettras les deux pierres sur les épaulettes de l'éphod, comme des pierres de mémorial pour les enfants d'Israël; et Aaron portera leurs noms devant l'Éternel, sur ses deux épaules, en mémorial.
13 Nawe fanya vijalizo viwili vya dhahabu
Tu feras aussi des agrafes d'or,
14 na mikufu miwili ya dhahabu safi; utaifanya iwe mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa; nawe uitie ile mikufu ya kazi ya kusokotwa katika vile vijalizo.
Et deux chaînettes d'or pur, que tu tresseras en forme de cordons, et tu mettras dans les agrafes les chaînettes ainsi tressées.
15 Nawe lazima utafanya kifuko cha kifuani cha hukumu, kazi ya fundi stadi; utakifanya kwa kuiandama ile kazi ya hiyo naivera. Fanya nyuzi za dhahabu, na za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na nyekundu, na kitani safi yenye kusokotwa, ndivyo utakavyokifanya.
Tu feras aussi le pectoral du jugement en ouvrage d'art; tu le feras comme l'ouvrage de l'éphod; tu le feras d'or, de pourpre, d'écarlate, de cramoisi et de fin lin retors.
16 Kitakuwa mraba, tena cha kukunjwa; urefu wake utakuwa shibiri moja, na upana wake shibiri moja.
Il sera carré et double; sa longueur sera d'un empan, et sa largeur d'un empan.
17 Nawe ukijaze viweko vya vito, safu nne za vito; safu moja itakuwa ni akiki, na yakuti ya rangi ya manjano, na baharamani, hivi vitakuwa safu ya kwanza.
Et tu le garniras d'une garniture de pierreries à quatre rangs de pierres: au premier rang, une sardoine, une topaze et une émeraude;
18 Na safu ya pili itakuwa zumaridi, na yakuti samawi, na almasi.
Au second rang une escarboucle, un saphir et une calcédoine;
19 Na safu ya tatu itakuwa hiakintho, na akiki nyekundu, na amethisto.
Au troisième rang, une opale, une agate et une améthyste;
20 Na safu ya nne itakuwa ni zabarajadi, na shohamu, na yaspi. Vito hivyo vitakazwa ndani ya dhahabu kwa kujaa mahali pake.
Et au quatrième rang, un chrysolithe, un onyx et un jaspe. Ces pierres seront enchâssées dans de l'or, dans leurs garnitures.
21 Na vile vito vitakuwa sawasawa na majina ya wana wa Israeli, kumi na viwili, sawasawa na majina yao. Mfano wa kuchora kwa muhuri kila kimoja sawasawa na jina lake, vitakuwa vya hizo kabila kumi na mbili.
Et les pierres, selon les noms des enfants d'Israël, seront au nombre de douze, d'après leurs noms; elles seront pour les douze tribus, chacune d'après son nom, en gravure de cachet.
22 Nawe lazima utie katika kile kifuko cha kifuani mikufu mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa, ya dhahabu safi.
Tu feras aussi, sur le pectoral, des chaînettes, tressées en forme de cordons, en or pur.
23 Nawe utie maduara mawili ya dhahabu katika kile kifuko cha kifuani, na kuzitia hizo pete mbili katika ncha mbili za kifuko cha kifuani.
Puis tu feras sur le pectoral deux anneaux d'or; et tu mettras les deux anneaux aux deux extrémités du pectoral.
24 Nawe utie hiyo mikufu miwili ya dhahabu iliyosokotwa katika zile pete mbili zilizo katika ncha za kifuko cha kifuani.
Et tu mettras les deux cordons d'or aux deux anneaux, aux extrémités du pectoral.
25 Na ncha zile nyingine za hiyo mikufu miwili ya kusokotwa utazitia katika vile vijalizo viwili, na kuvitia katika vile vipande vya mabegani vya naivera upande wa mbele.
Et tu mettras les deux bouts des deux cordons aux deux agrafes; et tu les mettras sur les épaulettes de l'éphod sur le devant.
26 Nawe utafanya viduara vili vya dhahabu, uzitie katika hizo ncha mbili za kifuko cha kifuani, katika ukingo wake.
Tu feras aussi deux autres anneaux d'or, et tu les mettras sur les deux autres extrémités du pectoral, sur le bord qui sera du côté de l'éphod, en dedans.
27 Nawe lazima ufanye viduara vili vya dhahabu, na kuzitia katika vile vipande viwili vya mabegani vya ile naivera chini yake, upande wa mbele, karibu na kifungo chake, juu ya huo mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi.
Et tu feras deux autres anneaux d'or, et tu les mettras aux deux épaulettes de l'éphod par le bas, sur le devant, à côté de l'endroit où il se joint, au-dessus de la ceinture de l'éphod.
28 Nao watakikaza kile kileso kwa vile viduara vyake kwenye viduara za naivera kwa ukanda wa rangi ya samawi, ili kwamba kikae pale juu ya ule mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi, ili kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera.
Et on attachera le pectoral par ses anneaux aux anneaux de l'éphod, avec un cordon de pourpre, afin qu'il tienne sur la ceinture de l'éphod, et que le pectoral ne se détache pas de l'éphod.
