< Kutoka 23 >

1 Haupaswi kutoa taarifa ya uongo kuhusu yeyote. usijiunge na mwanaume muovu kuwa shahidi wa uongo.
Thou shalt not raise a false report: put not thy hand with the wicked to be an unrighteous witness.
2 Haupaswi kufuata umati kufanya uovu, wala kutoa ushahidi ukiwa na umati ili kupotosha haki.
Thou shalt not follow a multitude to [do] evil; neither shalt thou speak in a cause to decline after many to wrest [judgment]:
3 Haupaswi kumpendelea mwanaume maskini kwenye kesi yake.
Neither shalt thou countenance a poor man in his cause.
4 Ukikutana na ng'ombe wa adui wako au punda wake amepotea, lazima umrudishie.
If thou shalt meet thy enemy's ox or his ass going astray, thou shalt surely bring it back to him again.
5 Ukiona punda wa yule anaye kuchukia ameanguka chini na mzigo wake, hauta muacha huyo mtu. Lazima umsaidie na punda wake
If thou shalt see the ass of him that hateth thee lying under his burden, and wouldest forbear to help him, thou shalt surely help with him.
6 Haupaswi kupotosha haki kama yapaswa kwenda kwa watu maskini katika kesi ya mwanaume maskini.
Thou shalt not wrest the judgment of thy poor in his cause.
7 Usijiunge na wengine kufanya shutuma za uongo, na usiue asiye na hatia wala mwenye haki, kwa kuwa sitamuacha muovu.
Keep thee far from a false matter; and the innocent and righteous slay thou not: for I will not justify the wicked.
8 Husiwai chukuwa rushwa, kwa kuwa rushwa inawapofusha wanaoona, na kupotosha maneno ya wakweli.
And thou shalt take no gift: for the gift blindeth the wise, and perverteth the words of the righteous.
9 Haupaswi kumnyanyasa mgeni, kwa kuwa wewe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri.
Also thou shalt not oppress a stranger; for ye know the heart of a stranger, seeing ye were strangers in the land of Egypt.
10 Kwa miaka sita utapanda mbegu kwenye nchi yako na kukusanya mazao yake.
And six years thou shalt sow thy land, and shalt gather in the fruits thereof:
11 Lakini katika mwezi wa saba utaacha hakujalimwa, ili kwamba maskini miongoni mwenu wale. Wanacho acha, wanyama wa porini watakula. Utafanya hivyo na mashamba yenu ya mizabibu na ya mizaituni.
But the seventh [year] thou shalt let it rest and lie still; that the poor of thy people may eat: and what they leave, the beasts of the field shall eat. In like manner thou shalt deal with thy vineyard, [and] with thy olive-yard.
12 Wakati wa siku sita utafanya kazi, lakini siku ta saba utapumzika. Fanya hivi ili ng'ombe na punda wako wapumzike, na ili wana wa watumwa wako wa kike na wageni wapumzike na kupata hauweni.
Six days thou shalt do thy work, and on the seventh day thou shalt rest: that thy ox and thy ass may rest, and the son of thy handmaid, and the stranger, may be refreshed.
13 Kuwa makini kwa kila kitu nilicho kwambia. Husitaje majina ya miungu mingine, wala kuruhusu majina yao kusikika kutoka mdomoni mwako.
And in all [things] that I have said to you be circumspect: and make no mention of the names of other gods, neither let it be heard from thy mouth.
14 Lazima usafiri kusherehekea mara tatu kwa ajili yangu kila mwaka.
Three times thou shalt keep a feast to me in the year.
15 Lazima uadhimishe sherehe ya Mkate usiotiwa Chachu. Kama nilivyo kuamuru, utakula mkate usiotiwa chachu kwa siku saba. Wakati huo, utajitokeza kwangu mwezi wa Abibu, uliowekwa kwa ajili ya kusudi hili. Ni kwa mwezi huu uliyo toka Misri. Lakini usijitokeze kwangu mikono mitupu.
Thou shalt keep the feast of unleavened bread: (thou shalt eat unleavened bread seven days, as I commanded thee, in the time appointed of the month Abib; for in it thou camest out from Egypt: and none shall appear before me empty: )
16 Lazima uadhimishe Sherehe ya Mavuno, matunda ya kwanza ya kazi yako ulipo panda mbegu shambani. Pia lazima uadhimishe Sherehe ya Ukusanyaji wa mwisho wa mwaka, unapo kusanya mazao yako kutoka shambani.
And the feast of harvest, the first-fruits of thy labors, which thou hast sown in the field: and the feast of in-gathering, [which] is in the end of the year, when thou hast gathered in thy labors out of the field.
17 Wanaume wote wako lazima wajitokeze kwa Bwana Yahweh mara tatu kila mwaka.
Three times in the year all thy males shall appear before the LORD God.
18 Haupaswi kutoa damu iliyo tolewa dhabihu kwangu na mkate uliyotiwa hamira. Mafuta kutoka kwa dhabihu za sherehe zangu hayapaswi kubaki usiku wote mpaka asubui.
Thou shalt not offer the blood of my sacrifice with leavened bread; neither shall the fat of my sacrifice remain until the morning.
19 Lazima ulete matunda ya kwanza bora kutoka shambani mwako ndani ya nyumba yangu, nyumba ya Yahweh Mungu wako. Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya.
The first of the first-fruits of thy land thou shalt bring into the house of the LORD thy God. Thou shalt not seethe a kid in his mother's milk.
20 Ninaenda kumleta malaika mbele yako kukuongoza njiani, na kukuleta sehemu niliyo iandaa.
Behold, I send an Angel before thee, to keep thee in the way, and to bring thee into the place which I have prepared.
21 Kuwa makini naye na kumtii.
Beware of him, and obey his voice, provoke him not; for he will not pardon your transgressions: for my name [is] in him.
22 Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe makosa yako. Jina langu liko kwake. Kama hakika ukimtii sauti yake na kufanya kila ninacho kwambia, kisha nitakuwa adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako.
But if thou shalt indeed obey his voice, and do all that I speak; then I will be an enemy to thy enemies, and an adversary to thy adversaries.
23 Malaika mwangu ataenda mbele zako na kukuleta kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanani, Wahivi, na Wayebusi. Nitawaharibu.
For my Angel shall go before thee, and bring thee in to the Amorites, and the Hittites, and the Perizzites, and the Canaanites, [and] the Hivites, and the Jebusites; and I will cut them off.
24 Haupaswi kuinamia miungu yao, kuabudu, au kufanya wanavyo fanya. Badala yake, lazima uwapindue kabisa na kuvunja nguzo zao za mawe vipande vipande.
Thou shalt not bow down to their gods, nor serve them, nor do after their works: but thou shalt utterly overthrow them, and quite break down their images.
25 Lazima umuabudu Yahweh Mungu wako, na atabariki mkate wako na maji. Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.
And ye shall serve the LORD your God, and he will bless thy bread, and thy water; and I will take sickness away from the midst of thee.
26 Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako. Nitawapa maisha marefu.
There shall nothing cast their young, nor be barren, in thy land: I will complete the number of thy days.
27 Nitatuma hofu yangu kwao ambao mnaenda. Nitaua wote mnao kutana nao. Nitafanya maadui zenu wawaogope kwa kugeuza migongo yao kwenu.
I will send my fear before thee, and will destroy all the people to whom thou shalt come, and I will make all thy enemies turn their backs to thee.
28 Nitatuma mavu kwenu watakao fukuza Wahivi, Wakanani, na Wahiti mbele zenu.
And I will send hornets before thee, which shall drive out the Hivite, the Canaanite, and the Hittite from before thee.
29 Sitawaondoa kwenu kwa mwaka mmoja, au nchi itakuwa imetelekezwa, na wanyama wa porini watakuwa wengi kwenu.
I will not drive them out from before thee in one year; lest the land should become desolate, and the beast of the field should multiply against thee.
30 Badala yake, nitawafukuza kidogo kidogo kutoka kwenu mpaka utakapo kuwa umestawi na kurithi nchi.
By little and little I will drive them out from before thee, until thou shalt be increased and inherit the land.
31 Nitatengeneza mipaka yako kutoka Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kutoka nyikani hadi Mto Frati. Nitakupa ushindi juu ya wakazi wote wa nchi. Utawaondoa kutoka kwako mwenyewe.
And I will set thy bounds from the Red sea even to the sea of the Philistines, and from the desert to the river: for I will deliver the inhabitants of the land into your hand; and thou shalt drive them out before thee.
32 Haupaswi kufanya agano na wao au na miungu yao.
Thou shalt make no covenant with them, nor with their gods.
33 Hawapaswi kuishi nchini mwako, au watakufanya ufanya dhambi dhidi yangu. Ukiabudu miungu yao, hakika watakuwa mtego kwako.'”
They shall not dwell in thy land, lest they make thee to sin against me: for if thou shalt serve their gods, it will surely be a snare to thee.

< Kutoka 23 >