29 Na Aruni atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu juu ya moyo wake kwa kufanya maamuzi, hapo atakapoingia ndani ya mahali patakatifu, kuwa ukumbusho mbele yaYahweh daima.
Ainsi Aaron portera les noms des enfants d'Israël, au pectoral du jugement, sur son cœur, quand il entrera dans le lieu saint, pour servir continuellement de mémorial devant l'Éternel.
30 Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo wa Aruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya Yahweh na Aruni atachukua hukumu ya hao wana wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya Yahweh daima.
Et tu mettras sur le pectoral du jugement l'Urim et le Thummim, et ils seront sur le cœur d'Aaron quand il entrera devant l'Éternel; et Aaron portera le jugement des enfants d'Israël sur son cœur, devant l'Éternel, continuellement.
31 Nawe fanya hiyo joho ya naivera ya rangi ya samawi yote.
Tu feras aussi la robe de l'éphod, entièrement de pourpre.
32 Nayo itakuwa na tundu katikati yake kwa kupitisha kichwa; itakuwa na utepe wa kazi ya kusokotwa kuzunguka hilo tundu lake, mfano wa tundu lililo katika kanzu ya chuma, ili lisipasuke.
Et l'ouverture pour passer la tête sera au milieu; il y aura une bordure à son ouverture tout autour, d'ouvrage tissé, comme l'ouverture d'une cotte d'armes, afin qu'elle ne se déchire pas.
33 Nawe katika pindo zake utatia makomamanga ya rangi ya samawi, na ya rangi ya zambarau, na ya rangi nyekundu, kuzunguka pindo zake kotekote; na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga pande zote.
Et tu mettras à ses bords des grenades de pourpre, d'écarlate, et de cramoisi, à ses bords, tout autour; et des clochettes d'or entremêlées, tout autour:
34 Kengele ya dhahabu na komamanga, kengele ya dhahabu na komamanga, katika pindo za joho kuizunguka pande zote.
Une clochette d'or et une grenade, une clochette d'or et une grenade, aux bords de la robe, tout autour.
35 Nayo itakuwa juu ya Aruni akitumika; na sauti ya hizo kengele itasikilikana hapo aingiapo ndani ya mahali patakatifu mbele ya Yahweh na hapo atokapo nje, ili kwamba asife.
Or, Aaron en sera revêtu pour faire le service; et on en entendra le son, quand il entrera dans le lieu saint devant l'Éternel, et quand il en sortira; et il ne mourra point.
36 Nawe fanya bamba la dhahabu safi na kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri, “Mtakatifu kwa Yahweh.”
Tu feras aussi une lame d'or pur, sur laquelle tu graveras, en gravure de cachet: SAINTETÉ A L'ÉTERNEL.
37 Nawe ulitie hilo bamba katika ukanda wa rangi ya samawi, nalo litakuwa katika kile kilemba; litakuwa upande wa mbele wa kile kilemba.
Tu la mettras sur un cordon de pourpre; elle sera sur la tiare, sur le devant de la tiare;
38 Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Aruni, na Aruni atauchukua uovu wa vile vitu vitakatifu, watakavyovitakasa hao wana wa Israeli katika vipawa vyao vyote vitakatifu, nalo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote, ili kwamba vipate kukubaliwa mbele za Yahweh.
Et elle sera sur le front d'Aaron; et Aaron portera les iniquités que les enfants d'Israël auront commises dans les saintes oblations qu'ils offriront, dans toutes leurs saintes offrandes; et elle sera sur son front continuellement, pour les rendre agréables devant l'Éternel.
39 Na hiyo kanzu utaifuma ya kitani nzuri ya kazi ya urembo, ufanye na kilemba cha nguo ya kitani nzuri, nawe utafanya mshipi wa kazi ya mwenye kutia taraza.
Tu feras aussi la tunique en tissu de fin lin, et tu feras une tiare de fin lin; mais tu feras la ceinture en ouvrage de broderie.
40 Kisha utafany kanzu kwa ajili ya wana wa Aruni, nawe wafanyie mishipi, wafanyie na kofia kwa utukufu na uzuri.
Tu feras aussi pour les fils d'Aaron des tuniques, des ceintures et des mitres pour leur gloire et pour leur ornement.
41 Nawe mvike huyo nduguye Aruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.
Et tu en revêtiras Aaron, ton frère, et ses fils avec lui; tu les oindras, tu les installeras, et tu les consacreras, afin qu'ils exercent la sacrificature devant moi.
42 Nawe wafanyie suruali za nguo ya kitani, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani.
Fais-leur aussi des caleçons de lin, pour couvrir leur nudité; qu'ils tiennent depuis les reins jusqu'aux cuisses.
43 Aruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake.
Et Aaron et ses fils en seront revêtus quand ils entreront dans le tabernacle d'assignation, ou quand ils approcheront de l'autel, pour faire le service dans le lieu saint, et ils ne seront point coupables, et ne mourront point. C'est une ordonnance perpétuelle pour lui et pour sa postérité après lui.

< Kutoka 28 >